Mkuu Bunju nafikiri ukienda kwenye ramani za City Master Plan iko kwenye ramani hiyo
Sawa inawezekana eneo lako halijapimwa ila liko katika mipango ya jiji ya kuendelezwa
What you can do ni kwamba wasiliana na watu wa Jiji au manispaa uwaambie wazi eneo lako lilipo na unachotaka kujenga na waombe kama inawezekana wakupe ramani ya manispaa ya kinondoni ile master plan uone eneo lako linaangukia wapi
Usije kujenga wakati kwenye master plan wamesema eneo hilo ni eneo la shule au wazi au wana mpango wa kujenga hospital
Ukishaona master plan sasa unaweza kuongea nao uwaambie mpango wako na wakupe ushauri cha kufanya maana wanajua namna ya kudeal na viwanja ambavyo havijapimwa
Kaushauri kidogo pima eneo lako na uwe na hati mkuu maana kujenga nyumba wakati hata hati huna ni hatari nyingine
Wakija wao wenye manguvu yao wakichukua ardhi yako na huna hata cha kuitetea utapata balaa jingine