Natamani kumuacha ila nashindwa

sirnare

Senior Member
Joined
Nov 27, 2016
Posts
120
Reaction score
23
Habari za wakati huu wanaJF,
Naomba niende moja kwa moja, Nimekua kwenye mahusiano na binti mmoja kwa mda wa mwaka 1 na 1/2 sasa.

Nimekumbana na yafuatayo:-
-Sikujua hapendi utani, nikamtania alinichoma kalamu na kwa kua nampenda nikavumilia.

-Wewe ni shetani tu kumbe unajifanya malaika. Pale unaponihitaji tu.

Sababu kaniomba tsh. laki 2.5 nikamgomea kwasababu hiyo ndo siku tumeingiziwa boom iitoshe na yeye kaingiziwa so sote tulikua na hela hivyo nikawa mgumu kumpa maana hana sababu za msingi.

- Toka mbele ya macho yangu shetani wewe.
Hapo ni baadaye kidogo tulikua tinaelekea COET kufanya UE nikataka kumsaidia begi ndugu yangu aliniaibisha mpaka machozi yalinitoka nikachukulia poa tu.

Baada ya paper nikamfuata tuongee nikamuuliza kulikoni. Akanijibu kuna mtu alimuudhi hivyo alikua na hasira (hasira za mtu mwingine ziniangukie mimi?) (nikajisemea kimoyomoyo) Nikajitahidi sana kuropoka nikamwambia siwezi kuendelea naye tena, akajibu poa (kirahisi) (sijui alijuaje nampenda)

Tukaagana vizuri tu mida ya usiku napigiwa simu rafiki yake akidai niende nikamuone (mpenzi wangu) coz muda wote analia tu. Nikashindwa kujizuia nikaenda ndugu yangu"! Macho ya mtoto kike yalibadilika rangi nakuambia basi sijui ilikuaje nikamhug na kumsamehe kabisa.

Baada ya hapo ameendelea na tabia zake mara shetani mara toka mbele ya macho yangu mara my kuna lecture ananitongoza mambo mengi.
Kila nikitaka kumuacha naumia sana na sijui kwanini inanitokea hivi.

Ushauri wako ni wa maana sana, naomba matusi yasiwepo.
 
tatizo pesaaaaaa
 
Achana naye...huyo atakufanya usifikie malengo? Uko mwaka wa ngapi dogo? Piga shule ujiweke sawa kwanza!! Jiwekee malengo ya kupata GPA ya 5.0 uone kama utapata muda wa kupoteza!!
 
Hivi wazazi wenzangu kwanini tunapeleka hawa vijana kusoma wasichokijua wala kutilia mkazo kukijua
Mtu upo chuo kikuu lakini hujui kutofautisha Lecture (mhadhara) na Lecturer (Mhadhiri),acha ngono zingatia masomo Huyo binti si mke wako na kamwe hawezi kuwa mkeo maana kama sasa huna uwezo wa kumtunza japo kwa kidogo je utaweza vikubwa hapo baadae?
 
Endelea kua nae, sababu bado haujawa na utayari wa kumuacha
 
watoto wa shule wasiwafanye mpagawe ilhali kuna wenye haiba kama Halima Bandawe... Me kwa mabinti NISAHAULIWE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…