Navunja ndoa ya mtu!!!!

Rafiki we kubali tu ulivunja mipaka ya mahusiano na huyo bidada.. So tafuta solution na uache ubishi lol

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Tatizo watu wanachanganya kazi na mapenzi...
Sasa watu wanataka kazi zilale, deadline zisifikiwe, kisa kuna mke wa mtu mumewe mkali asipigiwe simu?
Hivi huyo jamaa mwenye wivu, mkewe angekuwa na kazi za kusafiri kwenda mkoa ama nje ya nchi kama wiki hivi..hiyo kazi ingefanyika kweli? Tusiwatumie wanawake kama vyombo ya moto...Yaani lazima ukishikie usukani ndipo kiende mbele.
Wanawake ni partners wetu kwenye mahusiano...
Wivu usio na mipaka hauna maana katika zama hizi za kisimbuzi (king'amuzi) na Dijiti (dijitali).
 
Hayo sio mapenzi ni upuuzi...yaani kweli kuna wengine wana shida.
 

Afadhali umejua kuwa wewe ndiyo chanzo.

Ulipoona mumewe ameanza kuingiwa wasiwasi na wewe ulifanyaje? Hilo ndilo kosa lako la kwanza.

Hata wewe fikiria, mtu kaenda kumpokea mumewe toka safari,kwanza maana yake hawajaonana muda kiasi, halafu njia nzima anaongea na wewe, hadi anafika nyumbani anaongea na wewe, hadi saa 2 usiku?! Ungekuwa wewe ungejisikiaje?

Kulikua na ulazima gani wa wewe kumpigia simu hadi saa 2 usiku eti kisa unamsaidia kazi?
Maana hawakuweza kuongea habari zozote za familia yao hadi ulipokata simu, hivyo ni kama vile huyo dada alikua kazini tu, mumewe angeweza kwenda hata kwa tax nyumbani.

Kosa la huyo dada pia ni kukuendekeza, angeweza kukwambia kama huwezi kuifanya (maana ulimpigia simu mda wote aliokuwa anaifanya, hivyo ni kama aliifanya mwenyewe) ataifanya hiyo kazi mwenyewe siku iliyofuata ili apate muda wa kuwa na mumewe.
 

pamoja mdau wa oldtrashboard, pamoja na vitasa ulivyompa bwana tai, ushauri na somo kalipata!!!
 
Mvaa Tai

Pole kwa matukio yaliyokukuta. Maelezo yako hayawezi kuwa na jibu la moja kwa moja, nafikiri hata siyo sawa kumlaumu mume wa huyo dada kwani hapa hatujapata maelezo toka kwake.


Kuna uwezekano wewe ni mhanga tu wa matatizo yaliyokuwepo toka kabla ya siku hiyo, sijui uhusiano wa kindoa kati ya huyo dada nia mumewe ulikuwaje kabla ya mkasa uliokukuta.

Ndoa huwa zinabeba mambo mengi, maelezo yako yangekuwa na msaada sana kama uhusiano wako na huyo dada ungekuwa zaidi ya kikazi, yaani mnaongea hata mambo ya kindoa, maana ungekuwa unatoa maelezo ukiwa na ufahamu wa maisha yao ya ndoa.

Pili, je una hakika pasi na shaka yeyote kuwa huyo dada hana hisia zozote na wewe? Si ajabu amekuona huelekei, lakini kama ungeamua kufanya uamuzi wa kusaliti ndoa yako asingekuwa na hiyana. Unaweza kuwa unajua, au hutaki kujua, lakini wapo watu wanakuwa obsessed na waume/wake za watu, na kwavile hakuna anachoweza kufanya, hivyo hata mawasiliano ya kawaida yanasaidia kuwapa furaha. Bahati mbaya sana, ukiwa na mwenzi smart ni rahisi kuona kama mwenzi wake ana mahusiano yasiyo ya kawaida. Jaribu kuchunguza. Angalia sinema inaitwa " The Perfect Assistant"

Kama ulichosema ni kweli kwa pande zote, ningekushauri ufanye yafuatayo:- Wasiliana na huyo dada, ajue unataka kuokoa ndoa yake kwani una hisia wewe ni chanzo cha mgogoro katika ndoa yake.

- Kwavile yeye anawafahamu watu ambao mume wake anawaheshimu na anaweza kuwasikiliza, muombe akupe angalau contact za watu wawiili ambao utaweza kukutana nao, ni vizuri zaidi akawa mtu mmoja.

- Kutana na huyo jamaa, ikiwezekana wawili sehemu ya public kama hotel, bar etc. Huyo jamaa muelezee yote unayojua, na muombe akusaidie kukutanisha wewe na huyo mume wa mfanyakazi mwenzako.Katika yote unayofanya, hakikisha mkeo anajua na una mtu mwingine unayemuamini unaongozana naye na si lazima yeye ashiriki kwenye mazungumzo yenu.

Naamini ukifanya hayo itakusaidia, kukufanya uwe huru, lakini kujenga uaminifu kwa mkeo na mume wa mfanyakazi mwenzako. Ugomvi unahusisha wivu wa kimapenzi wakati fulani unapelekea watu kufanya maamuzi ya kutisha sana, ambayo wanakuja jutia baadaye.
 

Niwe mkweli yule dada tunaheshimiana sana kiasi kwamba ilikuwa vigumu sana hata kuanza kuzungumza mambo ya ndani ya ndoa yake, sembuse kuwa naye kimapenzi? Sikatai huenda yeye anahisia fulani kwangu lakini mimi sijawahi kufikiria kuwa naye kimapenzi, siyo kwamba hana mvuto lakini kwa namna tunavyoishi naye na tunavyoheshimiana sikuwahi kufikiria huko, isitoshe mimi huwa siwezi kujiingiza kwenye mapenzi na office mate
 

ushauri mzuri sana na pia naomba uwe makini maana wivu huwa mbaya sana jamaa anaweza toa hata roho yako
 

Kama vp fanya kweli!
 
Kwanza kaa mbali na huyo jamaa hii kwa ajili ya maisha yako na familia yako

Pili ushajifunza jinsi ya kusihi na wake za watu ogopa sana hatari kuliko

Tatu mkeo anajua ili sakata au umekaa kimya kwa kuogopa atakuja juu

Nne futa ushauri wa waliotangulia kwa kuuchambua vzr
 

Mkuu mimi nakushauri in the long RUN,Short run nawaachia wengine,
Jitahidi kuwa nae mbali,mkiwa kazini fanyeni kazi kama kawaida,ila punguza ukaribu,hii imetokea hata kazini kwetu,si unajua mambo ya kazi? lunch wanatoka wote,kazi wote,kurudi wote,mbaya zaidi mpaka sms zilishaonwa na wanoko za kushukuru maloveee,so in the long run Keep Distance mkaka,kazi mnafanya wote,so unazielewa,inakuwaje mpaka akiwa home,on the way to home wampigia mke wa mtu?Keep Distance bwana....,Tatizo la vijana wa kisasa anataka awe anasaidia kila kitu kikazi,mwisho ukitaka kujua ukweli kazini watu wanasemaje kuhusu ukaribu wenu?lazima watasema kitu flani ambacho wewe kwa sasa hukioni,Keep Distance.....unakuta simu yake imejaa call zako,sms zako,we are human being bwana,hata kama ni za kikazi.au wewe ni mgeni wa kazi mpaka kila muda umpigie?Keep Distance which will remove worries....Mawazo yangu tu ya Long Run
 
Tatizo uelewa wa Maisha ya Kindoa, hata kama mnaongea mambo ya kikazi, lazima kuwe na kikomo cha maongezi, embu fikiria ametoka kumpokea mumewe airport, wewe una muweka bize na simu, hv unafikiri ni ustaarabu? Je kama mlikuwa na mahusiano ya karibu ya kikazi ingekuwa rahisi hata familia zenu kufahamiana, hapo mambo mengine yasingejitokeza, inaoneka si wewe wala huyo mwanamke aliyekuwa muwazi kwa ubavu wake, ndo maana jamaa kawa mkali. Lazima upime mawasiliano unayoyafanya na Mume au Mke wa mtu. Wapo wengi wenye mahusiano kama yako na huyo mwanamke lakini kwa sababu wamekuwa wawazi kwa familia zao tangia awali hakuna tatizo!! Sikutetei wala kukuunga mkono wala kukushauri, jirekebishe
 
Jamaa kakosea kumpiga bila ushaidi, kuishi na mtu wa kuhisi hisi ni hatari sana!! msiwazoee mno wake za watu jamani!!
 
Always wedding calculation is one plus one is equal to one
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…