Amoxlin
JF-Expert Member
- May 30, 2016
- 3,784
- 4,097
Amani iwe nanyi ndugu zangu.
Leo nimeona niwaelezee japo kwa ufupi mateso nliyokumbana nayo ktk shule ya wavulana Lyamungo iliyopo wilaya ya hai mkoa wa Kilimanjaro.
Enzi za utawala:-
-Gervas.
-Wandiba.
-Mtera.
Nilipojiunga kidato cha kwanza nilipokelewa na waalimu na kupangiwa bweni la Agrey, wakati napelekwa bwenini nlisikia sauti zikiuliza kama nimebeba Mbuzi (mkate) na wengine kuulizia nimebeba dekio (kumbe kazi ya kidato cha kwanza ni kudeki shule nzima).
Usafi: Bweni letu (yote manne: Aggrey, Shaban robert, Lumumba na Amri Abedi) yalikuwa ni ghorofa moja lenye vyumba ishirini (kumi juu na kumi chini). Kazi ya kudeki bweni ilikua ni form one hivyo tulipangiwa vyumba viwili, kimoja juu na cha pili chini kudeki kila siku saa nne usiku baada ya prep.
Kulikuwa na utaratibu wa kumwagwa maji bweni zima na kikundi kilichoitwa "mwaga-maji" kisha ndo tuanze kudeki wakati mwingine bila taa na ukidek juu ukienda chini, juu maji yashaingia kweny chumba tena.
Mara nyingi tuliamshwa saa nane usiku na kulazwa sakafuni kisha kumwagiwa maji na kupigwa mikanda kisa hatujadeki vizuri. Tulikata tamaa na shule.
Jukumu la kudeki kordo za shule nzima lilikua la kwetu pia, hivyo tulikua kama watumishi wa shule na ikipita siku bila kupigwa vibaya unashukuru Mungu.
Kuna wakati tulipigwa marungu ya migongo mpaka kuvimba huku wengine wakiingizwa kwenye masink yenye utelezi wa kijani (fangasi), mabaki ya chakula na kufunguliwa bomba za maji.
Nilipochoka mateso hayo niliamua kuomba kazi kweny mradi wa Ng'ombe ambapo tulikua tukizoa mbolea na kuchunga ng'ombe siku ya Jumamosi, wengine walikua kwenye mradi wa nguruwe.
Chakula: Shule ilikuwa na Wanafunzi zaidi ya 3000 na utaratibu wa kula ilikua ni kwa mstari, tulipigwa sana mikanda kutokana na vurugu za mstari na tulikua wa mwisho kula. Mara nyingi tulikosa chakula au tulipata ugali na kukosa mboga.
Mzee Manase (Zizu) alikua mpishi katili sana, akiwa kwenye foleni kabla hujafika kwenye sufuria ashakurushia ugali uudake sasa ole wako uanguke chini. Huyu mpishi akigawa haangalii sura ila ole wako urudie chakula lazima akudake mkono na kichapo kizito. Alipenda kutukana sana. Wengine ni mzee Urasa na Mzee mwingine wa kijiji cha Narum.
Vijana toka kanda ya ziwa walikua vinara wa kula sana, walikua wakiitana "tuigonge" maana watatu wanaweza gonga dish zima la msosi. Tuliwaheshimu sana kwa kula yao japo hawakua smart.
Viongozi Miungu: Viongozi wa serikali ya wanafunzi walikua miungu watu.
Head boy alikuwa Isaya na makamu wake Lema. Waziri wa chakula Saika na wengine. Hawa walikua wakifanya kila walichotaka na walipiga hata kwa nondo bila kuhojiwa na mtu. Mpaka walimu waliwaogopa tokana na karate uchwara zao.
Viongozi walikuwa wakiagiza vitu mgahawani bila kukupa hata cent na ole usilete utatafuta pa kulala.
Wengi walipata majeraha na kugeuka kama majangili.
Wizi: Hii ilikua ni sehemu ya maisha, vijana walevi walikua wanakupora huku unaona. Mtu akilewa anakuja saa saba usiku anabeba tranka lako huku unamwangalia anaelekea nalo msituni kulivunja. Ukimfwata anaweza kuchoma kisu, lilinipata hilo japo hawakufanikiwa kuiba simu walodhani ipo ktk sanduku.
Simu, discman na vifaa vingine vya thamani vilikua vikiibiwa kupita kiasi na viliuzwa Moshi mjini.
Nidhamu: Kulikua na makundi mengi sana ya kihuni yaliyojihusisha na uvutaji bangi, wizi, ubabe nk. Vikundi kama Ragamafi, jumba la dhahabu nk. Kila kikundi kilikua na viongozi na hakikutaka kuonewa hali iliyopelekea baadae shule kufukuza kidato cha tatu na nne wote tokana na machafuko ya mara kwa mara.
Uhasama na Umbwe sekondari: Hizi zilikuwa ni shule mbili za wavulana zilizokuwa zikioneshana ubabe na wakati mwingine kuvamiana na kutwangana. Baadhi ya wanafunzi waliuwawa ktk uvamizi uliokua unafanywa.
Pia wezi kutoka uraiani kuuwawa ilikuwa ni jambo la kawaida sana. Hali hii ilitunyima hata uhuru wa kutembea kijijini.
Maandamano: Kuna siku alifariki mwanafunzi mwenzetu kwa uzembe wa kimatibabu, tuliamshwa saa kumi asubuhi tukaanza maandamano 25 km mpaka Moshi mjini. Tuliziba upande mzima wa barabara na ilibidi wakati wa kurudi tukodishiwe fuso za kuturudisha maana idadi yetu ilikuwa kubwa mno.
Vita kati ya Advance na O-level: Hakika tulikua hatupendani hata kidogo, mara kwa mara yalizuka mapigano kati yetu na tulitumia silaha kama mawe, mafyekeo, majembe nk.
Polisi wa Boma ng'ombe walikua na wakati mgumu kutuliza fujo zilizokua zikitokea usiku wa manane. Wengi tulilala mashambani kuokoa maisha yetu.
Mahudhurio darasani: Kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi mahudhurio hayakuwa mazuri. Nakumbuka kidato cha pili tulikuwa 500 na tuliwekwa ktk mikondo mitano (J,K,T,U, na V). Niliwahi kuandikishwa barua na mkuu wa shule kwa kutoonekana darasani miezi mitano kwani hata mwalimu wa darasa alisema hanifahamu na hajawahi kuniona.
Kidato cha 3 na 4 kufukuzwa shule: Kutokana na nidhamu mbovu kulitokea ugomvi mzito baina ya makundi ya wahuni na viongozi ambao ulipelekea hasara kubwa na shule kufungwa kwa muda. Kila mwanafunzi ililipa faini ya sh.9000/= na baada ya hapo kidato cha 3 na 4 tulifukuzwa wote na kupewa ofa ya kuhamia shule yeyote ya kata.
Tulipakana na shule kama: Lyaskika, Somsom, Narum nk ambapo tulikua tunapoozea mioyo kwa mabinti wa shule hizo.
Waweza ongeza lolote kwa uliyepitia mambo hayo:
Leo nimeona niwaelezee japo kwa ufupi mateso nliyokumbana nayo ktk shule ya wavulana Lyamungo iliyopo wilaya ya hai mkoa wa Kilimanjaro.
Enzi za utawala:-
-Gervas.
-Wandiba.
-Mtera.
Nilipojiunga kidato cha kwanza nilipokelewa na waalimu na kupangiwa bweni la Agrey, wakati napelekwa bwenini nlisikia sauti zikiuliza kama nimebeba Mbuzi (mkate) na wengine kuulizia nimebeba dekio (kumbe kazi ya kidato cha kwanza ni kudeki shule nzima).
Usafi: Bweni letu (yote manne: Aggrey, Shaban robert, Lumumba na Amri Abedi) yalikuwa ni ghorofa moja lenye vyumba ishirini (kumi juu na kumi chini). Kazi ya kudeki bweni ilikua ni form one hivyo tulipangiwa vyumba viwili, kimoja juu na cha pili chini kudeki kila siku saa nne usiku baada ya prep.
Kulikuwa na utaratibu wa kumwagwa maji bweni zima na kikundi kilichoitwa "mwaga-maji" kisha ndo tuanze kudeki wakati mwingine bila taa na ukidek juu ukienda chini, juu maji yashaingia kweny chumba tena.
Mara nyingi tuliamshwa saa nane usiku na kulazwa sakafuni kisha kumwagiwa maji na kupigwa mikanda kisa hatujadeki vizuri. Tulikata tamaa na shule.
Jukumu la kudeki kordo za shule nzima lilikua la kwetu pia, hivyo tulikua kama watumishi wa shule na ikipita siku bila kupigwa vibaya unashukuru Mungu.
Kuna wakati tulipigwa marungu ya migongo mpaka kuvimba huku wengine wakiingizwa kwenye masink yenye utelezi wa kijani (fangasi), mabaki ya chakula na kufunguliwa bomba za maji.
Nilipochoka mateso hayo niliamua kuomba kazi kweny mradi wa Ng'ombe ambapo tulikua tukizoa mbolea na kuchunga ng'ombe siku ya Jumamosi, wengine walikua kwenye mradi wa nguruwe.
Chakula: Shule ilikuwa na Wanafunzi zaidi ya 3000 na utaratibu wa kula ilikua ni kwa mstari, tulipigwa sana mikanda kutokana na vurugu za mstari na tulikua wa mwisho kula. Mara nyingi tulikosa chakula au tulipata ugali na kukosa mboga.
Mzee Manase (Zizu) alikua mpishi katili sana, akiwa kwenye foleni kabla hujafika kwenye sufuria ashakurushia ugali uudake sasa ole wako uanguke chini. Huyu mpishi akigawa haangalii sura ila ole wako urudie chakula lazima akudake mkono na kichapo kizito. Alipenda kutukana sana. Wengine ni mzee Urasa na Mzee mwingine wa kijiji cha Narum.
Vijana toka kanda ya ziwa walikua vinara wa kula sana, walikua wakiitana "tuigonge" maana watatu wanaweza gonga dish zima la msosi. Tuliwaheshimu sana kwa kula yao japo hawakua smart.
Viongozi Miungu: Viongozi wa serikali ya wanafunzi walikua miungu watu.
Head boy alikuwa Isaya na makamu wake Lema. Waziri wa chakula Saika na wengine. Hawa walikua wakifanya kila walichotaka na walipiga hata kwa nondo bila kuhojiwa na mtu. Mpaka walimu waliwaogopa tokana na karate uchwara zao.
Viongozi walikuwa wakiagiza vitu mgahawani bila kukupa hata cent na ole usilete utatafuta pa kulala.
Wengi walipata majeraha na kugeuka kama majangili.
Wizi: Hii ilikua ni sehemu ya maisha, vijana walevi walikua wanakupora huku unaona. Mtu akilewa anakuja saa saba usiku anabeba tranka lako huku unamwangalia anaelekea nalo msituni kulivunja. Ukimfwata anaweza kuchoma kisu, lilinipata hilo japo hawakufanikiwa kuiba simu walodhani ipo ktk sanduku.
Simu, discman na vifaa vingine vya thamani vilikua vikiibiwa kupita kiasi na viliuzwa Moshi mjini.
Nidhamu: Kulikua na makundi mengi sana ya kihuni yaliyojihusisha na uvutaji bangi, wizi, ubabe nk. Vikundi kama Ragamafi, jumba la dhahabu nk. Kila kikundi kilikua na viongozi na hakikutaka kuonewa hali iliyopelekea baadae shule kufukuza kidato cha tatu na nne wote tokana na machafuko ya mara kwa mara.
Uhasama na Umbwe sekondari: Hizi zilikuwa ni shule mbili za wavulana zilizokuwa zikioneshana ubabe na wakati mwingine kuvamiana na kutwangana. Baadhi ya wanafunzi waliuwawa ktk uvamizi uliokua unafanywa.
Pia wezi kutoka uraiani kuuwawa ilikuwa ni jambo la kawaida sana. Hali hii ilitunyima hata uhuru wa kutembea kijijini.
Maandamano: Kuna siku alifariki mwanafunzi mwenzetu kwa uzembe wa kimatibabu, tuliamshwa saa kumi asubuhi tukaanza maandamano 25 km mpaka Moshi mjini. Tuliziba upande mzima wa barabara na ilibidi wakati wa kurudi tukodishiwe fuso za kuturudisha maana idadi yetu ilikuwa kubwa mno.
Vita kati ya Advance na O-level: Hakika tulikua hatupendani hata kidogo, mara kwa mara yalizuka mapigano kati yetu na tulitumia silaha kama mawe, mafyekeo, majembe nk.
Polisi wa Boma ng'ombe walikua na wakati mgumu kutuliza fujo zilizokua zikitokea usiku wa manane. Wengi tulilala mashambani kuokoa maisha yetu.
Mahudhurio darasani: Kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi mahudhurio hayakuwa mazuri. Nakumbuka kidato cha pili tulikuwa 500 na tuliwekwa ktk mikondo mitano (J,K,T,U, na V). Niliwahi kuandikishwa barua na mkuu wa shule kwa kutoonekana darasani miezi mitano kwani hata mwalimu wa darasa alisema hanifahamu na hajawahi kuniona.
Kidato cha 3 na 4 kufukuzwa shule: Kutokana na nidhamu mbovu kulitokea ugomvi mzito baina ya makundi ya wahuni na viongozi ambao ulipelekea hasara kubwa na shule kufungwa kwa muda. Kila mwanafunzi ililipa faini ya sh.9000/= na baada ya hapo kidato cha 3 na 4 tulifukuzwa wote na kupewa ofa ya kuhamia shule yeyote ya kata.
Tulipakana na shule kama: Lyaskika, Somsom, Narum nk ambapo tulikua tunapoozea mioyo kwa mabinti wa shule hizo.
Waweza ongeza lolote kwa uliyepitia mambo hayo: