bahati93
JF-Expert Member
- Aug 6, 2015
- 1,385
- 2,587
Ni siku ya ijumaa alasiri naelekea kituo cha mabasi ya usafiri kwa raia ndani ya jiji la dar es salaam, hii ni ijumaa tulivu jua lishaanza mapumziko yake, rangi yake maridadi ya kahawia iliyochanganyikana na yangi ya machungwa imetanda angani, hakika ni siku tulivu ndege wanaruka na kuimba kwa shangwe, miti nayo inayumba yumba na upepo mwanana wa kutoka baharini ukipuliza taratibu.
Nikiwa nikijongea kituoni nikiongozana na wanafunzi wenye furaha wakicheza michezo yao barabarani pasipo wasi wa wasi wa bodaboda, kwa mda mfupi nikakumbuka jinsi gani nilivyokuwa na furaha utotoni mwangu kipindi kile kila kitu ni mchezo hata mauwa yalipendeza Zaidi, vyakula vilikuwa vitamu muno hasa hasa pipi, katika mawazo yangu ghafla nikashtukia SHIKAMORE kwa kukurupuka nikajibu marahaba.
Katika kujibu kwangu nikaangalia ni mtoto yupi mwenye adabu na uungwana wa kusalimia wakubwa zake, nikageuza shingo na kichwa kuelekea chini ndipo nikamwona mtoto mzuri mdomo wake mdogo unaoshindwa kufunika meno yake makubwa mapya meupe kama theluji yanamweka mweka, ngozi yake ya usoni laini ikiwa imerembwa na mistari ya vumbi kwenye mashavu kutokana na michezo aliyocheza na wenzake, macho sasa meupe hayana doa yanamatarajio makubwa sana ata kwenye gizaa yatakuwa yanangaa, hakika wanajamii wenzangu yatupasa kuwajali sana watoto hawa kwani wanastaili mengii mema sana kutoka kwetu.
Basi nikiwa nimejawa na furaha tele ghafla mtoto yule nilimsikia akisema naomba pesa ya nauli, ndipo nikajua nature yake kumbe adabu yote ni kwa sababu ya kutaka pesa, daah jamani kumbe hadi watoto ni matapeli wa hisia yaani kumbe kunisalimia kote kwa sababu anataka pesa, hii tabia yapaswa kupigwa kwa nguvu zote.
Kuwa na adabu ni jambo ambalo haliitaji kulipwa, ujumbe kwa wanaoleaa watoto kwamba kuna mambo ya msingi ambayo yanasimama yenyewe kama yenyewe kama utu, heshima, uhuru hizi ni idea ambazo zinasimama zenyewe hutakiwi kumpa mtoto pesa ili aonyeshe adabu au heshima bali mtoto aonyeshe heshima kwa sababu heshima ni kitu kilichopewa thamani na jamii na mtoto atazawadiwa kuitwa mtoto mwenye heshima na jamii full stop nothing more.
Natoa onyo kwa wale wote wanaotoa pesa kwa hawa watoto wanaoomba pesa kwa gia ya shikamore, na kwa wazazi wanaofundisha maadili kwa njia ya kuhonga MSITISHE mara moja tabia hio kwani madhara yake ni exponential katika generation za huko mbele kama huyo mtoto ambaye hajajua thamani ya kweli ya heshima, watoto wake wana asilimia kubwa ya kutokujua pia. Jamani tusingangane sana kuelekeza nguvu zetu zote katika kupata utajiri wa mali kwani kuna utajiri pia wa jamii ya watu wastarabu ambayo dhamani yake haiwezi ikalinganishwa na mkusanyo wowote wa mali za kidunia.
Nikiwa nikijongea kituoni nikiongozana na wanafunzi wenye furaha wakicheza michezo yao barabarani pasipo wasi wa wasi wa bodaboda, kwa mda mfupi nikakumbuka jinsi gani nilivyokuwa na furaha utotoni mwangu kipindi kile kila kitu ni mchezo hata mauwa yalipendeza Zaidi, vyakula vilikuwa vitamu muno hasa hasa pipi, katika mawazo yangu ghafla nikashtukia SHIKAMORE kwa kukurupuka nikajibu marahaba.
Katika kujibu kwangu nikaangalia ni mtoto yupi mwenye adabu na uungwana wa kusalimia wakubwa zake, nikageuza shingo na kichwa kuelekea chini ndipo nikamwona mtoto mzuri mdomo wake mdogo unaoshindwa kufunika meno yake makubwa mapya meupe kama theluji yanamweka mweka, ngozi yake ya usoni laini ikiwa imerembwa na mistari ya vumbi kwenye mashavu kutokana na michezo aliyocheza na wenzake, macho sasa meupe hayana doa yanamatarajio makubwa sana ata kwenye gizaa yatakuwa yanangaa, hakika wanajamii wenzangu yatupasa kuwajali sana watoto hawa kwani wanastaili mengii mema sana kutoka kwetu.
Basi nikiwa nimejawa na furaha tele ghafla mtoto yule nilimsikia akisema naomba pesa ya nauli, ndipo nikajua nature yake kumbe adabu yote ni kwa sababu ya kutaka pesa, daah jamani kumbe hadi watoto ni matapeli wa hisia yaani kumbe kunisalimia kote kwa sababu anataka pesa, hii tabia yapaswa kupigwa kwa nguvu zote.
Kuwa na adabu ni jambo ambalo haliitaji kulipwa, ujumbe kwa wanaoleaa watoto kwamba kuna mambo ya msingi ambayo yanasimama yenyewe kama yenyewe kama utu, heshima, uhuru hizi ni idea ambazo zinasimama zenyewe hutakiwi kumpa mtoto pesa ili aonyeshe adabu au heshima bali mtoto aonyeshe heshima kwa sababu heshima ni kitu kilichopewa thamani na jamii na mtoto atazawadiwa kuitwa mtoto mwenye heshima na jamii full stop nothing more.
Natoa onyo kwa wale wote wanaotoa pesa kwa hawa watoto wanaoomba pesa kwa gia ya shikamore, na kwa wazazi wanaofundisha maadili kwa njia ya kuhonga MSITISHE mara moja tabia hio kwani madhara yake ni exponential katika generation za huko mbele kama huyo mtoto ambaye hajajua thamani ya kweli ya heshima, watoto wake wana asilimia kubwa ya kutokujua pia. Jamani tusingangane sana kuelekeza nguvu zetu zote katika kupata utajiri wa mali kwani kuna utajiri pia wa jamii ya watu wastarabu ambayo dhamani yake haiwezi ikalinganishwa na mkusanyo wowote wa mali za kidunia.