NCCR wamgwaya Kafulila

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
BAADA ya Chama cha NCCR-Mageuzi kumfukuza uanachama mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila sasa kinasuasua kulijulisha Bunge kwa barua kuwa mbunge huyo kijana siyo mwanachama wa chama hicho.

Mwananchi pia limebaini kwamba, Kafulila pamoja na wenzake bado hawajakabidhiwa barua za kufukuzwa kwao na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, uamuzi ambao umepata upinzani mkubwa kutoka kwa watu na taasisi mbalimbali nchini.

Jana viongozi wa NCCR Mageuzi walipoulizwa walitupiana mpira kuzungumzia suala hilo, ikiwa ni wiki moja tangu Nec ya chama hicho kumvua uanachama Kafulila kutokana na kile kilichodaiwa ni kosa la kuzungumza siri za ndani za chama katika vyombo vya habari.

Kafulila alifukuzwa uanachama pamoja na wenzake watatu, akiwemo aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho katika uchaguzi wa mwaka jana, Hashim Rungwe. Katibu Mkuu wa chama hicho Samwel Ruhuza alisema huenda barua hiyo ilipelekwa katika ofisi za Bunge jana huku akishikwa na kigugumizi kufafanua zaidi na kuomba atafutwe Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Kampeni na Uchaguzi wa chama hicho, Faustine Sungura. "Sijui wameshapeleka…, itakuwa wamepeleka bungeni, inawezekana ikawa wamepeleka leo (jana), ila sitaki kufafanua zaidi wala ku ‘confirm' (kuthibitisha) kwa sababu nipo safarini," alisema Ruhuza.

Hata hivyo, gazeti hili lilipomtafuta Sungura alisema hafahamu chochote kuhusu suala hilo huku akimrushia mpira Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, George Kahangwa. Kahangwa alipoulizwa alisema hawezi kujibu lolote na kutaka iulizwe ofisi ya bunge. "Iulizeni ofisi ya bunge kama barua hiyo wameshaipata ama laa…, unajua hatupendi kuzungumza masuala haya tena, hivi sasa mkitaka maelezo waulizeni wahusika wenyewe, kama chama tumeshafanya kikao na kutoa uamuzi," alisema Kahangwa.
 
Mkuu, kama habari kwamba alimpigia magoti Mbatia ni za kweli,then kumgwaya kivipi?

Si useme tu maybe wamemsamehe?
 
Huyu Kahangwa si member hapa??
Anaweza kua na jibu zuri zaidi kuhusu Kafulila!!
 
Kwa niaba ya chama changu cha NCCR, nawataarifu rasmi kuwa jana tuliwasilisha barua kwa spika kumtaarifu rasmi juu ya kuvuliwa uanachama wa Kafulila kwa makosa ya utovu wa nidhamu.

Kwa hiyo anayedhani tunamgwaya aachane na mtazamo huo, hiki chama ni makini, hakina woga kinajiamini katika mambo yake na ndiyo maana pamoja na kuwa na wabunge wa chache bado kimeonesha msimamo wa kutojali kumvua uanachama mtovu wa nidhamu Kafulia.

Kubwa hasa ni kuonesha mfano kwa vyama vingine kuwa hakuna sababu ya kumwogopa mbunge akikiuka taratibu zilizowekwa, kuna watu wanaona kafulila kaonewa kwa sababu ya ushabiki wao.

Kaonewa wapi na kivipi? HIVI MNATAKA KUTUAMBIA KUWA KAFULILA YUPO JUU YA SHERIA KIASI KWAMBA AMEKOSEA ASIADHIBIWE? Ukweli huo utakuwa ni wendawazimu, sasa barua imepelekwa kwa spika, Aidha madai ya tendwa na katibu ya bunge ni ya kipuuzi kuwa inabidi ofisi ya bunge inapinga kuvuliwa uanachama wa Kafulila ni ya kipuuzi, iwapo wamehongwa warudishe chenji mapema kwa Sababu hawana mamlaka ya kuingilia uhuru wa vyama vya siasa kwa katibu wa Bunge SIYO MAHAKAMA, na tendwa siyo mahakama hali kadharika na hata mahakama inapaswa kufanay review juu ya uamuzi wa NCCR kumvua uanachama kafulila na wenzake na ikiona alionewa itatoa Ruling juu ya hilo.

Kwa hiyo siyo sahihi hata kidogo kwa katibu wa bunge na Tendwa kuingila maamuzi ya chama kwa kupinga isipokuwa wana haki ya kushauri na kutoa maoni yao juu ya uamuzi uliofanywa na NCCR. Tunasisitiza tena kuwa waache mara moja kujifanya wana mamlaka ya kuingilia uhuru wa chama zaidi ya kutoa maoni ambayo ni kama ushauri tu. Katika hili wakumbuke kuwa utaratibu ni kwamba Mbunge anapokuwa amevuliwa uananchama ni kuwa chama kinamtaarifu spika na na kisha spika anapaswa kutoa taarifa kwa tume ya taifa ya uchaguzi ili tume iendelee na utaratibu mwingine. Na inapotokea mbunge aliyevuliwa uanachama kaonewa inampasa aende mahakamani kudai haki yake na ikitokea kashinda kesi basi ataendelea kuwa mwanachama na kuwa mbunge tena huku akilazimika kuheshimu kanuni na taratibu za chama.

Hivyo basi, Kafulila iwapo ameenda mahakamani kama imevyoripotiwa na vyombo vya habari hapo yupo sahihi kisheria na siyo kama katibu wa bunge amevyoripoitwa na baadhi ya magazeti kuwa watapitia uamuzi wa NCCR, tunasema hana mamlaka hayo kisheria lakini kama anabeep ajaribu aone. Asiingilie uhuru wa chama na kutaka kuvunja katiba ya chama chetu, iwapo amehongwa arudishe hela za watu. Hatutaki kupuuzwa na kuingilia taratibu zetu, hawezi kutulazimisha kuwa na mtu ambaye hatutaki awe mwanachama wetu, labda mahakama ndiyo inaweza kwa mujibu wa sheria iwapo chama p[ia hakitaridhika na hukumu ya mahakama milango itakuwa wazi kwetu sisi kukata rufaa kwa mahakama za juu zaidi.

Hata hivyo tunasema kuwa Kafulila hakuonewa na hatuoni atashindaje kesi, amevunja taratibu za chama, aldhabu aliyopewa ni sahihi kwa mujibu wa katiba na kanuni za chama. Anayetaka kujua kuwa barua imeshawasilishwa kwa spika wa bunge awasiliane na ofisi za bunge.

Hatumgwayi Kafulila; NCCR tunasema yupo sahihi kwenda mahakamani, tutakutana huko.
 
Hivi waandishi wetu wamefundishwaje hawa? Wanaudhi bwana, eti nccr wamgwaya? Watamgwaya vipi wakati jamaa kilio na machozi ya posho hayakumsaidia! NCCR wameonesha ukomavu ktk kusimamia katiba yao. Tendwa na Kashilila mbona nao kiherehere vile? Nashangaa hii nchi sijui tuna wasomi wa aina gani hawa! Hayo mamlaka ya kuingilia vyama wameyatoa wapi? Hata Ma-Pinda naye aliwahi kushauri watu waende mahakamani eti wameonewa, matokeo yake wakagaragazwa ikawa aibu kwake. Well done nccr!
 
Wananchi wa Kasulu kusini wanatakiwa kusoma hii makala!

*"Nimesoma taarifa mbali mbali juu ya kufukuzwa uanachama kwa Mbunge**David**Kafulila na nilipata fursa**ya kutoa maoni yangu pale vyombo vya habari vilipotaka hivyo kutoka kwangu, nimefuatilia kwa makini sana mijadala mbali mbali haswa katika mtandao wa Jamii Forum na kuona mawazo ya**Watanzania mbali mbali juu ya jambo hili.

Na ninafikiri ninao wajibu**kama kijana tena Mbunge kutoa maoni yangu na mtazamo wangu kwa kina juu ya jambo hili ambalo limemkuta Mbunge mwenzetu na rafiki yetu kijana Bwana David Kafulila.

" Kwanza kabisa Bwana David Kafulila pole sana lakini kikubwa zaidi jipe moyo kwani changamoto katika siasa mara nyingi ni matukio yasio ya kawaida ambayo yanaweza kushusha heshima ya mtu au kupandisha heshima ya mtu, lakini tambua kuwa matatizo sio msingi mkuu wa kuharibu ndoto ya mtu makini aliyekusudia kutimiza jambo ambalo wajibu wake ni upendo , utu na ukweli katika jamii ni imani yangu kuwa**changamoto hii inaweza kukufanya uwe kijana mwenye**hekima zaidi**kwani katika kila changamoto kubwa Duniani hapo ndipo ukombozi ulipotokea Duniani.

*Ninatambua wakati unaopitia kwa sasa wewe na familia yako na wapiga kura wako , lakini kwa mtu makini kama mimi ni lazima pia nikipongeze Chama chako kwa uamuzi wake dhidi yako , chama chako cha NCCR-Mageuzi**kimechukua hatua muhimu katika maisha yake ya siasa na kwamba**" Nidhamu katika Chama itakuwa ni msingi mkuu katika kutafuta ukombozi wa kweli katika Taifa,**Binafsi**sifurahi wewe kufukuzwa katika Chama lakini nimefarijika na jinsi Chama**kinachukuwa**taratibu kama NCCR kinavyoweza kuchukua maamuzi magumu ya kulinda nidhamu na heshima ndani ya Taasisi ya Chama cha Siasa.

Watu wengi hata mimi ningependa usamehewe , lakini David katika maisha ya siasa na Nyanja nyingine , uvumilivu na nidhamu katika kufanikisha maono au ndoto ni vitu ambayo ni msingi mkuu wa mafanikio**na hauwezi kuviepuka**ndio maana , Mtu mmoja mwenye hekima aliwahi kupata kunena kuwa " huwezi kupata kifaranga cha kuku kwa kuvunja yai bali kwa kusubiri yai liatamiwe kwa siku kadhaa na**baadae vifaranga watatotolewa.

Lakini vile vile Mtu huyu mwenye hekima akasema tena**" haijalishi**unampenda mke wako kiasi gani , kuna vitu unaweza kumsaidia na kuna vitu huwezi kumsaidia " kwa mfano huwezi kumsaidia mke wako kubeba mimba hata kama unampenda**sana , hivyo malengo makubwa katika siasa ni jambo muhimu kwa kijana makini kama wewe kufikiria lakini uvumilivu na kusubiri ni*muhimu katika kufikia malengo makuu.

Mimi binafsi ninatofautiana na watu wengi kwamba kupoteza jimbo ni jambo gumu na baya , hapana kupoteza jimbo kwa sababu ya kulinda nidhamu ni jambo jema linalopaswa kufanyiwa hata sherehe , hivi kweli tunaweza kupima nidhamu**na ni kitu gani katika maisha ya mwanadamu**? na vile vile tufikirie kama leo Mbunge au Diwani akifukuzwa kwa utovu wa nidhamu na sisi tukafikiri ni makosa , je ni halali sasa vyama vya upinzani kutafuta kuunda dola kama vitashindwa kusimamia tu**nidhamu ndani ya vyama vyao**,je*vitaweza kweli kusimamia nidhamu ya dola pindi vitakapochukua madaraka ?


NCCR Mageuzi wamefanya maamuzi ya msingi na ya uhakika kulinda nidhamu ndani ya chama ambaye yeyoye atakayethubutu kulaani basi ajiulize swali hili ? Kama nafasi ya Ubunge inathamani kubwa kuliko nidhamu ndani ya chama na jamii , je mtakuwa na ujasiri kweli wa kupinga dhambi**dhidi ya utu wa mwanadamu ambapo hivi karibuni mlipewa masharti ya ndoa ya jinsia moja kama mnataka misaada ?

**sasa mkisema nidhamu ipuuzwe dhidi ya nafasi moja ya Ubunge , mtawezaje sasa kuvumilia**njaa ,mateso na dhiki dhidi ya kutetea utu wenu ? nina wasi wasi kuwa**siku moja pengine mtakubali yale mashariti mliyopewa**na**waziri Mkuu wa Uingereza ili muweze**kula lakini**kwa kudhalilisha utu wenu , kwani nafasi ya nidhamu katika maisha ya binadamu haupaswi kupigiwa kura .


Hivyo tukifahamu msingi mkuu wa mafanikio**kuwa ni**pamoja na**nidhamu ya kweli , nafikiri maoni ya wachangiaji**yatajikita katika kuutukuza ukweli na wala sio nafasi au cheo cha mtu,**Na ni hatari**wasomi wakifikiri kwamba lengo la vyama vya upinzani ni kushinda viti vya ubunge , madiwani bila kuzingatia maadili na nidhamu basi ni ukweli kuwa hatutakuwa na sababu ya msingi ya kuwaondoa madarakani chama tawala , kwani ugomvi wetu**vyama vya upinzani na chama tawala hausababishwi na tofauti ya rangi za bendera**bali ni msingi katika maadili, nidhamu na uwajibikaji usiozingatia haki na kweli ndio maana kwa sababu hiyo ufisadi,wizi na ubabaishaji umekuwa ukiongezeka kila wakati na kuletea Taifa madhara makubwa.

*Aliyekosa akiwa muungwana anaomba radhi na ndio ushauri wangu kwa David , lakini jambo hili limeshitua lakini pia limefundisha**na jambo la kushangaza hapa,**ni kwanini watu wameshituka sana Mbunge kufutiwa uanachama na sio kwanini Mbunge amekuwa mtovu wa nidhamu**, hata hivyo sifahamu mgogoro huu kwa kina sana , lakini najua**sihitaji ruhusa kuingia chumbani kwangu , mgogoro huu na malumbano yalikuwa wazi tena wazi sana ,
Sasa nimalizie kwa kusema**David bado unayo nafasi kubwa ya kujirekebisha na kuwa kiongozi mzuri , wako waliopata matukio magumu ya kisiasa kuliko wewe lakini waliweza kurudi kwenye nafasi zao kwa utumishi**kama,**Martin Luther King Jr.**alivyopata*kunena***"*The ultimate measure of a man is not where he stands in moments of comfort, but where he stands at times of challenge and controversy.

Naibu Katibu mkuu wetu Mh Zitto nimesoma habari mbali mbali kuwa amekukaribisha Chadema ,**lakini mimi kwa sasa**nakukaribisha**Arusha kama utapenda kupumzika huku ukitafakari ili upate kujua kuwa unapaswa kuhama Chama au unapaswa kuomba radhi na kujirekebisha ?

Mfano ,ukiuguua ugonjwa wa zinaa pamoja na kutubu dhambi kwa mwenyezi Mungu lakini**pia itakupasa kwenda Hosipatalini kutafuta dawa, sioni kama ni muhimu sana kuhama Chama isipokuwa kuomba radhi hata kama wewe sio Mbunge tena


*"Jipe moyo David Kafulila na Hongera NCCR-MAGEUZI. . Sasa ningekushauri utafute kitabu kinachoitwa**" THE 21 MOST POWERFUL MINUTES IN A LEADERS DAY " Kilichoandikwa na na mwandishi maarufu " John C. Maxwell.
*
If you are a leader , it's not enough to know what to do . You have to know when to act. " John C. Maxwell.

Godbless Lema . (Mb)

 
Wananchi wa Kasulu kusini wanatakiwa kusoma hii makala!
*"Nimesoma taarifa mbali mbali juu ya kufukuzwa uanachama kwa Mbunge**David**Kafulila na nilipata fursa**ya kutoa maoni yangu pale vyombo vya habari vilipotaka hivyo kutoka kwangu, nimefuatilia kwa makini sana mijadala mbali mbali haswa katika mtandao wa Jamii Forum na kuona mawazo ya**Watanzania mbali mbali juu ya jambo hili.

Na ninafikiri ninao wajibu**kama kijana tena Mbunge kutoa maoni yangu na mtazamo wangu kwa kina juu ya jambo hili ambalo limemkuta Mbunge mwenzetu na rafiki yetu kijana Bwana David Kafulila.

" Kwanza kabisa Bwana David Kafulila pole sana lakini kikubwa zaidi jipe moyo kwani changamoto katika siasa mara nyingi ni matukio yasio ya kawaida ambayo yanaweza kushusha heshima ya mtu au kupandisha heshima ya mtu, lakini tambua kuwa matatizo sio msingi mkuu wa kuharibu ndoto ya mtu makini aliyekusudia kutimiza jambo ambalo wajibu wake ni upendo , utu na ukweli katika jamii ni imani yangu kuwa**changamoto hii inaweza kukufanya uwe kijana mwenye**hekima zaidi**kwani katika kila changamoto kubwa Duniani hapo ndipo ukombozi ulipotokea Duniani.

*Ninatambua wakati unaopitia kwa sasa wewe na familia yako na wapiga kura wako , lakini kwa mtu makini kama mimi ni lazima pia nikipongeze Chama chako kwa uamuzi wake dhidi yako , chama chako cha NCCR-Mageuzi**kimechukua hatua muhimu katika maisha yake ya siasa na kwamba**" Nidhamu katika Chama itakuwa ni msingi mkuu katika kutafuta ukombozi wa kweli katika Taifa,**Binafsi**sifurahi wewe kufukuzwa katika Chama lakini nimefarijika na jinsi Chama**kinachukuwa**taratibu kama NCCR kinavyoweza kuchukua maamuzi magumu ya kulinda nidhamu na heshima ndani ya Taasisi ya Chama cha Siasa.

Watu wengi hata mimi ningependa usamehewe , lakini David katika maisha ya siasa na Nyanja nyingine , uvumilivu na nidhamu katika kufanikisha maono au ndoto ni vitu ambayo ni msingi mkuu wa mafanikio**na hauwezi kuviepuka**ndio maana , Mtu mmoja mwenye hekima aliwahi kupata kunena kuwa " huwezi kupata kifaranga cha kuku kwa kuvunja yai bali kwa kusubiri yai liatamiwe kwa siku kadhaa na**baadae vifaranga watatotolewa.

Lakini vile vile Mtu huyu mwenye hekima akasema tena**" haijalishi**unampenda mke wako kiasi gani , kuna vitu unaweza kumsaidia na kuna vitu huwezi kumsaidia " kwa mfano huwezi kumsaidia mke wako kubeba mimba hata kama unampenda**sana , hivyo malengo makubwa katika siasa ni jambo muhimu kwa kijana makini kama wewe kufikiria lakini uvumilivu na kusubiri ni*muhimu katika kufikia malengo makuu.

Mimi binafsi ninatofautiana na watu wengi kwamba kupoteza jimbo ni jambo gumu na baya , hapana kupoteza jimbo kwa sababu ya kulinda nidhamu ni jambo jema linalopaswa kufanyiwa hata sherehe , hivi kweli tunaweza kupima nidhamu**na ni kitu gani katika maisha ya mwanadamu**? na vile vile tufikirie kama leo Mbunge au Diwani akifukuzwa kwa utovu wa nidhamu na sisi tukafikiri ni makosa , je ni halali sasa vyama vya upinzani kutafuta kuunda dola kama vitashindwa kusimamia tu**nidhamu ndani ya vyama vyao**,je*vitaweza kweli kusimamia nidhamu ya dola pindi vitakapochukua madaraka ?


NCCR Mageuzi wamefanya maamuzi ya msingi na ya uhakika kulinda nidhamu ndani ya chama ambaye yeyoye atakayethubutu kulaani basi ajiulize swali hili ? Kama nafasi ya Ubunge inathamani kubwa kuliko nidhamu ndani ya chama na jamii , je mtakuwa na ujasiri kweli wa kupinga dhambi**dhidi ya utu wa mwanadamu ambapo hivi karibuni mlipewa masharti ya ndoa ya jinsia moja kama mnataka misaada ?

**sasa mkisema nidhamu ipuuzwe dhidi ya nafasi moja ya Ubunge , mtawezaje sasa kuvumilia**njaa ,mateso na dhiki dhidi ya kutetea utu wenu ? nina wasi wasi kuwa**siku moja pengine mtakubali yale mashariti mliyopewa**na**waziri Mkuu wa Uingereza ili muweze**kula lakini**kwa kudhalilisha utu wenu , kwani nafasi ya nidhamu katika maisha ya binadamu haupaswi kupigiwa kura .


Hivyo tukifahamu msingi mkuu wa mafanikio**kuwa ni**pamoja na**nidhamu ya kweli , nafikiri maoni ya wachangiaji**yatajikita katika kuutukuza ukweli na wala sio nafasi au cheo cha mtu,**Na ni hatari**wasomi wakifikiri kwamba lengo la vyama vya upinzani ni kushinda viti vya ubunge , madiwani bila kuzingatia maadili na nidhamu basi ni ukweli kuwa hatutakuwa na sababu ya msingi ya kuwaondoa madarakani chama tawala , kwani ugomvi wetu**vyama vya upinzani na chama tawala hausababishwi na tofauti ya rangi za bendera**bali ni msingi katika maadili, nidhamu na uwajibikaji usiozingatia haki na kweli ndio maana kwa sababu hiyo ufisadi,wizi na ubabaishaji umekuwa ukiongezeka kila wakati na kuletea Taifa madhara makubwa.

*Aliyekosa akiwa muungwana anaomba radhi na ndio ushauri wangu kwa David , lakini jambo hili limeshitua lakini pia limefundisha**na jambo la kushangaza hapa,**ni kwanini watu wameshituka sana Mbunge kufutiwa uanachama na sio kwanini Mbunge amekuwa mtovu wa nidhamu**, hata hivyo sifahamu mgogoro huu kwa kina sana , lakini najua**sihitaji ruhusa kuingia chumbani kwangu , mgogoro huu na malumbano yalikuwa wazi tena wazi sana ,
Sasa nimalizie kwa kusema**David bado unayo nafasi kubwa ya kujirekebisha na kuwa kiongozi mzuri , wako waliopata matukio magumu ya kisiasa kuliko wewe lakini waliweza kurudi kwenye nafasi zao kwa utumishi**kama,**Martin Luther King Jr.**alivyopata*kunena***"*The ultimate measure of a man is not where he stands in moments of comfort, but where he stands at times of challenge and controversy.

Naibu Katibu mkuu wetu Mh Zitto nimesoma habari mbali mbali kuwa amekukaribisha Chadema ,**lakini mimi kwa sasa**nakukaribisha**Arusha kama utapenda kupumzika huku ukitafakari ili upate kujua kuwa unapaswa kuhama Chama au unapaswa kuomba radhi na kujirekebisha ?

Mfano ,ukiuguua ugonjwa wa zinaa pamoja na kutubu dhambi kwa mwenyezi Mungu lakini**pia itakupasa kwenda Hosipatalini kutafuta dawa, sioni kama ni muhimu sana kuhama Chama isipokuwa kuomba radhi hata kama wewe sio Mbunge tena


*"Jipe moyo David Kafulila na Hongera NCCR-MAGEUZI. . Sasa ningekushauri utafute kitabu kinachoitwa**" THE 21 MOST POWERFUL MINUTES IN A LEADERS DAY " Kilichoandikwa na na mwandishi maarufu " John C. Maxwell.
*
If you are a leader , it's not enough to know what to do . You have to know when to act. " John C. Maxwell.

Godbless Lema . (Mb)


unawashauri wasome utumbo huu,ambaye hata yeye anajuta kuuandika!!
 
Wananchi wa Kasulu kusini wanatakiwa kusoma hii makala!
*"Nimesoma taarifa mbali mbali juu ya kufukuzwa uanachama kwa Mbunge**David**Kafulila na nilipata fursa**ya kutoa maoni yangu pale vyombo vya habari vilipotaka hivyo kutoka kwangu, nimefuatilia kwa makini sana mijadala mbali mbali haswa katika mtandao wa Jamii Forum na kuona mawazo ya**Watanzania mbali mbali juu ya jambo hili.

Na ninafikiri ninao wajibu**kama kijana tena Mbunge kutoa maoni yangu na mtazamo wangu kwa kina juu ya jambo hili ambalo limemkuta Mbunge mwenzetu na rafiki yetu kijana Bwana David Kafulila.

" Kwanza kabisa Bwana David Kafulila pole sana lakini kikubwa zaidi jipe moyo kwani changamoto katika siasa mara nyingi ni matukio yasio ya kawaida ambayo yanaweza kushusha heshima ya mtu au kupandisha heshima ya mtu, lakini tambua kuwa matatizo sio msingi mkuu wa kuharibu ndoto ya mtu makini aliyekusudia kutimiza jambo ambalo wajibu wake ni upendo , utu na ukweli katika jamii ni imani yangu kuwa**changamoto hii inaweza kukufanya uwe kijana mwenye**hekima zaidi**kwani katika kila changamoto kubwa Duniani hapo ndipo ukombozi ulipotokea Duniani.

*Ninatambua wakati unaopitia kwa sasa wewe na familia yako na wapiga kura wako , lakini kwa mtu makini kama mimi ni lazima pia nikipongeze Chama chako kwa uamuzi wake dhidi yako , chama chako cha NCCR-Mageuzi**kimechukua hatua muhimu katika maisha yake ya siasa na kwamba**" Nidhamu katika Chama itakuwa ni msingi mkuu katika kutafuta ukombozi wa kweli katika Taifa,**Binafsi**sifurahi wewe kufukuzwa katika Chama lakini nimefarijika na jinsi Chama**kinachukuwa**taratibu kama NCCR kinavyoweza kuchukua maamuzi magumu ya kulinda nidhamu na heshima ndani ya Taasisi ya Chama cha Siasa.

Watu wengi hata mimi ningependa usamehewe , lakini David katika maisha ya siasa na Nyanja nyingine , uvumilivu na nidhamu katika kufanikisha maono au ndoto ni vitu ambayo ni msingi mkuu wa mafanikio**na hauwezi kuviepuka**ndio maana , Mtu mmoja mwenye hekima aliwahi kupata kunena kuwa " huwezi kupata kifaranga cha kuku kwa kuvunja yai bali kwa kusubiri yai liatamiwe kwa siku kadhaa na**baadae vifaranga watatotolewa.

Lakini vile vile Mtu huyu mwenye hekima akasema tena**" haijalishi**unampenda mke wako kiasi gani , kuna vitu unaweza kumsaidia na kuna vitu huwezi kumsaidia " kwa mfano huwezi kumsaidia mke wako kubeba mimba hata kama unampenda**sana , hivyo malengo makubwa katika siasa ni jambo muhimu kwa kijana makini kama wewe kufikiria lakini uvumilivu na kusubiri ni*muhimu katika kufikia malengo makuu.

Mimi binafsi ninatofautiana na watu wengi kwamba kupoteza jimbo ni jambo gumu na baya , hapana kupoteza jimbo kwa sababu ya kulinda nidhamu ni jambo jema linalopaswa kufanyiwa hata sherehe , hivi kweli tunaweza kupima nidhamu**na ni kitu gani katika maisha ya mwanadamu**? na vile vile tufikirie kama leo Mbunge au Diwani akifukuzwa kwa utovu wa nidhamu na sisi tukafikiri ni makosa , je ni halali sasa vyama vya upinzani kutafuta kuunda dola kama vitashindwa kusimamia tu**nidhamu ndani ya vyama vyao**,je*vitaweza kweli kusimamia nidhamu ya dola pindi vitakapochukua madaraka ?


NCCR Mageuzi wamefanya maamuzi ya msingi na ya uhakika kulinda nidhamu ndani ya chama ambaye yeyoye atakayethubutu kulaani basi ajiulize swali hili ? Kama nafasi ya Ubunge inathamani kubwa kuliko nidhamu ndani ya chama na jamii , je mtakuwa na ujasiri kweli wa kupinga dhambi**dhidi ya utu wa mwanadamu ambapo hivi karibuni mlipewa masharti ya ndoa ya jinsia moja kama mnataka misaada ?

**sasa mkisema nidhamu ipuuzwe dhidi ya nafasi moja ya Ubunge , mtawezaje sasa kuvumilia**njaa ,mateso na dhiki dhidi ya kutetea utu wenu ? nina wasi wasi kuwa**siku moja pengine mtakubali yale mashariti mliyopewa**na**waziri Mkuu wa Uingereza ili muweze**kula lakini**kwa kudhalilisha utu wenu , kwani nafasi ya nidhamu katika maisha ya binadamu haupaswi kupigiwa kura .


Hivyo tukifahamu msingi mkuu wa mafanikio**kuwa ni**pamoja na**nidhamu ya kweli , nafikiri maoni ya wachangiaji**yatajikita katika kuutukuza ukweli na wala sio nafasi au cheo cha mtu,**Na ni hatari**wasomi wakifikiri kwamba lengo la vyama vya upinzani ni kushinda viti vya ubunge , madiwani bila kuzingatia maadili na nidhamu basi ni ukweli kuwa hatutakuwa na sababu ya msingi ya kuwaondoa madarakani chama tawala , kwani ugomvi wetu**vyama vya upinzani na chama tawala hausababishwi na tofauti ya rangi za bendera**bali ni msingi katika maadili, nidhamu na uwajibikaji usiozingatia haki na kweli ndio maana kwa sababu hiyo ufisadi,wizi na ubabaishaji umekuwa ukiongezeka kila wakati na kuletea Taifa madhara makubwa.

*Aliyekosa akiwa muungwana anaomba radhi na ndio ushauri wangu kwa David , lakini jambo hili limeshitua lakini pia limefundisha**na jambo la kushangaza hapa,**ni kwanini watu wameshituka sana Mbunge kufutiwa uanachama na sio kwanini Mbunge amekuwa mtovu wa nidhamu**, hata hivyo sifahamu mgogoro huu kwa kina sana , lakini najua**sihitaji ruhusa kuingia chumbani kwangu , mgogoro huu na malumbano yalikuwa wazi tena wazi sana ,
Sasa nimalizie kwa kusema**David bado unayo nafasi kubwa ya kujirekebisha na kuwa kiongozi mzuri , wako waliopata matukio magumu ya kisiasa kuliko wewe lakini waliweza kurudi kwenye nafasi zao kwa utumishi**kama,**Martin Luther King Jr.**alivyopata*kunena***"*The ultimate measure of a man is not where he stands in moments of comfort, but where he stands at times of challenge and controversy.

Naibu Katibu mkuu wetu Mh Zitto nimesoma habari mbali mbali kuwa amekukaribisha Chadema ,**lakini mimi kwa sasa**nakukaribisha**Arusha kama utapenda kupumzika huku ukitafakari ili upate kujua kuwa unapaswa kuhama Chama au unapaswa kuomba radhi na kujirekebisha ?

Mfano ,ukiuguua ugonjwa wa zinaa pamoja na kutubu dhambi kwa mwenyezi Mungu lakini**pia itakupasa kwenda Hosipatalini kutafuta dawa, sioni kama ni muhimu sana kuhama Chama isipokuwa kuomba radhi hata kama wewe sio Mbunge tena


*"Jipe moyo David Kafulila na Hongera NCCR-MAGEUZI. . Sasa ningekushauri utafute kitabu kinachoitwa**" THE 21 MOST POWERFUL MINUTES IN A LEADERS DAY " Kilichoandikwa na na mwandishi maarufu " John C. Maxwell.
*
If you are a leader , it's not enough to know what to do . You have to know when to act. " John C. Maxwell.

Godbless Lema . (Mb)
nakubaliana na wewe katika swala zima la Nidhamu na maamuzi magumu ambayo hivi karibuni vyama vya siasa vimefanya. ila katika hili la NCCR-mageuzi ninashaka nalo kutokana na tarifa nilizosipata kutoka chanzo cha habari ambocho sina hakika nacho sana ya kuwa " siku chache kabla ya kikao cha NEC-Nccr kufanya maamuzi hayo wajumbe wa kikao hicho walibadilishwa kimyakimya/kinyemela na hata kupiga kura kulifanyika kwa njia ya wazi(kunyoosha vidole)" Kama nikweli kuhusu madai haya huoni kuwa haya ni maamuzi ya kukomoana? CDM walikuwa wavumilivu sana zidi ya madiwani waasi huko Arusha na hata kuwabembeleza kuwaita mmojammoja kuwahoji, tena hatukusikia tetesi za kubadilishwa wajumbe wa kamati husika. Je wewe unalionaje hili? enwei ni mtazamo tu.
 
Sina kumbukumbu sana lakini wakati mfumo wa mageuzi unaanza miaka ya 95 kama niko sawa mheshimiwa Chiku Abwao alitimliwa lakini alikula shushu ubunge mpaka uchaguzi wa 2000, Tena hawa hawa NCCR-WAGEUZI,
Na hii inshu ya mheshimiwa David Kafulila nadhani ndio inavyoelekea hukohuko.
 
Kwa niaba ya chama changu cha NCCR, nawataarifu rasmi kuwa jana tuliwasilisha barua kwa spika kumtaarifu rasmi juu ya kuvuliwa uanachama wa Kafulila kwa makosa ya utovu wa nidhamu.

Kwa hiyo anayedhani tunamgwaya aachane na mtazamo huo, hiki chama ni makini, hakina woga kinajiamini katika mambo yake na ndiyo maana pamoja na kuwa na wabunge wa chache bado kimeonesha msimamo wa kutojali kumvua uanachama mtovu wa nidhamu Kafulia.

Kubwa hasa ni kuonesha mfano kwa vyama vingine kuwa hakuna sababu ya kumwogopa mbunge akikiuka taratibu zilizowekwa, kuna watu wanaona kafulila kaonewa kwa sababu ya ushabiki wao.

Kaonewa wapi na kivipi? HIVI MNATAKA KUTUAMBIA KUWA KAFULILA YUPO JUU YA SHERIA KIASI KWAMBA AMEKOSEA ASIADHIBIWE? Ukweli huo utakuwa ni wendawazimu, sasa barua imepelekwa kwa spika, Aidha madai ya tendwa na katibu ya bunge ni ya kipuuzi kuwa inabidi ofisi ya bunge inapinga kuvuliwa uanachama wa Kafulila ni ya kipuuzi, iwapo wamehongwa warudishe chenji mapema kwa Sababu hawana mamlaka ya kuingilia uhuru wa vyama vya siasa kwa katibu wa Bunge SIYO MAHAKAMA, na tendwa siyo mahakama hali kadharika na hata mahakama inapaswa kufanay review juu ya uamuzi wa NCCR kumvua uanachama kafulila na wenzake na ikiona alionewa itatoa Ruling juu ya hilo.

Kwa hiyo siyo sahihi hata kidogo kwa katibu wa bunge na Tendwa kuingila maamuzi ya chama kwa kupinga isipokuwa wana haki ya kushauri na kutoa maoni yao juu ya uamuzi uliofanywa na NCCR. Tunasisitiza tena kuwa waache mara moja kujifanya wana mamlaka ya kuingilia uhuru wa chama zaidi ya kutoa maoni ambayo ni kama ushauri tu. Katika hili wakumbuke kuwa utaratibu ni kwamba Mbunge anapokuwa amevuliwa uananchama ni kuwa chama kinamtaarifu spika na na kisha spika anapaswa kutoa taarifa kwa tume ya taifa ya uchaguzi ili tume iendelee na utaratibu mwingine. Na inapotokea mbunge aliyevuliwa uanachama kaonewa inampasa aende mahakamani kudai haki yake na ikitokea kashinda kesi basi ataendelea kuwa mwanachama na kuwa mbunge tena huku akilazimika kuheshimu kanuni na taratibu za chama.

Hivyo basi, Kafulila iwapo ameenda mahakamani kama imevyoripotiwa na vyombo vya habari hapo yupo sahihi kisheria na siyo kama katibu wa bunge amevyoripoitwa na baadhi ya magazeti kuwa watapitia uamuzi wa NCCR, tunasema hana mamlaka hayo kisheria lakini kama anabeep ajaribu aone. Asiingilie uhuru wa chama na kutaka kuvunja katiba ya chama chetu, iwapo amehongwa arudishe hela za watu. Hatutaki kupuuzwa na kuingilia taratibu zetu, hawezi kutulazimisha kuwa na mtu ambaye hatutaki awe mwanachama wetu, labda mahakama ndiyo inaweza kwa mujibu wa sheria iwapo chama p[ia hakitaridhika na hukumu ya mahakama milango itakuwa wazi kwetu sisi kukata rufaa kwa mahakama za juu zaidi.

Hata hivyo tunasema kuwa Kafulila hakuonewa na hatuoni atashindaje kesi, amevunja taratibu za chama, aldhabu aliyopewa ni sahihi kwa mujibu wa katiba na kanuni za chama. Anayetaka kujua kuwa barua imeshawasilishwa kwa spika wa bunge awasiliane na ofisi za bunge.

Hatumgwayi Kafulila; NCCR tunasema yupo sahihi kwenda mahakamani, tutakutana huko.
Sina uhakika kama kweli wewe unawakilisha msimamo wa chama hata hivyo unaweza kutuambia Kafulila alipewa siku ngapi za kujitetea?
 
Back
Top Bottom