Natamani kuwa na mwisho mwema kama Babu wa Loliondo

Rest in peace mzee wakikombe.
Umeniachia funzo sana..kamwe nisikate tamaa kwasababu yaumri,
Unaeza kukosa kwenye ujana ukapata uzeeni kikubwa akiri nakujituma.
 
"Hatakumbukwa sana hapa duniani, ila mbinguni ana nafasi yake' Wewe ni nani mpaka ya babu wa Loliondo na Mungu wake uyajue? Acheni kupotosha watu.
 
Ok.
Pamoja na yote, alidhihirisha jinsi Wanyakyusa walivyo katika ubora wao. Yupo mwenzake alitumia imani ya aina hiyo kupukutisha watu wa ukanda huohuo,,,
Mwisho wa mtu tumwachie Mwenyezi MUNGU
 
03_11_hk6ka9.jpg
 
Kwamba bado kuna watu mnaamini kile kikombe ni tiba?

I swear Tz tuna shida bado. Ndiyo sababu unaona mvutano mkubwa juu ya chanjo kwakua Tz elimu haijasambaa kote ndiyo maana wajinga bado wengi.
 
Kwamba bado kuna watu mnaamini kile kikombe ni tiba?

I swear Tz tuna shida bado. Ndiyo sababu unaona mvutano mkubwa juu ya chanjo kwakua Tz elimu haijasambaa kote ndiyo maana wajinga bado wengi.
Ile ni kama tiba nyingine tuu kuna kupona, kuna kutopona.. Hizo tiba zingine za kuaminika kama kweli zingekuwa timamu dunia isingeugua
 
Ile ni kama tiba nyingine tuu kuna kupona, kuna kutopona.. Hizo tiba zingine za kuaminika kama kweli zingekuwa timamu dunia isingeugua
Hoja ya kwamba kwakua dunia bado ina magonjwa hivyo inahalalisha unywaji wa kikombe unaiona ni sahihi?
 
Ukiwa mhitaji na ukaambiwa mkojo ni dawa na ukanywa kwa imani unapona! BTW kabla ya tiba za kizungu hatukuwa na tiba zetu? Zilikuwa hazitusaidii?
Kwamba tiba zetu ziliponya watu kwa imani waliyokua nayo. Si ndivyo unamaanisha hapa
 
Hiki ni mojawapo ya kifo cha furaha nilichowahi kushuhudia ...! Mzee Mwaisapile almaarufu kama Babu wa Loliondo ametwaliwa kutoka maisha haya.. Mwendo ameumaliza salama ... Kwa amani na kwa furaha... Alimuishi Kristo Yesu akamtumikia Mungu kwa uaminifu mkubwa

Maneno ya Mungu yanasema maisha ya mwanadamu ni miaka 70 na ukiwa na nguvu ni miaka 80, baada ya hapo unaishi miaka ya bakshish...Naamini mzee Mwaisapile kaishi na ya ziada

Hakuwahi kujulikana popote katika kazi yake ya utumishi wa kiroho kwenye imani yake ya Kikristo kupitia kanisa la Kilutheri..alihubiri na kutumika kwenye madhabahu ya Mungu mpaka anastaafu akiwa hana kitu chochote cha thamani cha kidunia zaidi ya kibanda cha nyasi alichokiita nyumba yake. Lakini hakuwahi kulalamika popote wala kumlalamikia yeyote

Mungu anaona yote ... Naye akamwambia.. Kwakuwa umenitumikia kwa uaminifu NITAUSHIBISHA MEMA UZEE WAKO! Mara paap! Kikombe hicho
Hakujitangaza popote iwe mitandaoni, kwenye vyombo vya habari ama kutembea na maspika ALITANGAZWA kwa sauti iliyoenda mbali sana
Hakuhangaika kutafuta wasaidizi na watenda kazi..! WALIKUJA wenyewe..
Hakuhangaika kuleta WALINZI wala kuwalipa POSHO watu walijitolea

Watu wakamiminika Loliondo toka pande zote za dunia kwenda Loliondo kupata kikombe cha babu kinachoponya magonjwa mbalimbali...Habari zake zikavuma na kutangazwa mpaka na vyombo vikubwa vya habari duniani

Akawa balozi mzuri aliyeitangaza Tanzania na Loliondo kwa uzuri baada ya eneo hilo kugubikwa na migogoro na kashfa zilizosababishwa na wanasiasa WAROHO wa mali
Wanasiasa na viongozi mbalimbali wa nchi yetu hawakuwa nyuma kwenye kwenda kupata kikombe cha Babu..Mungu akaushibisha mema uzee wa babu..Mchungaji mstaafu Mwaisapile..!

Lililo kubwa na la ajabu hakutoza fedha kubwa kwenye tiba yake ya kikombe! Alitoza mia tano tuu/500 na katika hiyo yeye alichukua mia mbili tuu/200 nyingine zikaenda kwa watenda kazi na wasaidizi wake.. Na wote walitumikia kwa uaminifu mkubwa..!
Tiba ile ilikuwa na maajabu mengi
Kupitia hiyo tiba utalii ukaongezeka
Kupitia hiyo tiba Tanzania ikazidi kujitangaza kimataifa
Kupitia hiyo tiba watu wakafanya sana biashara
Kupitia hiyo tiba watu wengi wakapona maradhi yao, wengine walikufa njiani na wengine hawakupona.. Kwakuwa kila kitu kina pande mbili
Kupitia hiyo tiba tuliwaona manabii na mitume wengi katika rangi zao halisi..Wivu ukawajaa na kuanza kumshambulia babu kwa kila hali..LAKINI KAMWE HAKUJIBIZANA NAO..Alimuachia Mungu aseme nao...

Atazikwa mazishi ya kawaida kabisa. Mwili wake hautataabishwa huku na kule wala hautanuka.. Atazikwa akiwa fresh kabisa bila kuanza kuoza akiwa bado duniani..pengine hatakumbukwa duniani lakini anayo nafasi yake mbinguni siku ya kiama...
Apumzike kwa amani mtumishi mwema na mwaminifu wa Mungu.. Natamani kuwa na mwisho mema kama yeye

Mungu nisaidie

giphy.gif

Hata mimi. Hapa nipo natafuta kakitu ka kuwavuruga wabongo waingie kingi kuwa ni tiba au suluhisho la jambo fulani. Nitaiweka kama marehemu babu huyo. Yani huwezi kuthibitisha kama ni miyeyusho au la. Ukihoji sana nakwambia nimeoteshwa, wewe imani yako tu ndo itakuponya. Kw astaili hii lazima nitakufa nikiwa na furaha. Sitokosa pesa ya pweza na al-kasusu. Sema sijui kwa Mungu nako nitachomoa au atanitaiti, ndo sijui.
 
Back
Top Bottom