Deo Meck Mbagi
JF-Expert Member
- Apr 19, 2015
- 360
- 525
Nimeattach gazeti lenye tamko la chama cha nccr mageuzi wilaya ya Tarime kikipinga mgawanyo wa majimbo ndani ya Ukawa.
Ni dhahiri kuwa kuna tatizo kubwa ndani ya ukawa na viongozi wetu hawawi wakweli kuhusu kinachojiri ndani ya vikao, wanachoeleza kwa umma kinatofautiana na uhalisia.
Ni wakati sasa viongozi wa ngazi za Taifa wakawa wanaratibu mambo yao na viongozi wa ngazi za chini. Unafiki unaofanywa na viongozi ngazi ya Taifa hautasaidia kuwa na muungano imara, maana hadi sasa kuna sintofahamu na kujenga juu bila kuwa na msingi mzuri ni sawa na kujenga nyumba yenye paa zuri bila kuwa na msingi imara.
===============
Chanzo: Habari Leo
Ni dhahiri kuwa kuna tatizo kubwa ndani ya ukawa na viongozi wetu hawawi wakweli kuhusu kinachojiri ndani ya vikao, wanachoeleza kwa umma kinatofautiana na uhalisia.
Ni wakati sasa viongozi wa ngazi za Taifa wakawa wanaratibu mambo yao na viongozi wa ngazi za chini. Unafiki unaofanywa na viongozi ngazi ya Taifa hautasaidia kuwa na muungano imara, maana hadi sasa kuna sintofahamu na kujenga juu bila kuwa na msingi mzuri ni sawa na kujenga nyumba yenye paa zuri bila kuwa na msingi imara.
===============
06 MAY 2015
KAMATI ya Utendaji ya Chama cha NCCR-Mageuzi wilayani Tarime, imepinga uamuzi wa umoja wa vyama vya upinzani unaofahamika kama Ukawa wa kukipa Chadema hadhi ya kusimamisha wagombea katika asilimia 50 ya majimbo nchini.
Imedai kuwa, kwa kufanya hivyo ni sawa na kuibeba Chadema na kuviua vyama vingine vya upinzani.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki wakati wa kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho wilayani Tarime, Nelson Chacha Makaranga, Katibu wake, Julius Andrea na kushirikisha baadhi ya wajumbe kutoka wilaya za Rorya na Serengeti, mkoani Mara.
Wakitoa maazimio hayo katika kikao hicho, walisema kwa pamoja wanapinga taarifa inayodai Chadema imejichukulia 114 kati ya 227, huku CUF kikigawiwa majimbo 80 sawa na asilimia 35, NCCR majimbo 33 sawa na asilimia 15, na NLD ambacho haikuoneshwa idadi ya majimbo yake.
Tujiulize, kama wakishinda asilimia 50 ya majimbo yote si ndio watakuwa na wabunge wengi bungeni na kuchagua Waziri Mkuu kutoka chama chao? Sisi wa NCCR-Mageuzi Tarime tunaazimia kupinga. Tunaamini kwa staili hii wenzetu wanataka kutuburuza na kukwamisha juhudi za vyama vingine vya siasa kukua. Ilikuwa sehemu ya maazimio ya kikao hicho.
Wajumbe hao walitoa mfano wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana 2014 NCCR Mageuzi kiliweka Wagombea katika Vijiji vya Nyarutu, Mjini Kati, Nyabichune na Nyangoto Nyamongo, lakini Chadema nao waliweka wagombea wao na hivyo kukiuka makubaliano ya Ukawa, hali iliyochangia kushindwa kufanya vizuri katika maeneo hayo.
Maazimio hayo yaliwasilishwa kwa Katibu Mwenezi wa NCCR Mageuzi ngazi ya Taifa, Faustin Sungura (pichani), ambaye mara baada ya kuyapokea, alisema: Nimepokea Mazimio yenu haya ambayo hata mimi nimeona yana Hoja za Msingi na nitayafikisha katika Uongozi wa Juu wa Chama chetu na kufanyiwa kazi , ili kuweka wazi muungano huu wa UKAWA usiwe wa kuvihujumu vyama vingine Maazimio haya ya Tarime tutayapeleka katika Vikoa vya vyama vingine vya Upinzani ili kuweka Wazi Hoja yenu hii.
Chanzo: Habari Leo