punainen-red
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 1,731
- 451
well well said mkuu ukweli ni kwamba muungano huu una kero nyingi kuliko faida therefore tuvunje kama ilivyokuwa east african community ile ya miaka ya 1970 na sasa imerudi kivingine kwani sio dhambi maana wenzetu wamezidi kulalamika ikionekana ipo haja ya kungana tutaungana tena ila kwa sasa tutengane kwa kwelini kweli usiopingika wazanzibar wanadhulumiwa. Kama ni muungano wa kweli wa nchi mbili lazima mgawo uwe sawa nusu kwa nusu. Hapa nina maana watanganyika acheni kuzubaa pazeni sauti kuutafuta uhuru wenu na hazina yenu tanganyika ilikofichwa na hawa wenye akili finyu. Huu muungano huu ni wa kihuni tu. Unaposema muungano wa nchi unazungumzia nchi hizo zimeungana zenye ku- share ya uchumi wao kwa sawa. Tunazungumzia muungano wa mataifa mawili. Lakini uhuni uliopo ni kuwa tuna serkali mbili tu ya muungano na ya zanzibar. Je zanzibar imeungano na serikali ya muungano. Kwa nini watanganyika wanaendelea kuficha umwall wa mambo? Kuna siri gani hapo? Mara utasikia kuna wizara za muungano na zisizo za muungano. Hiilo bunge lisilo la muungano upande mwingine wa muungano linakutana lini kujadiri maendeleo yao kama wazanzibar? Ina maana bunge la muungano ndilo hilo hilo linajadili mambo ya muungano na baadaye hubadilika kama kinyonga huvua gamba wakiwemo wanzanzibar wananza kujadili mambo yasiyo yammuungano kama baraza la wawakilishi zanzibar. Bajeti inapitishwa ya muungno halafu inbadilika automatical kuwa pia ya tanganyika. Ccm acheni unafiki tumegundua ndiyo maana nchi haendelei kwa sababu ya kufanya kazi kwa hofu na unafiki. Jifunze muungano kama wa nchi za kiarabu, ulaya, n.k. Hata nchi zilizoendelea zina muungano lakini nchi kama nchi imebaki na haadhi yake. Wanayo mambo ya muungano yanayoeleweka lakini pia kila nchi inafanya mambo yake bila kuingiliwa. Sio kama muungano wa tanzania uliojaa unafiki na udikiteta. Ndiyo maana wanataka kufanya kama kitu kitakatifu kisichojadiliwa. Muungano gani unakuwa na miaka mingi mamma hii bila. Kufanyiwa evaluation. Umefika wakati kizazi hiki kijadili kwa undani kuona tumefaidikaje na muungano huu. Je inafaa tuendelee na mfumo huu au hapana.
nyeyerere alitabiri hivyo tu ? hata bara alitabiri itakuwa wanyamwezi na wamakua na wachanga na wamasai
Hapo nimekuelewa hasa ya point ya 5 lakini ya 4 kuwa muungano ni bora na mapungufu yake ni kosa kubwa sana ni lazima mapungufu yake yoote yaondolewe tusifanye kitu kwa kujifurahisha sasa halafu baadaye ikawa ugonvi ni lazima tuhakikishe kila kitu ni safi hata mwanangu ajue kuwa ni kitu kizuri wazazi walikiunda, Nyerere na Karume walifanya kazi nzuri ni wajibu wetu kuboresha na si kuvunja, TANGANYIKA ipo na itakuwepo tuuu sababu ndo muunganiko wenyewe huwezi kuitoa.historia, nimesoma japo si sana inaonekana hukunielewa vizuri kwa vile post imekaakaa kaa shairi fulani hivi, laki my point is:
1. Tanganyika ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wakoloni
2. Tanzania ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wazalendo
3. mimi na wingine wenye umri usiofikia miaka 47, tumezaliwa Tanzania na sio Tanganyika
4. muungano ni kielelezo cha umoja wetu na licha ya mapungufu yake, ni bora kuliko kutengana
5. changamoto tuliyonayo ni kuondoa mapungufu yake, iwe ni kwa kuunda serikali moja, tatu au kubaki na mbili za sasa, vyovyote vile, muhimu tuondoe kero zinazohusiana na muungano
kilichotufanya tusindwe kuijenga Tanzania si muungano uliopo, bali masuala mengi tu tunayojadili hapa kila siku kama ufisadi nk. kwa hiyo hata tukiuvunja muungano, tutashindwa kuijenga Tanganyika pia kama hatutapambana na matatizo haya (ufisadi nk)
historia, nimesoma japo si sana inaonekana hukunielewa vizuri kwa vile post imekaakaa kaa shairi fulani hivi, laki my point is:
1. Tanganyika ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wakoloni
2. Tanzania ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wazalendo
3. mimi na wingine wenye umri usiofikia miaka 47, tumezaliwa Tanzania na sio Tanganyika
4. muungano ni kielelezo cha umoja wetu na licha ya mapungufu yake, ni bora kuliko kutengana
5. changamoto tuliyonayo ni kuondoa mapungufu yake, iwe ni kwa kuunda serikali moja, tatu au kubaki na mbili za sasa, vyovyote vile, muhimu tuondoe kero zinazohusiana na muungano
kilichotufanya tusindwe kuijenga Tanzania si muungano uliopo, bali masuala mengi tu tunayojadili hapa kila siku kama ufisadi nk. kwa hiyo hata tukiuvunja muungano, tutashindwa kuijenga Tanganyika pia kama hatutapambana na matatizo haya (ufisadi nk)
wazanzibar siyo kuwa wanatubagua ila wanataka marekebisho kwenye muungano huuu mbona mnajaribu kutoka kwenye matakwa ya wazanzibar, Muungano unatakiwa marekebisho hapo hakuna ubishi wakuu!Alitabiri atakayeanza kumbagua mwenzie dhambi ile haimwachi, ila aliyebaguliwa atabaki salama!
Hapana sisi sio watanganyika kwa kuwa Tanganyika ilikufa toka tarehe 26 aprili 64, hata kama wao ni waznz sisi ni watz tu, tuidumishe tz hata bila znz.
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa Tanganyika,
maana ya neno Tanganyika, siijui,
Tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa tanganyika,
maana ya neno tanganyika, siijui,
tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui
nilizaliwa tanzania,
nilizaliwa afrika
nilizaliwa duniani
nlizaliwa na mwanadamu
kwa hiyo;
mimi ni mtanzania
mimi ni mwafrika
mimi ni mdunia
mimi ni mwanadamu
maana ya tanzania, najua
maana ya afrika, najua
maana ya dunia, najua
maana ya mwandamu, najua
nawauliza wazanzibari,
nini maana ya zanzibari,
nani aliipa jina zanzibari,
kwa nini wajivunie uzanzibari?
Kwa nini wasijivunie utanzania?
we waache tu wazenz waondoke, watanganyika tutaendelea, bali soon wao watakuwa wapemba na unguja, si nyerere alitabiri?
nimependa shairi lako miss j, lakini hata wasoviet walizaliwa na kubatizwa wasovieti hadi 1990 walipojikuta kuwa ni wa-georgia, wa-kazakhstan, wa-azerbaijan, wa-lithuania nk. Muungwana haachi asili. Nia yangu haikuwa kuanzisha thread ya kupinga muungano, bali sipendi kuitwa mbara na ndio maana ninasema sisi sio wabara, ni watanganyika. Ukisema tanganyika ni jina la kikoloni, basi kataa pia majina ya tabora, mwanza, dar es salaam, tanga na mengine mengi yanayopatikana katika ramani iliyochorwa na mkoloni.
Nimependa shairi lako miss j, lakini hata wasoviet walizaliwa na kubatizwa wasovieti hadi 1990 walipojikuta kuwa ni wa-Georgia, wa-Kazakhstan, wa-Azerbaijan, wa-Lithuania nk. Muungwana haachi asili. Nia yangu haikuwa kuanzisha thread ya kupinga muungano, bali sipendi kuitwa mbara na ndio maana ninasema sisi sio wabara, ni watanganyika. Ukisema Tanganyika ni jina la kikoloni, basi kataa pia majina ya Tabora, Mwanza, Dar es salaam, Tanga na mengine mengi yanayopatikana katika ramani iliyochorwa na mkoloni.
Ziliungana Tanganyika na Zanzibar kufanya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Jina refu likawa kero likafupishwa kuwa Tanzania...hatuwezi kuwa watanzania bara. Ni watanganyika.
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa tanganyika,
maana ya neno tanganyika, siijui,
tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui
nilizaliwa tanzania,
nilizaliwa afrika
nilizaliwa duniani
nlizaliwa na mwanadamu
kwa hiyo;
mimi ni mtanzania
mimi ni mwafrika
mimi ni mdunia
mimi ni mwanadamu
maana ya tanzania, najua
maana ya afrika, najua
maana ya dunia, najua
maana ya mwandamu, najua
nawauliza wazanzibari,
nini maana ya zanzibari,
nani aliipa jina zanzibari,
kwa nini wajivunie uzanzibari?
Kwa nini wasijivunie utanzania?
kilicho wazi ni kuwa zanzibar (hata ikiitwa tanzania visiwani) imefanya mabadiliko ya katiba yake ambayo yamezingatia mahitaji na maslahi yake ki-muungano. Isikubalike kuwa tanganyika (hata ikiitwa tanzania bara) isifanye mabadiliko ya katiba yasiyozingatia mahitaji na maslahi ya watu wake. Kuwa na uwakilishi wa 50/50 katika kila jambo ni kupuuza milioni 40 ya watu, huku umuihimu ukipewa kwa idadi ya nchi zilizoungana (nusu kwa nusu eti kwa sababu ni nchi 2 zimeungana). Kuchelewa kufanya mabadiliko ya ki-katiba kusiwe ni udhaifu ambao zanziba wanataka kuutumia sasa. Wa-tanzania bara hawakuhusishwa na mabadiliko ya katiba zanzibar. Lilichukuliwa kama ni swala na ki-siasa zaidi (ccm na cuf).
Hii ndilo kosa ambalo ccm kwa kufahamu au kwa kupuuzia, haikulifanya zaidi. Na ccm isihusike sasa kufanya mabadiliko. Si swala la rais wa kisiasa, ni swala la wananchi ktk ujumla wao, itikadi zao, imani zao, taaluma zao. It's not a political thing but rather socio-economical !!
mimi ni mtanganyika. Faida ya muungano wanaijua ccm-magamba. Kwani malawi/zambia/msumbiji siyo waafrika wenzetu? Kwa nini hatuungani? Waacheni wazenji waende kivyao, kwanza huko kunyonywa wanakosema hakumnufaishi mtanganyika wa kawaida. Waacheni, ikifikia hivyo visiwa vyao vìnamezwa na bahari, kama majirani tutawasaidia mashua wahamie uarabuni.