samamba oscar
Member
- May 16, 2017
- 20
- 4
Watu wa Mungu bwana Asifiwe, salaam poleni na majukumu ya jpili.nilikuwa nahitaji ushauri wenu ndugu zangu kuhusiana na maswaiba yaliyonipata. Hi ni week yapili niliyopo kwenye hofu isiyo yakawaida na yakukata tamaa, IPO ivi week mbili zilizopita siku Kama ya Leo nilimtembelea mshakaji saloon,wakati nipo a po msela akanambia nimsaidie kunyoa yeye anaendakula.Alikuja Dogo mmoja mdogo wakati namyoa alikuwa na MBA na vidonda kichwani nikamkwangua Kikawa kinatoa damu kimoja,wakati nilipofikia kumchonga akawa analalamika namuumiza ikabidi niijaribu mashine kwenye mkono ili nivalishe jino gafla ikanikwaruza kidogo, sikuhisi chochote muda ule baada Dogo kuondoka nikaanza hisi maumivu Kwa mbali kwenye mkono kukagua Sana nikahisi kimkwaruzo kidogo ambacho huwezikukiona kiurahisi, sikuwaza kitu Kwa mdaule.ilipofika kesho yake nikaanza piga chafya siku nzima,nikaanza jipaadhabu nakumfatilia yule Dogo ukuaji wake nahistoria yake week nzima (tuko mtaa mmoja).Mama ake ni binti mzuri mweuupe shombe mnene.nikaanza kumbuka wakati najaribu ile Mashine Dogo alishika mdomo kamakushtuka.kilanikikutana nae anabadlisha njia nakukimbia.gafla week yapili Siku Kama yaleo nikaanza pata mafua(sijawahi umwa mafua ya mdamrefu hivi) na koo kuuuma,uchovu,misuli na mifupa kuuma kipele/kidonda kwenye lips ambapo nimedumu nahiyo hali hadi leo nimeamka asubuhi Leo nimetokewa na kipele kidogo kifuan chekundu kinachonga'a navingine vinaonekana Kwa mbali ambapomdawowote vitakuwa vikubwa,sijuhi kesho symptom gan ita develop ndugu zangu nme google sinahaja yakwenda kupima hiv,maana dalili zaawali Flu na Skin rushes maeneo yakifua nidalili za vvu Kwa 85% 1week mpaka 3week tokea kuambukizwa ni kwa kilamtuanayepata maambukizi.Siamini miaka 25ndoto zangu zimeishia hapa,Week hii nimetoka Pima na mpenzi wangu katoka nahappy ilamimi simanzi maana miezi mitatu ijayo majibu yangu yanaenda badilika.Nimemnyima sex nawala ajuitatizo nini sitakimuaribia life,uyu angekuwa mwanamke wa kwanza kusexnae maana siujui utupu wajinsia KE tokanimezaliwa labda kwenye pic ha/video,kujitunza kote huu ugonjwa umenifata Kwa njia nyingine naombeni msaada Kwa hasa wenyehuu ugonjwa jinsi yakuishi maisha mapya natembea huku machozi yanadondoka,mwili wote wa mazoezi umeisha nimekonda week hizi mbili nimebaki fuvu