Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Huyu mi nilisha mwambia kitambo aache unafiki tunajua a&b zake
 
Lazima ataukataa tu, maana 2016 na leo 2020 kuna mengi
mradi jamaa keshanukuliwa kuwa hataongeza hata sekunde tusubirie
Principles zangu hazibadiliki. Zipo palepale.

Kama nilichompingia Magufuli 2016 bado anakisimamia, basi msimamo wangu upo palepale.

Yeyote mwingine atayetamani kama alivyotamani Magufuli, naye anapingwa tu.

Naye ataombewa ashindwe.

Tatizo nilionalo hapa, ni uwezo wenu mdogo nyie nyumbu.

Zaidi ya kusoma vichwa vya habari, mengine myasomayo hata hamyaelewi!

Kwa mfano wewe, umeelewa nini katika nilichokiandika?
 
NN naona umebadili gia angani😅
Mana we na Magu sikuhz hatukuambii kituu hehe
 
Mhhhhhhhh ,.kwny debate unamshauri aende ama asiende?
Suala la debate halina uhusiano wowote na principles zangu, ambazo msingi wake ndo ulinifanya nitamke nataka ashindwe [kuhusiana na jambo moja mahsusi].

Likija suala la debate, ni wazi kuwa msimamo wangu pia haujabadilika tokea 1995.

I am all in, ten toes down, for presidential debates.

Ngoja sasa nijibu swali lako moja kwa moja:

Ingawa mimi si mshauri wake na hivyo siwezi kumshauri, licha ya hilo, nataka mdahalo ufanyike kati ya wagombea wote wa urais.

And yes, Magufuli included.
 
Atashindwa mwaka huu
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Maxence kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hiyo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
 
Magufuli hawezi kujitokeza kwenye mdahalo, yes, ccm haijawahi kukubali mdahalo
Suala la debate halina uhusiano wowote na principles zangu, ambazo msingi wake ndo ulinifanya nitamke nataka ashindwe [kuhusiana na jambo moja mahsusi].

Likija suala la debate, ni wazi kuwa msimamo wangu pia haujabadilika tokea 1995.

I am all in, ten toes down, for presidential debates.

Ngoja sasa nijibu swali lako moja kwa moja:

Ingawa mimi si mshauri wake na hivyo siwezi kumshauri, licha ya hilo, nataka mdahalo ufanyike kati ya wagombea wote wa urais.

And yes, Magufuli included.
 
Magufuli hawezi kujitokeza kwenye mdahalo, yes, ccm haijawahi kukubali mdahalo
Na kweli akijitokeza it may cost him or polish him.,
It has a profound effect kwenye election results, hasa hapa kwetu ni kitu kigeni.,

Asipojitokeza nayo inashusha credibility..like kwani anaogopa nini?.
Ni mtego...na fursa at once

Kwa kuwa tushaingia Uchumi wa Kati basi ingekua poa tufanye matendo ya nchi za Uchumi wa Kati!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom