Nayakumbuka siku ile ya tar 29.

Nayakumbuka siku ile ya tar 29.

Lipijema

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2015
Posts
953
Reaction score
1,540
Hii siku nilikuwa na usafiri wangu wa Pikipiki nikielekea Katoro, mara baada ya kuingia mji huo nilikuta watu kadhaa wamekaa kimakundi punde si punde umbali kama wa mita mia tatu niliona gari la polisi likija kwa kasi, nilipunguza mwendo kwa haraka sana maana hao polisi walikuwa wakirusha risasi hovyo hovyo, nikapaki kwenye mkusanyiko wa watu kumbe pale palikuwepo na vijana ambao nao wanapambana kwa kuchoma moto matairi ili kuwazuia hao maaskari wasifanikishe kupiga raia.
Palikuwa na vituko vingi nilivyoshuhudia kuna Mama alikuwa anasubiri asafiri akapigwa risasi, kitu hicho kiliniogopesha sana, si hivyo tu ilinipasa niombe msaada wa kuifadhi usafiri wangu nikafanikisha kule mtaa wa kilimahewa nami nikatembea kwa njia za uchochoroni hadi nikafika nyumbani nyakati za usiku sana,kesho yake ilipofika mida ya saa nne asubuhi raia wakiwa wametulia walianza tena hao askari kupiga risasi zisizo na idadi hadi majumbani kuna kijana mdogo sana naye ilimpiga risasi nikishuhudia Mama wa huyo mtoto alichukua mwili wa kijana wake na kuanza kulia pale sebuleni, maaskari walifuata na kuuliza nanyi mnafanya nini hapa, wakatoa maelezo askari wakawaambia nyamazeni kimya la sivyo nanyi tutawafanya kama huyo.
Mauaji yalikuwa mengi mno ndani ya mji wa katoro na Buseresere walikuwa awaangalii mkubwa au mdogo, ibada zilisitishwa kwa waumini wa Islam kwa muda wa takriba siku nne.
Ndugu zangu mlio wa mijini tarehe 7/7 kama hali itarejea hivyo basi kazi tunayo, elewa hata ndani si salama.
Lakini ni nani aliyetufikisha hapa? Na kwa nini?
 
Screenshot_20260616-173300~2.png
 
Sasa hivi wamenulikwa kila kona mfano hata maandamano yakatokea tena haitakuwa kama 29 viongozi wa polccm wameogopa ni kutoa vitisho tu na kuuzia watu uoga. Yaani hawa watu wanatangaza amani huku wameficha mapanga
 
Sasa hivi wamenulikwa kila kona mfano hata maandamano yakatokea tena haitakuwa kama 29 viongozi wa polccm wameogopa ni kutoa vitisho tu na kuuzia watu uoga. Yaani hawa watu wanatangaza amani huku wameficha mapanga
Ukiwatazama mienendo yao unaona ni kama watu wenye uoga kweli?
Jamani wa kutoka watoke wakiwa kamili hado wa kujifungia wajifungie wa kusali wasali.
Lakini walah nakwambia hawa wehu hawatosita kurudia ya tar 29 ni wamechanganyikiwa na wameshaamua liwalo na liwe!
 
Ukiwatazama mienendo yao unaona ni kama watu wenye uoga kweli?
Jamani wa kutoka watoke wakiwa kamili hado wa kujifungia wajifungie wa kusali wasali.
Lakini walah nakwambia hawa wehu hawatosita kurudia ya tar 29 ni wamechanganyikiwa na wameshaamua liwalo na liwe!
sawa mkuu
 
Hii siku nilikuwa na usafiri wangu wa Pikipiki nikielekea Katoro, mara baada ya kuingia mji huo nilikuta watu kadhaa wamekaa kimakundi punde si punde umbali kama wa mita mia tatu niliona gari la polisi likija kwa kasi, nilipunguza mwendo kwa haraka sana maana hao polisi walikuwa wakirusha risasi hovyo hovyo, nikapaki kwenye mkusanyiko wa watu kumbe pale palikuwepo na vijana ambao nao wanapambana kwa kuchoma moto matairi ili kuwazuia hao maaskari wasifanikishe kupiga raia.
Palikuwa na vituko vingi nilivyoshuhudia kuna Mama alikuwa anasubiri asafiri akapigwa risasi, kitu hicho kiliniogopesha sana, si hivyo tu ilinipasa niombe msaada wa kuifadhi usafiri wangu nikafanikisha kule mtaa wa kilimahewa nami nikatembea kwa njia za uchochoroni hadi nikafika nyumbani nyakati za usiku sana,kesho yake ilipofika mida ya saa nne asubuhi raia wakiwa wametulia walianza tena hao askari kupiga risasi zisizo na idadi hadi majumbani kuna kijana mdogo sana naye ilimpiga risasi nikishuhudia Mama wa huyo mtoto alichukua mwili wa kijana wake na kuanza kulia pale sebuleni, maaskari walifuata na kuuliza nanyi mnafanya nini hapa, wakatoa maelezo askari wakawaambia nyamazeni kimya la sivyo nanyi tutawafanya kama huyo.
Mauaji yalikuwa mengi mno ndani ya mji wa katoro na Buseresere walikuwa awaangalii mkubwa au mdogo, ibada zilisitishwa kwa waumini wa Islam kwa muda wa takriba siku nne.
Ndugu zangu mlio wa mijini tarehe 7/7 kama hali itarejea hivyo basi kazi tunayo, elewa hata ndani si salama.
Lakini ni nani aliyetufikisha hapa? Na kwa nini?
kuna genge la wahuni ni kama lina nguvu kuliko Rais, CDF, CPF, DGIS, na kila taasisi ya umma.

genge hili limejaa ushetani. Linakwenda kuanguka sasa kwa nguvu za Mungu Aliye hai.
 
Back
Top Bottom