Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 123,593
- 234,219
Nikiwa kama Mtanzania na Mzaliwa wa Kyela mkoani Mbeya nawasilisha maombi kwa kila mwenye huruma kuiombea kyela .
Barabara inayozunguka soko kuu ambayo kwa ujumla wake haifiki hata kilometa 5 iko kwenye ujenzi kwa zaidi ya mwaka ! Haya ni maajabu ! Wananchi na wafanyabiashara wanaendelea kula vumbi kwa kipindi chote hicho , hata namna ya utengenezaji wake unatia shaka kubwa sana , ama ni wa kisasa zaidi au ni wa kizamani sana , wanamwaga kwanza rami halafu ndio kokoto zinawekwa juu yake , sijawahi kuona !
Kipande kidogo namna hii kinajengwaje kwa kipindi kirefu namna hii ? Ikumbukwe kwamba vifusi vilimwagwa miezi kadhaa kabla ya uchaguzi baada ya kishindo kikubwa cha UKAWA Kupitia mgombea wake wa ubunge Abraham Mwanyamaki , Sasa hivi wameziba njia kutoka mafura soap hadi mjini , hatufahamu ukarabati wa kipande hicho utakamilika lini kama hili tu limechukua zaidi ya mwaka na bado hatujui litaisha lini .
Nimetembelea eneo la ukarabati , nilichokiona ni aibu ! Mafundi wanatumia sululu kuchimbua barabara ili waweke viraka ! Ukiangalia barabara ya kyela kutoka mjini hadi Nkuyu , njia panda ya ipinda , imejaa viraka mithili ya ubao wa kuchezea draft ! Wako wapi viongozi wenye uchungu na kyela ? Ni lini magari ya abiria yataacha kupita kwenye vinjia hatarishi vilivyojaa vumbi na mawe makubwa ambayo ni hatari kwa usalama wa magari na abiria ?
Mungu ibariki Kyela .
........... Itaendelea .......
Barabara inayozunguka soko kuu ambayo kwa ujumla wake haifiki hata kilometa 5 iko kwenye ujenzi kwa zaidi ya mwaka ! Haya ni maajabu ! Wananchi na wafanyabiashara wanaendelea kula vumbi kwa kipindi chote hicho , hata namna ya utengenezaji wake unatia shaka kubwa sana , ama ni wa kisasa zaidi au ni wa kizamani sana , wanamwaga kwanza rami halafu ndio kokoto zinawekwa juu yake , sijawahi kuona !
Kipande kidogo namna hii kinajengwaje kwa kipindi kirefu namna hii ? Ikumbukwe kwamba vifusi vilimwagwa miezi kadhaa kabla ya uchaguzi baada ya kishindo kikubwa cha UKAWA Kupitia mgombea wake wa ubunge Abraham Mwanyamaki , Sasa hivi wameziba njia kutoka mafura soap hadi mjini , hatufahamu ukarabati wa kipande hicho utakamilika lini kama hili tu limechukua zaidi ya mwaka na bado hatujui litaisha lini .
Nimetembelea eneo la ukarabati , nilichokiona ni aibu ! Mafundi wanatumia sululu kuchimbua barabara ili waweke viraka ! Ukiangalia barabara ya kyela kutoka mjini hadi Nkuyu , njia panda ya ipinda , imejaa viraka mithili ya ubao wa kuchezea draft ! Wako wapi viongozi wenye uchungu na kyela ? Ni lini magari ya abiria yataacha kupita kwenye vinjia hatarishi vilivyojaa vumbi na mawe makubwa ambayo ni hatari kwa usalama wa magari na abiria ?
Mungu ibariki Kyela .
........... Itaendelea .......