Jabakeke
JF-Expert Member
- Apr 18, 2019
- 386
- 355
Nimeoa mwanamke kimeo hatari,changamoto ninazozipitia kwenye ndoa yangu naamini hata shetani ananionea huruma.Nimemtembelea dada yangu nina wiki Sasa nipo hapa kwao,yeye na mumewe na watoto wao watatu,maisha ninayoyaona hapa daaaa najiona nina mkosi hawa watu wanaishi kwa upendo wa hali ya juu sana,na nilichogundua dada yangu anamheshimu na kumjali sana mumewe,na shemeji pia anampenda sana mkewe,
Shemeji ni mfanyabiashara mdogo mdogo na dada ni mtumishi serikalini,baada ya mumewe kuyumba kibiashara dada yangu ikabidi akavute mkopo benki(haya nimeambiwa na mdogo wake shemeji) dada yangu anakatwa mshahara,na dada yangu kila akitoa msaada wowote kwa wazazi kamwe hajawahi kusema Msaada katoa yeye ila mume wake,yote haya nimeyajua baada ya kufika hapa,
Je karne hii wangapi mnawafanyia haya waume zenu? Wangapi mnafanyiwa haya na wake zenu?mke anakujengea heshima kwao heshima ambayo alistahili yeye anakupa wewe mumewe,ndio maana nimejikuta ghafla nimetamani dada angekuwa ndio mke wangu,maana mke wangu mimi ni bingwa wa kunivunjia heshima kwao nk,mliooa wanawake wa namna hii hongereni Sana ,Wenzangu na mimi poleni ,tupambane na hali zetu.
Shemeji ni mfanyabiashara mdogo mdogo na dada ni mtumishi serikalini,baada ya mumewe kuyumba kibiashara dada yangu ikabidi akavute mkopo benki(haya nimeambiwa na mdogo wake shemeji) dada yangu anakatwa mshahara,na dada yangu kila akitoa msaada wowote kwa wazazi kamwe hajawahi kusema Msaada katoa yeye ila mume wake,yote haya nimeyajua baada ya kufika hapa,
Je karne hii wangapi mnawafanyia haya waume zenu? Wangapi mnafanyiwa haya na wake zenu?mke anakujengea heshima kwao heshima ambayo alistahili yeye anakupa wewe mumewe,ndio maana nimejikuta ghafla nimetamani dada angekuwa ndio mke wangu,maana mke wangu mimi ni bingwa wa kunivunjia heshima kwao nk,mliooa wanawake wa namna hii hongereni Sana ,Wenzangu na mimi poleni ,tupambane na hali zetu.