Anikajema
JF-Expert Member
- Mar 2, 2014
- 605
- 530
Habari wakuu.
Mimi najiona siko sawa akilini mwangu, maana nimejiona Niko tofauti sana tangu nianze maisha yakukosa mpaka pesa ya kula.... Nikiri Tu hapa katikati nimepitia wakati mgumu baada ya kupoteza pesa nyingi kweny biashara yangu mpya ambayo nimeianza na mwisho wa siku nikawa sina hata mia na biashara ikafeli, nikajikuta Nina madeni kila sehemu, hadi Mwenye nyumba akaniletea shida nikauza baadhi ya vitu nikapata nauli yakwenda Nyumbani na nia yangu nilienda Nyumbani kuipeleka familia yangu kwa mama maana naona kama hadi watoto wangekosa hela ya kula na mahitaji mengine , nilipo enda Nyumbani nikakaa huko week mbili nikarudi town sasa toka nirudi naona kabisa siko saw kiakili kwasababu hizi hapa...
...nimekuwa mnyonge hadi najitenga na watu
...kuna mda sisikii vitu vizuri,
Mtaa niliopo nimekuwa kama mgeni naona watu wanaongea kiluga sana na huu mtaa sikuwa mgeni kivile .
Naona kama Niko nyuma sana kujua vinavyoendelea duniani, ingawa simu ninayo.
...sina amani ,sina hela sina rafiki
...nimekosa kujiamini kabisa alafu nimekuwa mgumu kabisa kuelewa na nimekuwa msahaulifu mno, yaani kuna vitu vingine naweza kufanya lisaa limoja nyuma lakini naweza kukuambia nilifanya Jana.
....yaani sina swaga I mean sina point yeyote ya kuongea na watu.
....nimekuwa MTU wa kujistukistukia tu bila sababu.
....sipendi kuongea na simu kabisa na mitandao imekaa kushoto kwangu.
Kikubwa unaweza niongelesha hichi nikakujibu kingine kabisa nakurupuka hovyo na nikikaa mda wote nashika tama hata kama hakuna nachowaza, geto sipataki hata kwenda kuna siku nimelala na mlinzi kwenye kiofisi hichi nachofanyia kazi nimekuwa sijijali kabisa..... Sasa hapa naona kama vile nipo dunia nyingine au kama vile nimeamka usingizini nikakuta watu wameshaondoka tuliopanga kwenda nao safari.
Kiufupi sijielewi wakuu sasa sijui napaswa kusaidiwaje hapa.
Samahanini Mimi sio mwandishi mzuri Sana ila nafikir nimefikisha kile kinanitesa.
Mimi najiona siko sawa akilini mwangu, maana nimejiona Niko tofauti sana tangu nianze maisha yakukosa mpaka pesa ya kula.... Nikiri Tu hapa katikati nimepitia wakati mgumu baada ya kupoteza pesa nyingi kweny biashara yangu mpya ambayo nimeianza na mwisho wa siku nikawa sina hata mia na biashara ikafeli, nikajikuta Nina madeni kila sehemu, hadi Mwenye nyumba akaniletea shida nikauza baadhi ya vitu nikapata nauli yakwenda Nyumbani na nia yangu nilienda Nyumbani kuipeleka familia yangu kwa mama maana naona kama hadi watoto wangekosa hela ya kula na mahitaji mengine , nilipo enda Nyumbani nikakaa huko week mbili nikarudi town sasa toka nirudi naona kabisa siko saw kiakili kwasababu hizi hapa...
...nimekuwa mnyonge hadi najitenga na watu
...kuna mda sisikii vitu vizuri,
Mtaa niliopo nimekuwa kama mgeni naona watu wanaongea kiluga sana na huu mtaa sikuwa mgeni kivile .
Naona kama Niko nyuma sana kujua vinavyoendelea duniani, ingawa simu ninayo.
...sina amani ,sina hela sina rafiki
...nimekosa kujiamini kabisa alafu nimekuwa mgumu kabisa kuelewa na nimekuwa msahaulifu mno, yaani kuna vitu vingine naweza kufanya lisaa limoja nyuma lakini naweza kukuambia nilifanya Jana.
....yaani sina swaga I mean sina point yeyote ya kuongea na watu.
....nimekuwa MTU wa kujistukistukia tu bila sababu.
....sipendi kuongea na simu kabisa na mitandao imekaa kushoto kwangu.
Kikubwa unaweza niongelesha hichi nikakujibu kingine kabisa nakurupuka hovyo na nikikaa mda wote nashika tama hata kama hakuna nachowaza, geto sipataki hata kwenda kuna siku nimelala na mlinzi kwenye kiofisi hichi nachofanyia kazi nimekuwa sijijali kabisa..... Sasa hapa naona kama vile nipo dunia nyingine au kama vile nimeamka usingizini nikakuta watu wameshaondoka tuliopanga kwenda nao safari.
Kiufupi sijielewi wakuu sasa sijui napaswa kusaidiwaje hapa.
Samahanini Mimi sio mwandishi mzuri Sana ila nafikir nimefikisha kile kinanitesa.