Nataka kuoa barmaid. Je, nitadumu nae?

Umeongea pointi sana
Mimi nina uzoefu na hawa watu
 
Utadumu nae tu Mkuu, haina shaka kabisa.
But ikiwa tu wewe ndio Meneja au Mmiliki wa hiyo Bar anayofanyia kazi.
 
Reactions: JMF
Study case chukuwa kwa Masaburi alioa bar made na sasa ni mbunge yupo mjengoni.

Msichokijuwa wengi hawa mnaodhani ndio wanafanya kazi za maana na degree kibao ni malaya mbwa wengine wanapigwa dudu mpaka maofisini au kwenye vyoo vya ofisi.

Wengi wanafanyakazi za bar kibongobongo kwa sababu ya ukosefu wa ajira.
 
Mkuu umeishi naye mwaka mzima, halafu unauliza kama umuoe au laa. Kwa mtazamo wangu huyo ni kama umeshamuoa tu.

Pili, wewe hautakuwa wa kwanza kuoa bar maid, kuna mifano mingi ya wanaume waliojenga familia na wanawake waliwahi kuwa ma-bar maid
 
Hao watu ukioa baadhi hutulia sana ila nikuombe kitu kimoja ukioa mtafutie biashara na aachane na hiyo kazi ya awali.
 
bata ukitizama aokotavyo chakula kwenye maji machafu yenye hadi kinyesi chake na chawanyama wengine HUTOMLAaaa.
 
oa tu ila vumilia akishikwa tako mbele yako, maana kuhudumia walevi sio kazi ndogo na hatakiwi kuwakera wateja maana watahama bar
 
Kuna barmaid wengine huwa wanakosa watu makini tu, lakini akipata pa kutulia aisee huwa wanatulia kwelikweli na hapo unaweza kumwachisha kazi akawa mother house au kazi ingine bora zaidi, unaweza kumfungulia duka akafanya vizuri zaidi, oa bro
 
Nawahofia zaidi slay queens wa mjini kuliko bar maids!

Follow your heart, but remember to take your brains with you!
 
Nilishawahi kufikiria kuoa mhudumu wa bar au mdada wa kazi za ndani.
 
Mimi nimeoa huyo barmaid mwaka wa nne sasa, full amani heshima ndiyo usiseme ingawa nilipitia changamoto nyingi sana pindi nilipotangaza nia ya kumuoa, ndugu jamaa na marafiki walinisema sana zaidi ya sana sikusikia wala kujali la mtu.

Hadi sasa maisha yanaendelea.
 
Miaka miwilo hujaona kasoro yoyote jamani si umuoe tuu ila mbadilishe asifanye tena hiyo kazi kama kweli wampenda.. uone je atakubali au atakataa akikataa ujue ana lake jambo hakufai ila akikubali oa tu hana tatizo
 
Hiyo ni ajira Kama ajira nyingine japo wengi wafanyakazi wake huwa Malaya. Sasa Kama una wasiwasi mbadilishie kazi, ama mpe mtaji wa biashara ili uwe na amani.
 
Japokuwa aina ya biashara anayofanya ina changamoto zake ila kwanza tambua bar maid ni binadamu kama ilivyo wengine, japokuwa asilimia kubwa ya kada hiyo pia hutegemea kipato cha zaida toka kwa wateja kwa njia ya ngono ila bado wapo wengine ambao si wa namna hiyo, katika hili, wapo wadada wengine pia ambao sio bar maid lakini nao wanafanya siku hizi mnaita "kudanga".
Linapokuja suala la kuoa/kuolewa binafsi naona jambo la masingi ni "Utayari" wa mhusika, kwani, kuna baadhi ya mambo mtu hulazimika kuyaacha kisha kijikita ktk majukumu ya msingi kwa manufaa ya ndoa, Utayari mzuri huanzia kwenye Fikra kisha hudhihirishwa ktk mwili. Kama moyo wako umeridhia na mnapendana, wote mnatamani kuwa na familia sioni tatizo, peleka jambo lenu mbele za Mungu kwa njia ya maombi na sadaka, Mungu ndiye alindae ndoa&familia zetu, yeye ndiye awezaye kubadilisha mienendo yetu kupitia Msamaha kutokana na wingi wa Neema&Rehema.
Kila lakheri comrade.
 
Inategemea, ila mabamedi wengi ninaowafahamu wameishia kuwauwa waume zao. Tena mmoja kafa juzi kati hapa dar. Kisa bamedi yeye akiona mwanaume ana hela anajiona anamuhitaji, au anaweza kutaka amiliki hela zako zote awe na mamlaka, yaani ukabidhi kadi ya bank, pia akigundua una demu analipiza kisasi, kwa ufupi kuoa bamedi ni upuuzi, hao ni wa shetani achana naye
 
Aah aisee sijui, inategemea
mabaa maid wako aina tatu wote huhudumia walevi pombe na kazi zao kuzibua vizibo vya pombe

1.Ma baa maid wa mahoteli mfano ya kitalii
2.Baa maid wa baa za mitaani
3.Baa maid wa kwenye ndege wanaitwa Air hostess hawa hufungua pombe kwenye ndege

Ajabu wanaonyanyapaliwa hata na viongozi wa dini na hao wa baa za mitaani akiwa anafanya hotel au kwenye ndege au hoteli za kitalii hanyanyapaliwi wakati wote kazi zao ile zile za ubaa maid.Vipi mkuu AIR hostess baa maid wa angani waweza oa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…