Nchi ya Morocco imewa-prove wrong

Nchi ya Morocco imewa-prove wrong

Kijakazi

Platinum Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
9,313
Reaction score
14,983
Jarida la the Bloomberg la Marekani limechapisha the most innovative countries in the World na nchi ya kwanza mpaka ya tano hakuna hata moja inayozungumza au kutumia Kiingereza Nchi ya kwanza ni Korea Kusini(kikorea), ya pili Ujapani(kijapani) na ya tatu ni Ujerumani(Kijerumani) lakini lililonivutia kuliko yote na hata kunifanya nilete mada hii hapa ni nchi ya Moroko ambayo iko Kaskazini mwa Bara la Afrika nchi hii imeshika nafasi ya 50 katika nchi most innovative Duniani.

Sasa hizo za kwanza mtasema ni nchi tajiri tayari na Je Moroko? Wamewezaje kuwa the most innovative country (50) in world wakati Watanzania wanajua kiingereza kuwashinda hata Wamoroko?

Na kama kiingereza ndiyo Maendeleo mbona Kenya,Uganda na sijui Zambia, Nigeria na Zimbabwe ambao watoto wanabandikwa makaratasi mgongoni yanayosema.

Iam stupid for speaking African language" hawamo kwenye orodha ya most innovative countries?


Most Innovative: Countries - Bloomberg Best (and Worst)
 
Nadhani sababu watanzania wengi wanajua kiswahili ingekuwa bora mitaala yetu iwe ya kiswahili toka zamani enzi hizo.
 
Waswahili walionya kuhusu kuiga tembo kunya na kupasuka msamba.

Morocco wanaongea Kifaransa na Kiarabu.

Duuuuuu umeua! nimeshangaa mada yake kubwa inahusu lugha, point yake kubwa ya reference ni morroco. Hio morocco hajaweza kusema wanaongea lugha gani.


Poor you cc: limetumbuka
 
South Korea, mitaala yao ya sasa ni full English, English haikwepeki katika dunia ya leo...tunamiuse matumizi ya rasilimali zetu kwa kuanza kutumia muda wetu kutafuta maneno mbadala ya kufindishana wakati lugha yetu yenyewe haina maktaba ya kutosha. Only in Tanzania...where politicians do whatever they want!!
 
Duuuuuu umeua! nimeshangaa mada yake kubwa inahusu lugha, point yake kubwa ya reference ni morroco. Hio morocco hajaweza kusema wanaongea lugha gani!


Poor you cc: limetumbuka
Bila shaka kwa kuwa MOROCCO imehudumia watalii kwa mda mrefu! Utalii huko Morocco. Unanyanyua uchumi kwa kiwango kikubwa.
 
Duuuuuu umeua..............., nimeshangaa mada yake kubwa inahusu lugha, point yake kubwa ya reference ni morroco. Hio morocco hajaweza kusema wanaongea lugha gani!


Poor you cc: limetumbuka

Watanzania hata Kiswahili hawajui.

Wanatafuta mchawi wakati tatizo lao uchafu.

Hata wakibadilisha mambo kwenda Kiswahili watajikuta hawakijui.

Then what?

Tubadilishe kwenda kwenye lugha za makabila?
 
Last edited by a moderator:
Waswahili walionya kuhusu kuiga tembo kunya na kupasuka msamba.

Morocco wanaongea Kifaransa na Kiarabu.


Labda haujanielewa hoja kuu ya watu wengi ni kwamba bila kiingereza Dunia hii hauwezi kutoka na mimi ndio nikaleta mfano wa kamba kama Kiingereza ndio sababu ya nchi kutoka basi ningetegemea nchi zinazotumia kiingereza kwenye elimu yao kama Kenya, Nigeria&Co. kuwa juu kimaendeleo kuliko zisizotumia Kiingereza hapa Afrika kama hilo ndio tatizo, kwa maana Wanigeria au Waghana wanajua kiingereza kuliko Wamoroko.
 
Duuuuuu umeua..............., nimeshangaa mada yake kubwa inahusu lugha, point yake kubwa ya reference ni morroco. Hio morocco hajaweza kusema wanaongea lugha gani!


Poor you cc: limetumbuka


Moroko hawaongei Kiingereza si nimeshaandika au haujanielewa? Nimesema hata Watz wanaweza kuongea Kiingereza klk Wamoroko hivyo kama Kiingeraza kingekuwa ni kigezo cha maendeleo basi ningetegemea nchi zinazoongea Kiingereza hapa Afrika ziwe juu zaidi!
 
South Korea, mitaala yao ya sasa ni full English, English haikwepeki katika dunia ya leo...tunamiuse matumizi ya rasilimali zetu kwa kuanza kutumia muda wetu kutafuta maneno mbadala ya kufindishana wakati lugha yetu yenyewe haina maktaba ya kutosha. Only in Tanzania...where politicians do whatever they want!!


Wewe ni Muongo Namba moja Duniani! Nimefika Korea Kusini na hawatumii Kiingereza, Kiingereza kinafundishwa kama Somo na masomo mengine yote yaliyobaki yanafundishwa kwa kikorea, Chuo Kikuu unaweza kusoma Kiingereza ukiwa na bahati lakini ni advanced degrees tena za baadhi sana lkn degree ya kwanza ni kikorea kitupu na ili usome Korea haijalishi unatoka wapi lazima mwaka mmoja usome kikorea na kufanya mtihani wa kikorea kwanza!
 
Labda haujanielewa hoja kuu ya watu wengi ni kwamba bila kiingereza Dunia hii hauwezi kutoka na mimi ndio nikaleta mfano wa kamba kama Kiingereza ndio sababu ya nchi kutoka basi ningetegemea nchi zinazotumia kiingereza kwenye elimu yao kama Kenya, Nigeria&Co. kuwa juu kimaendeleo kuliko zisizotumia Kiingereza hapa Afrika kama hilo ndio tatizo, kwa maana Wanigeria au Waghana wanajua kiingereza klk Wamoroko!

Kwanza labisa hakuna nchi yoyote "inayotoka" kwa kitu kimoja.

Pili, katika mambo ya maendeleo na lugha, point ya muhimu ni watu kutumia lugha yao au ya kigeni. Tukitumia Kituruki au Kiingereza zitabaki kuwa lugha za kigeni tu. Kwa hiyo argument ya msingi ni Kiswahili vs lugha za ughaibuni. In our case lugha ya ughaibuni imekuwa Kiingereza, wa Morocco kwao ni Kifaransa.

Sasa unapotoa mfano wa Morocco kufanikiwa bila kutumia Kiingereza wakati mtu mmoja katika kila watatu anajua Kifaransa unashangaza.
 
Watanzania hata Kiswahili hawajui.

Wanatafuta mchawi wakati tatizo lao uchafu.

Hata wakibadilisha mambo kwenda Kiswahili watajikuta hawakijui.

Then what?

Tubadilishe kwenda kwenye lugha za makabila?

Kwani ni nchi gani ambayo wananchi wake wote wanajua Lugha yake ya taifa yote? Mbona mnataka kuwa unfair sana kwa Waafrika? Hata Marekani kwenyewe kuna Wamarekani wengi tu wana shida na lugha ya Kiingereza, hata Uingereza hilo ni tatizo kuna watoto Waingereza (ethnic na wala siyo wahamiaji) na wana shida na Kiingereza mpaka wengine wanapewa kozi maalumu sasa kwa nini iwe ishu kwetu?
 
Kwanza labisa hakuna nchi yoyote "inayotoka" kwa kitu kimoja.

Pili, katika mambo ya maendeleo na lugha, point ya muhimu ni watu kutumia lugha yao au ya kigeni. Tukitumia Kituruki au Kiingereza zitabaki kuwa lugha za kigeni tu. Kwa hiyo argument ya msingi ni Kiswahili vs lugha za ughaibuni. In our case lugha ya ughaibuni imekuwa Kiingereza, wa Morocco kwao ni Kifaransa.

Sasa unapotoa mfano wa Morocco kufanikiwa bila kutumia Kiingereza wakati mtu mmoja katika kila watatu anajua Kifaransa unashangaza.

Kwa hiyo unataka kusema nini sasa? Kwa maana hoja ni kwamba tuko nyuma kwa maana hatujui kiingereza wewe unakuja unasema Wamoroko imewezekna kwa maana wanatumia Kifaransa, unamaanisha nini? Kwa maana kama Wamoroko wangekuwa wanatumia Kiswahili wasingeweza kuwa (among) most innovative countries?
 
Kusoma kiingereza na lugha zingine za kigeni ni jambo muhimu sana. Wachina wanasoma kwa kutumia kichina lakini aibu ni kwamba ukiinia hotel za wachina kule kwao uchina unakuta anaejua kiingereza ni hotel meneja tu wengine wote ukiwasemesha kiingereza wanakimbia kumwita hotel meneja. Naomba aibu hii isitupate watanzania.

Kusoma kwa kiswahili sio zambi lakini je kitatusaidiaje linapofika swala la kimwingiloano wakimataifa. Binafsi nahisi tutafeli.

Uzembe wetu wakujisomea luga mbalimbali na vitu vingine isiwe sababu yakukimbilia kukataa kiingereza na luga zingine za kigeni.
 
Kwa hiyo unataka kusema nini sasa? Kwa maana hoja ni kwamba tuko nyuma kwa maana hatujui kiingereza wewe unakuja unasema Wamoroko imewezekna kwa maana wanatumia Kifaransa, unamaanisha nini? Kwa maana kama Wamoroko wangekuwa wanatumia Kiswahili wasingeweza kuwa (among) most innovative countries?

Kwanza kabisa nimekwambia kwamba maendeleo hayatokani na kitu kimoja.

Kwa kurudi kwenye mazungumzo yanayoonyesha hujaelewa point hiyo, unaonyesha una ukosefu wa uelewa.

Pili, nimeeleza kwamba matatizo ya Watanzania ni zaidi ya lugha. Na tunaweza kubadili lugha kwenda Kiswahili tukajikuta hata Kiswahili hatukijui. Tutake kuanza kutumia lugha za makabila.

Hilo nalo umeonyesha ukosefu wa uelewa. Ungelielewa usingerudi kwenye kufanya lugha ndiyo tatizo letu.
 
Kusoma kiingereza na lugha zingine za kigeni ni jambo muhimu sana. Wachina wanasoma kwa kutumia kichina lakini aibu ni kwamba ukiinia hotel za wachina kule kwao uchina unakuta anaejua kiingereza ni hotel meneja tu wengine wote ukiwasemesha kiingereza wanakimbia kumwita hotel meneja. Naomba aibu hii isitupate watanzania.

Kusoma kwa kiswahili sio zambi lakini je kitatusaidiaje linapofika swala la kimwingiloano wakimataifa. Binafsi nahisi tutafeli.

Uzembe wetu wakujisomea luga mbalimbali na vitu vingine isiwe sababu yakukimbilia kukataa kiingereza na luga zingine za kigeni.


Hata wewe bado haujaelewa! Serikali haijakitupa kiingereza bali kitabaki kuwa somo kama vile yalivyo masomo mengine, na hivyo umahiri wa hilo somo utategema na umahiri wa mwalimu wa hilo somo, ni kama vile Hisabaiti tu ni somo kama lingine na ili lieleweke vizuri ni lazima Serikali iwekeze kwenye walimu wazuri wa Hisabati, hivyo kama Kiingereza (kama somo) kikifundishwa kwa ufanisi na ufasaha hakuna shida wanafunzi wataelewa tu, tatizo liko wapi?
 
Kwanza kabisa nimekwambia kwamba maendeleo hayatokani na kitu kimoja.

Kwa kurudi kwenye mazungumzo yanayoonyesha hujaelewa point hiyo, unaonyesha una ukosefu wa uelewa.

Pili, nimeeleza kwamba matatizo ya Watanzania ni zaidi ya lugha. Na tunaweza kubadiki lugha kwenda Kiswahili tukajikuta hata Kiswahili hatukijui. Tutake kuanza kutumia lugha za makabila.

Hilo nalo umeonyesha ukosefu wa uelewa. Ungelielewa usingerudi kwenye kufanya lugha ndiyo tatizo letu.

Na ndiyo hoja yangu kwamba tatizo la Tanzania au Afrika kwa ujumla SIYO Lugha Kiingereza bali tatizo liko sehemu nyingine kabisa na sababu hasa ya mimi kuleta hii mada kwa maana tumekuwa tukiaminishwa kwamba sisi ni masikini kwa maan hatujui kiingereza sasa kama ni hivyo basi nilitegema wanaojua Kiingereza wawe wameendelea lkn SIYO kweli hivyo tatizo letu liko mahali pengine kabisa na ni kweli hata kama leo TZ yote tukizumzungumza Kiingereza kama Uingereza bado tutakuwa masikini tu, ndiyo hoja yangu!

 
Back
Top Bottom