Nauza nissan xtrail mil9.5

Nauza nissan xtrail mil9.5

Mimi mwenyewe nimebaki nimeduwaa, hata Mimi Nina Nissan xtrail 2005 inaingia mwaka wa pili sasa nasukuma ndinga bila tatizo lolote... service tuu ndo nafanya na hii gari iko more comfortable kuliko hata rav 4. sasa sielewi wabongo wana ugonjwa na toyota au gari isipokuwa toyota ni bovu. acheni ushamba hizo ni roho za kimaskini.
Hata mie nashangaa kwamba Extrail gari mbaya. Nimetumia na naendelea kuitumia gari ipo vizuri. Matatizo ni ya kawaida kama magari mengine yote. Mwanzoni walikuwa wanasema hakuna spare ila kwa sasa kuna spare za kumwaga . Sijaona tatizo kubwa na gari hili.
 
Nimetumia Nissan X-trail huu ni mwaka wa tatu sasa, na naweza kuwahakikishia ni gari nzuri sana. Ni low maintanance, na ukilitunza vizuri utadumu nalo. Tatizo la bongo ni kwamba mafundi wazuri wa Nissan ni wachache, wengi wamezoea Toyota. Wanaweza kukuharibia gari kama na wewe hujui kutafuta information. Gari yangu iliwahi kuharibika sensor ikawa inajizima nikisimama, nikauliza baadhi ya mafundi wa mtaani...mwingine akawa anadai tushushe gear box, mwingine engine, mwingine tubadilishe control box...kumbe hawajui kitu. Nikaingia google nikaandika hilo tatizo nikapata jibu kwamba ni sensor. Nikaenda CFA motors, pale nilimpata fundi wa Nissan akanielekeza kwenye gereji yake mtaani. Haikuchukua dakika kumi kubadilisha hiyo sensor, gharama 100,000 tu, na sasa ni miaka mitatu gari haijawahi kuguswa na fundi. Najitahidi sana kutafuta information mtandaoni kabla sijamuita fundi. Hivi karibuni gari ilikuwa inamiss, na inawaka kwa shida...nikaingia google nikagundua chanzo moja wapo ni plug. Nimebadilisha plug tatizo limeisha. Sasa binafsi siwezi kununua gari mkononi kwa mtu bila kujali aina, maana siwezi kujua alikuwa analitunza vipi. Ila kama matunzo ni mazuri X-trail ni gari mmoja nzuri sana.
You have said it all!
 
Haya wataalam na wajuzi tumewasikia wa magari haya ,mi nitanunua la majaribio Tena yana ofa kwa ten navuta mchuma white Nissan ooooyi oyii
 
Tatizo mnakuwa mnasikiliza mambo ya watu amabao utakuta pengine hata baiskeli hawana. Nina Nissan Ex-trail Manual, imemaliza Mwaka mzima sasa lakini haijawahi kuguswa na fundi yeyote. gari ni matunzo tu
Ndomana limedumu, ila gari linalodumu kwa kutunzwa Pekee sio gari. Townace yangu imegonga sana lakini inadai juzi nmepga ruti ya km zaidi ya2000 Dar to songea lituhi lakini liko fresh
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom