Nawaonea wivu wakenya

Nawaonea wivu wakenya

Sio kila wivu ni mbaya kuna nyivu zinazoleta faida na kuna nyivu zinazoketa magonjwa ya moyo na kadhalika.

Hatimaye wakenya wamefanikiwa kuwa na usafiri wa ndege moja kwa moja kutoka Nairobi(Kenya) mpaka New York(Marekani) Hongera sana kwa Uhuru Kenyata na wakenya kwa ujumla.

Haya mafanikio hayajanipa wivu...kilichonifanya niwaonee wivu wakenya. Ni hulka yao ya kupongeza maendeleo kwa mstakabali wa nchi yao.

Sijasikia wala kuona wapinzani (Kina Odinga na wenzake) wakipinga au kukosoa maendeleo haya.

Wakenya wote, matajiri kwa maskini wamefurahia na kuimba nyimbo za uzalendo. Kwa kweli nimeona wivu.

Ingekuwa hapa kwetu, kuna watu wapinga kila kitu wangetukana na kukejeli. Cha ajabu watanzania wengi wamempongeza Uhuru Kenyata wakati huo huo wakiponda shirika la ndege la Tanzania.

Wameshindwa kukumbuka kuwa kabla ya Magufuli kuwa rais, serikali haikuwa na ndege za abiria za kuaminika na shirika lilikufa.

Sasa shirika limenunua ndege kutoka Canada na Marekani watu wanakejeli eti hazitadumu mara mapanga...

Kwa kweli aliyeturoga kafa...




MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA.

MUNGU MUBARIKI MTUMISHI WAKO MAGUFULI MKOMBOZI WA TAIFA KUBWA LA TANZANIA.


View attachment 915620View attachment 915621View attachment 915622
Wapinzani hawawezi kupinga mtu anapofuata taratibu za manunuzi. Kwa hiyo unadhani Kenya asingefuata taratibu wangemchekea kwa kuwa ananunua ndege tu.

Tatizo ndugu zetu ccm akili mnatunziwa Lumumba.
 
Huwezi kutufananisha na wakenya hata siku moja Tanzania ubabaishaji mwingi kwa mambo ya kawaida (nitayaeleza baadae)

Nadhani ungeishi Kenya ungefaham vizuri zaidi..unadhani kenya walificha ficha mambo yao kwa wananchi? Waliwaficha bei halisi za ndege? Waliwaficha kama ni mtumba au mpya? Waliwaficha kwanini wamezipata kwa wakati? Waliwaficha kama wanadaiwa na nchi husika deni lililosababishwa kwa uzembe wa kiongozi? Waliwaficha wananchi wao kuhusu nini wamefanya ndege ikaachiwa, je walilipa faini ya fedha ambazo ni kodi zetu??

Usikubali kupelekeshwa na kuonwa kama mjinga flani hivi kwamba usipate taarifa sahihi bali ukae utulie kuona mambo mazuri tu
 
Hivi unaanzaje kuilinganisha Kenya na Tanzania ktk maendeleo? KENYA NI HABARI NYINGINE KABISA.

Umeanza vizuri thread yako ila umaliziaji wako umebainisha wewe ni mtu wa aina gani.

KENYA IACHE ILIVYO, ulishawahi kujiuliza ni jinsi gani inasurvive mbele ya Alshabab?

Ulishawahi kujiuliza jinsi gani inasurvive mbele ya ukabila mkubwa?

Kenya ina maadui hawa, ugaidi wa alshabab na ukabila mkubwa ambao Tanzania haina lakini wanatuzidi kimaendeleo kila kukicha.

Hatahivyo Kenya inakimbilia ubepari uliokomaa lakini Tz haieleweki inakimbilia ubepari mchanga au inarudi kwenye ujamaa kwa kuimarisha serikali na kudhoofisha sekta binafsi.
 
Sio kila wivu ni mbaya kuna nyivu zinazoleta faida na kuna nyivu zinazoketa magonjwa ya moyo na kadhalika.

Hatimaye wakenya wamefanikiwa kuwa na usafiri wa ndege moja kwa moja kutoka Nairobi(Kenya) mpaka New York(Marekani) Hongera sana kwa Uhuru Kenyata na wakenya kwa ujumla.

Haya mafanikio hayajanipa wivu...kilichonifanya niwaonee wivu wakenya. Ni hulka yao ya kupongeza maendeleo kwa mstakabali wa nchi yao.

Sijasikia wala kuona wapinzani (Kina Odinga na wenzake) wakipinga au kukosoa maendeleo haya.

Wakenya wote, matajiri kwa maskini wamefurahia na kuimba nyimbo za uzalendo. Kwa kweli nimeona wivu.

Ingekuwa hapa kwetu, kuna watu wapinga kila kitu wangetukana na kukejeli. Cha ajabu watanzania wengi wamempongeza Uhuru Kenyata wakati huo huo wakiponda shirika la ndege la Tanzania.

Wameshindwa kukumbuka kuwa kabla ya Magufuli kuwa rais, serikali haikuwa na ndege za abiria za kuaminika na shirika lilikufa.

Sasa shirika limenunua ndege kutoka Canada na Marekani watu wanakejeli eti hazitadumu mara mapanga...

Kwa kweli aliyeturoga kafa...




MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA.

MUNGU MUBARIKI MTUMISHI WAKO MAGUFULI MKOMBOZI WA TAIFA KUBWA LA TANZANIA.


View attachment 915620View attachment 915621View attachment 915622
Kenya kila jambo linalofanyika linafanywa na serikali yawananchi wa Kenya na si serikali ya Kenyatta au ya Jubilee. Wakenya wanaheshimu sana katiba ya nchi ndivyo sababu mambo yao hayatekwi na vyama, tatizo hapa kwetu maendeleo hayaletwi na wananchi yanaletwa na CCM! Wakati kodi ni yetu sote.
 
Back
Top Bottom