Marashi
JF-Expert Member
- Apr 14, 2018
- 2,774
- 4,269
Wakubwa shikamoni na wadogo hamjambo?
Nilitukanwa na jirani yangu, dada tu wa miaka 23 mfanya biashara. Kosa langu ni kumdai achangie bili ya maji, akasema mimi kimbelembele na akashusha matusi lukuki ambayo JF hairuhusu kuweka hapa.
Nilipoondoka kumuepuka alibadili mbinu akaanza kuvurumisha meseji za matusi ya kunisindikizia. Niliripoti polisi, nikalipia mafuta polisi wakamfuata na defender. Kesho yake akapewa dhamana.
Mwenendo wa upelelezi wa kesi hii haueleweki...nazungushwa. Tangu juzi naona mpelelezi anapost kwenye status ya whatsapp picha mbalimbali akiwa na yule dada kwenye maeneo ya starehe.
Kesi yangu hapeleki mahakamani nimetembea sana kwenda polisi lakini sioni chochote kinachoendelea. Kesi haijafika mahakamani miezi minne sasa na ushahidi upo wazi kabisa meseji zote za matusi ninazo sijafuta.
Naomba ushauri haki yangu inapotea mimi ni mtanzania mnyonge, au nikamuone Rais wetu anisaidie. Naomba ushauri
Nilitukanwa na jirani yangu, dada tu wa miaka 23 mfanya biashara. Kosa langu ni kumdai achangie bili ya maji, akasema mimi kimbelembele na akashusha matusi lukuki ambayo JF hairuhusu kuweka hapa.
Nilipoondoka kumuepuka alibadili mbinu akaanza kuvurumisha meseji za matusi ya kunisindikizia. Niliripoti polisi, nikalipia mafuta polisi wakamfuata na defender. Kesho yake akapewa dhamana.
Mwenendo wa upelelezi wa kesi hii haueleweki...nazungushwa. Tangu juzi naona mpelelezi anapost kwenye status ya whatsapp picha mbalimbali akiwa na yule dada kwenye maeneo ya starehe.
Kesi yangu hapeleki mahakamani nimetembea sana kwenda polisi lakini sioni chochote kinachoendelea. Kesi haijafika mahakamani miezi minne sasa na ushahidi upo wazi kabisa meseji zote za matusi ninazo sijafuta.
Naomba ushauri haki yangu inapotea mimi ni mtanzania mnyonge, au nikamuone Rais wetu anisaidie. Naomba ushauri