Nchi inamhitaji sana Dr. Magufuli

Nchi inamhitaji sana Dr. Magufuli

mahwahwajr

Member
Joined
Jun 10, 2010
Posts
18
Reaction score
22
Ndugu wanabodi,

Mjadala mkubwa hivi sasa nchini kwetu ni juu ya nani atakuwa kiongozi mkuu na kwa sasa mazungumzo yanawalenga zaidi watu wawili kwa maana ya Dr John Pombe Magufuli wa CCM na Mh Lowassa kwa upande wa UKAWA. Kwa bahati mbaya sana na kwa kusaidiwa na vyombo vya habari ambavyo kwa maoni yangu naona haviitendei haki nchi yetu, sasa hatujadili nini nchi yetu inahitaji na/au ni kiongozi mwenye qualities zipi tunahitaji ili kutoka hapa tulipo na kwenda mbele zaidi.

Mjadala sasa umekuwa juu ya mahudhurio ya watu kwenye mikutano na sio issues. SAD!!

Nimepata bahati ya kutafiti kazi za mgombea wa CCM Dr Magufuli hasa akiwa Wizara ya Ujenzi. Kwa maoni yangu huyu bwana ni MCHAPA KAZI hodari sana, sana. Sikumbuki kama tumewahi kupata kuwa na waziri mwenye uwezo mkubwa wa kiutendaji kama wa mheshimiwa Magufuli katika miaka ya hivi karibuni.

Tukiondoa ushabiki na madai ya mabadiliko ilhali nchi yetu inahitaji transformation, namuona Dr Magufuli akitufaa na kutuvusha kwenda hatua ya juu zaidi. Video hii hapa nchi ni ushuhuda wa namna bwana huyu alivyo mtendaji hodari.

 
Last edited by a moderator:
Sawa, Magufuli ni mchapa kazi ila tatizo lipo kwenye chama anacho fungamana nacho, hapo tuuuu. Hivi unamkumbuka profesa muhongo? Ubaya wake upo wapi zaidi ya kufungiwa nira na CCM?

Mkuu tafadhali acha kuitetea CCM, nina kila sababu za kuwakataa CCM kwani wamenihujumu mimi binafsi na pia wameihujumu jamii kwa ujumla ambayo mimi ni miongoni mwayo.
 
sawa, magufuli ni mchapa kazi ila tatizo lipo kwenye chama anacho fungamana nacho, hapo tuuuu. Hivi unamkumbuka profesa muhongo? Ubaya wake upo wapi zaidi ya kufungiwa nira na ccm?. Mkuu tafadhali acha kuitetea ccm, nina kila sababu za kuwakataa ccm kwani wamenihujumu mimi binafsi na pia wameihujumu jamii kwa ujumla ambayo mimi ni miongoni mwayo.


Kaka, i can feel your pain, lakini nchi yetu inwahitaji viongozi wa aina hii. Mimi wala siitetei CCM. Hili timbwili linaloendelea sasa hivi lazima limeinyoosha CCM kama kweli unadhani imewatenda vibaya wananchi wake. Nchi yetu inamhitaji sana Dr Magufuli
 
Sawa Dr Pombe hana shida..Lakini akishinda itakua tu business as usual tu..Kina vijanaa January, Rizi na nani watapewa uwaziri, mafisadi watalindwa, umaskini utadumishwa..

Huo upande mwingine nao ni vilevile...
Btw, mimi sioni tatizo yeyote kupewa uongozi kama anastahili. Suala ni je, akipewa uongozi anawatumikia watu?
 
Enough is enough. sera za kulindana na ufisadi ndio umewakatisha tamaa wananchi wengi.
Mtu akiboronga ofisi hii anahamishwa ofisi nyingine tu.
No. hakuna cha Magufuli wala makomeo, tunahitaji CHANGE period.
 
Magufuli mwenyewe alikwishatamka kuwa akiwa rais hatawaangusha wezi wenzake. Sasa unategemea mtu mwenye kauli ya namna hiyo analo jipya lipi kwa wananchi maskini?
 
Kifupi ni kwamba kuendelea kuitetea ccm ni kama kuhalalisha ujinga wao wa kuihujumu NCHI yetu.CCM wamefanya Nchi hii uongozi wake kuwa ni wa watu wenye pesa tu, masikini hata angekuwa na uwezo kiasi gani hawezi kuwa kiongozi siku hizi..Hivi kuna sababu yoyote ya msingi kuwauzia watanzania mafuta ya taa shs 2000? kuna sababu yoyote ya kuwauzi watanzania sukari shs 2000? kama unaipenda ccm na wewe una matatizo. mimi naiombea kifo chema
 
Mpaka sasa hatujasikia kauli za kijasiri toka kwa makufuli juu ya kushuhulikia mafisadi na rushwa. rushwa na ufisadi ndio matizo kubwa linaloisumbua Tanzania zaidi tumemsikia akimsifia Rais tu.Tunataka tusikie kauli yake dhidi ya mafisadi katiba Mpya escrow.
 
Kaka, i can feel your pain, lakini nchi yetu inwahitaji viongozi wa aina hii. Mimi wala siitetei CCM. Hili timbwili linaloendelea sasa hivi lazima limeinyoosha CCM kama kweli unadhani imewatenda vibaya wananchi wake. Nchi yetu inamhitaji sana Dr Magufuli

Mkuu ondoa neno"KAMA KWELI UNADHANI", ina maana wewe huoni matatizo yanayowapata Watanzania ambayo chanzo chake ni ccm..!? Au uko nje ya nchi wewe?
 
sawa, magufuli ni mchapa kazi ila tatizo lipo kwenye chama anacho fungamana nacho, hapo tuuuu. Hivi unamkumbuka profesa muhongo? Ubaya wake upo wapi zaidi ya kufungiwa nira na ccm?. Mkuu tafadhali acha kuitetea ccm, nina kila sababu za kuwakataa ccm kwani wamenihujumu mimi binafsi na pia wameihujumu jamii kwa ujumla ambayo mimi ni miongoni mwayo.

Kwanza pole sana ndugu.
Pili naomba kuchangia ktk mawazo yako kuwa unachokisema ni sahihi kwa asilimia kadha na kwa asilimia zingine si kweli kwamba eti tatizo ni chama kama chama. Chama kama chama naamini ukisoma makablasha yao naamini utakuta wameandika maandishi mazuri sana kama hivyo vyama vyetu vingine. Tatizo ninaloliona mie ni sisi watu wenyewe na wala sio mfumo tu. Ebu jipime nafsi yako mwenyewe ujiangalie. Suala la mtu kuitumia ofisi ya umma kama mradi wake au suala la mtu kuomba rushwa hili sio tatizo la mfumo bali ni tatizo la nafsi zetu kwa level ya mtu mmoja mmoja. Ivi Lowasa alivyopiga isue ya Richmond unataka kuniambia aliipiga na watumishi wote wa umma?
Je unata kuniambia wewe ukiombwa rushwa ni tatizo la mfumo au ni tatizo la huyo anayekuomba?

Naomba nimalizie kwa kusema kuwa tatizo sio chama cha mapinduzi bali tatizo ni sisi wenyewe.
Mfano: ivi kuna mtu hajui mchango wa Dr Slaa kwa cdm? Mbowe kamfanyia nini? Pale wa kulaumiwa ni cdm yote au ni mbowe?
 
Kaka, i can feel your pain, lakini nchi yetu inwahitaji viongozi wa aina hii. Mimi wala siitetei CCM. Hili timbwili linaloendelea sasa hivi lazima limeinyoosha CCM kama kweli unadhani imewatenda vibaya wananchi wake. Nchi yetu inamhitaji sana Dr Magufuli

magufur hawez kuendesha nch kwa mawazo yake,lazma aongozwe na chama,hata jk alikuwa mchapakaz xana lakn alipopewa urais akapoa na akawa mbwa asiyebweka
 
We cant solve the problem by the same level of thinking.lazma tubadir chama ili na chenyewe kiweze onesha uwezo wa kutatua matatzo ya wananchi
 
Back
Top Bottom