Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Mimi ni mtanganyika. Faida ya muungano wanaijua ccm-magamba. Kwani Malawi/Zambia/Msumbiji siyo waafrika wenzetu? kwa nini hatuungani? Waacheni wazenji waende kivyao, kwanza huko kunyonywa wanakosema hakumnufaishi Mtanganyika wa kawaida. Waacheni, ikifikia hivyo visiwa vyao vìnamezwa na bahari, kama majirani tutawasaidia mashua wahamie uarabuni.
 
well well said mkuu ukweli ni kwamba muungano huu una kero nyingi kuliko faida therefore tuvunje kama ilivyokuwa east african community ile ya miaka ya 1970 na sasa imerudi kivingine kwani sio dhambi maana wenzetu wamezidi kulalamika ikionekana ipo haja ya kungana tutaungana tena ila kwa sasa tutengane kwa kweli
 
nyeyerere alitabiri hivyo tu ? hata bara alitabiri itakuwa wanyamwezi na wamakua na wachanga na wamasai

Alitabiri atakayeanza kumbagua mwenzie dhambi ile haimwachi, ila aliyebaguliwa atabaki salama!
 
Hapo nimekuelewa hasa ya point ya 5 lakini ya 4 kuwa muungano ni bora na mapungufu yake ni kosa kubwa sana ni lazima mapungufu yake yoote yaondolewe tusifanye kitu kwa kujifurahisha sasa halafu baadaye ikawa ugonvi ni lazima tuhakikishe kila kitu ni safi hata mwanangu ajue kuwa ni kitu kizuri wazazi walikiunda, Nyerere na Karume walifanya kazi nzuri ni wajibu wetu kuboresha na si kuvunja, TANGANYIKA ipo na itakuwepo tuuu sababu ndo muunganiko wenyewe huwezi kuitoa.
 

miss J unachokisema ni kweli kabisa, lakini katika mazingira ambayo upande mmoja wa muungano wenye watu wasiozidi milioni moja (kama takwimu zangu ni sahihi) unataka uwe na haki sawa katika mgawanyo wa mapato na upande wa pili wenye watu zaidi au karibia milioni 40 unadhani hii ni ishara ya kukuza muungano? katika vikao vingi vya kurekebisha mapungufu wazanzibar wameendelea kudai hilo, kwa madai kuwa 5% ya mgao wa income tax wanaopewa ni ndogo na hivyo iwe 50% bila kujali wingi wa watu walio TZ bara.
 
Alitabiri atakayeanza kumbagua mwenzie dhambi ile haimwachi, ila aliyebaguliwa atabaki salama!
wazanzibar siyo kuwa wanatubagua ila wanataka marekebisho kwenye muungano huuu mbona mnajaribu kutoka kwenye matakwa ya wazanzibar, Muungano unatakiwa marekebisho hapo hakuna ubishi wakuu!
 
Hapana sisi sio watanganyika kwa kuwa Tanganyika ilikufa toka tarehe 26 aprili 64, hata kama wao ni waznz sisi ni watz tu, tuidumishe tz hata bila znz.

Mwanakatwe.

Tanganyika ilikufa kivipi?
Kama ilikufa au iliuliwa nani alitenda kosa, uhaini huu?

Halafu Jina Tanzania halikuundwa tarehe 26.April.64.
Jina Tanzania liliundwa miezi kadhaa baadae.
Nalo lina Tan--Tanganyika..Zan...Zanzibar...ia ya kiusanii.
Vipi Tanganyika imekufa?

Sheria ipi imeiua Tanganyika?
Hakuna Muungano unaoziua nchi wanachama wake!!

Mwalimu na CCM kwa miaka mingi sasa wamejaribu kutaka tuisahau Tanganyika lakini mzalendo hawezi kuisahau nchi yake.

Pia ni kawaida Muungano unapovunjika nchi wanachama wa muungano hurudi katika jina la awali.
Je una sababu ya msingi ya kuikataa Tanganyika au utanganyika?
 
Naipenda na kui-miss Tanganyika yangu!!
 
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa Tanganyika,
maana ya neno Tanganyika, siijui,
Tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui

Nimependa shairi lako miss j, lakini hata wasoviet walizaliwa na kubatizwa wasovieti hadi 1990 walipojikuta kuwa ni wa-Georgia, wa-Kazakhstan, wa-Azerbaijan, wa-Lithuania nk. Muungwana haachi asili. Nia yangu haikuwa kuanzisha thread ya kupinga muungano, bali sipendi kuitwa mbara na ndio maana ninasema sisi sio wabara, ni watanganyika. Ukisema Tanganyika ni jina la kikoloni, basi kataa pia majina ya Tabora, Mwanza, Dar es salaam, Tanga na mengine mengi yanayopatikana katika ramani iliyochorwa na mkoloni.
 

pole sana ....kama unaona aibu kuitwa mtanganyika baadae utaona aibu kwanini wewe mtu mweusi... "mkataa kwao mtumwa"
 
we waache tu wazenz waondoke, watanganyika tutaendelea, bali soon wao watakuwa wapemba na unguja, si nyerere alitabiri?

huyu nyerere ndio ilisababisha haya yote... Yeye hakua nabii wala mtakatifu. Umasikini wa nchi yetu yeye ndio sababu. Acha kumuabudu...
 

mara chache sana kuona mtanganyika anakubali kuitwa hivyo...ndio wazanzibar wanawaiteni wa bara, wa mrima, wa upande wapili n.k. Jina la tanganyika lili uliwa na watanganyika wenyewe kwa matumaini ya kuifanya tanzania .
 

Watu wanashindwa kufahamu kuwa Tanzanaia ni Tan..Tanganyika Zan..Zanzibar..ia- ya kisanii.
Leo hata wasomi wanasema watanzania bara, watanzania visiwani...what is this?
Kuna mtanzania tu...mtanzania huyu ama ni mtanganyika au mzanzibari.

Hawa CCm wanapenda kutuchakachua akili...lakini hawawezi kufanikiwa kwa hili. Hazikuungana Tanzania bara na Tanzania visiwani.

Ziliungana Tanganyika na Zanzibar kufanya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Jina refu likawa kero likafupishwa kuwa Tanzania...sasa kwa nini CCM wanataka kulirefusha tena?
Tusikubali kuchakachuliwa akili!

Sisi ni watanzania ok, lakini hatuwezi kuwa watanzania bara. Ni watanganyika.
 
Ziliungana Tanganyika na Zanzibar kufanya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Jina refu likawa kero likafupishwa kuwa Tanzania...hatuwezi kuwa watanzania bara. Ni watanganyika.

Kuna nchi inaitwa São Tomé and Príncipe, ni muungano wa nchi mbili (visiwa) na majina yote mawili yanatumika. Leo watu mnaona aibu kuitwa watanganyika!
 
Kilicho wazi ni kuwa Zanzibar (hata ikiitwa Tanzania Visiwani) imefanya mabadiliko ya Katiba yake ambayo yamezingatia mahitaji na maslahi yake ki-muungano. Isikubalike kuwa Tanganyika (hata ikiitwa Tanzania Bara) isifanye mabadiliko ya Katiba yasiyozingatia mahitaji na maslahi ya watu wake. Kuwa na uwakilishi wa 50/50 katika kila jambo ni kupuuza milioni 40 ya watu, huku umuihimu ukipewa kwa idadi ya nchi zilizoungana (nusu kwa nusu eti kwa sababu ni nchi 2 zimeungana). Kuchelewa kufanya mabadiliko ya ki-Katiba kusiwe ni udhaifu ambao Zanziba wanataka kuutumia sasa. Wa-Tanzania Bara hawakuhusishwa na mabadiliko ya Katiba Zanzibar. Lilichukuliwa kama ni swala na Ki-siasa zaidi (CCM na CUF).

Hii ndilo kosa ambalo CCM kwa kufahamu au kwa kupuuzia, haikulifanya zaidi. Na CCM isihusike sasa kufanya mabadiliko. Si swala la Rais wa kisiasa, ni swala la wananchi ktk ujumla wao, itikadi zao, imani zao, taaluma zao. It's not a political thing but rather socio-economical !!
 

kama ulizaliwa katika nchi ambayo imepakana na kenya,uganda,burundi,ruanda,zambia,malawi na msubiji ...wewe ni mtanganyika... Na kama ulizaliwa katika visiwa vya zanzibar wewe ni mzanzibari... Kama umezaliwa zanzibar au tanganyika na mzee wako mmoja akiwa mtanganganyika na mmoja akiwa mzanzibari , basi wewe utakua mtanzania.
 

kilicho bakia ni kudai katiba ya tanngankia kabla ya katiba ya muungano...zanzibar tayari wanayo katiba yao.
 

usilalamikie wanaodai haki zao. Kwanini wewe usidai haki ya kuwa na katiba ya tanganyika...baadae tuangalie katiba ya muungano.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…