PreGE2025 Naunga mkono hoja ya Lissu kwamba Rais apewe miaka 3 ya mpito ili kufanya mabadiliko, kisha Uchaguzi ndio ufanyike

PreGE2025 Naunga mkono hoja ya Lissu kwamba Rais apewe miaka 3 ya mpito ili kufanya mabadiliko, kisha Uchaguzi ndio ufanyike

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
2,308
Reaction score
4,687
CDM wana hoja ya msingi kabisa, kwenda kwenye uchaguzi bila uhakika 100% ya uthamani wa kura yako ni kupotezeana muda.

Leo hata kabla ya uchaguzi CCM washaanza kupangana safu za uongozi 2025 'cause they know ushindi kwao ni 100% kwa sheria na katiba yetu ni mjinga pekee anaweza kufikiri Samia anaweza kushindwa wakati yeye ndiye ndiye anateua wakuu wote wa kusimamia uchaguzi huo.

Lissu aungwe mkono ana hoja ya msingi sana kwa hatma ya nchi yetu leo na vizazi vijavyo.

No Reform No Election.
 
Itakuwa miaka ya vito na mauaji kwa yeyote aneonekana anauwezo was kusimama peke yake kifkra na upembuzi wa Mambo kuliko kuwa katika makundi makubwa yenye kuishi kwa miongozo ya vilaza.
 
Mkiahirisha uchaguzi Samia ataendelea
Mkifanya uchaguzi kwa tume hii Samia ataendelea

Kwa hiyo option ya kuahirisha ni bora tu, kwa sababu hakuna chochote cha maana kitatokea tukifanya uchaguzi kwa tume hii

Hata wale Chadema wanaotaka uchaguzi ukiangalia ni zile njaa za ubunge tu hakuna kingine. Walivyo na akili ndogo, hawaelewi kama Rais anaweza kuamua hakuna kumpa mpinzani yeyote ubunge.
 
Wazo la lissu ni mukide kabisa !! Rais apewe miaka mitatu ya mpito ili tufanye reforms za uhakika kuanzia katiba na maoni kwa wananchi kazi hii mpaka ikamilike itachukua sio chini ya miaka 3 !!

Hii itakuwa ofa tu kwa mheshimiwa rais na baada ya hapo uchaguzi uitishwe sasa na akishinda anapiga mitano Tena mpaka 2033!! Itakuwa tumemaliza Kila kitu kwa uzuri sana
Lisu anawaza tu ruzuku

Kuwa akiendelea kupokea kwa miaka hiyo mitatu ghorofa lake litakuwa limeisha kujengwa na hela ya kampeni atakuwa nayo

Jicho lote hapo liko.kwenye ruzuku ambayo mwezi huu wa sita ndio mwisho

Hizo zingine anaongea porojo tu

Kichwani anawaza ruzuku tu
 
Wazo la lissu ni mukide kabisa !! Rais apewe miaka mitatu ya mpito ili tufanye reforms za uhakika kuanzia katiba na maoni kwa wananchi kazi hii mpaka ikamilike itachukua sio chini ya miaka 3 !!

Hii itakuwa ofa tu kwa mheshimiwa rais na baada ya hapo uchaguzi uitishwe sasa na akishinda anapiga mitano Tena mpaka 2033!! Itakuwa tumemaliza Kila kitu kwa uzuri sana
Huo ndio mwelekeo sahihi, Ila utapingwa na mafisadi yaliyozoea vya kunyonga. 🤔
 
Huu ushauri angetoa mtu wa CCM lazima angeitwa chawa pro max
kwa kifupi huu ni ushauri wa kijinga na wanao unga mkono nao ni wajinga pia
waite kikao cha maridhiano\makubaliano ya mambo yafuatayo
uchaguzi uwe wa haki na uhuru
kuwepo na kalenda ya mchakato wa katiba mpya baada ya uchaguzi
 
Lisu anawaza tu ruzuku

Kuwa akiendelea kupokea kwa miaka hiyo mitatu ghorofa lake litakuwa limeisha kujengwa na hela ya kampeni atakuwa nayo

Jicho lote hapo liko.kwenye ruzuku ambayo mwezi huu wa sita ndio mwisho

Hizo zingine anaongea porojo tu

Kichwani anawaza ruzuku tu
Daaah mama samia dodooooo miaka miaka 14 kweli naungana na ww lissu anajivutia ruzuku
 
Lisu anawaza tu ruzuku

Kuwa akiendelea kupokea kwa miaka hiyo mitatu ghorofa lake litakuwa limeisha kujengwa na hela ya kampeni atakuwa nayo

Jicho lote hapo liko.kwenye ruzuku ambayo mwezi huu wa sita ndio mwisho

Hizo zingine anaongea porojo tu

Kichwani anawaza ruzuku tu
Kwahiyo unatamani waingie kwenye Uchaguzi kisha wapate wabunge wawili kisha muanze kumcheka kwamba tuliwaambia Lissu anaenda kukiua Chama sio?

Kwani kilitokea nini Mwaka 2020 ambapo Chadema walishiriki ule Uchaguzi Kwa tume hii hii ambayo Viongozi wote Wanateuliwa na Mgombea wa CCM ambaye naye anagombea URais?

Kati ya wewe na Lissu nani unadhani mwenye akili??
 
Upuuzi tu! Pia ni dharau! Mbona hamkutoa wazo hizi wakati wa John!

Nyie kama mnataka kususa Uchaguzi suseni, uchaguzi utaendelea! Hamna haki Wala uwezo wa kulazimisha hayo mnayotaka!
 
Wazo la lissu ni mukide kabisa !! Rais apewe miaka mitatu ya mpito ili tufanye reforms za uhakika kuanzia katiba na maoni kwa wananchi kazi hii mpaka ikamilike itachukua sio chini ya miaka 3 !!

Hii itakuwa ofa tu kwa mheshimiwa rais na baada ya hapo uchaguzi uitishwe sasa na akishinda anapiga mitano Tena mpaka 2033!! Itakuwa tumemaliza Kila kitu kwa uzuri sana
Siungi mkono hoja, uchaguzi ufanyike tutumie mifumo badala ya hii tume ya kitapeli ya CCM
 
Back
Top Bottom