Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Karibu nyumbani.Habari za muda huu wanajamii forum wote.. poleni na mihangaiko ya maisha...naomba niende kwenye mada moja kwa moja:
Mimi ni mtanzania ambaye nimekulia kenya.. Niliondoka Tanzania kipindi nipo mdogo kabisa na kukulia Kenya maeneo ya kilifi kwani huku ndo nimepata elimu yangu yote huku hadi dakika hii naandika hapa nipo maeneo ya huku.
Sasa nimeona sio mbaya kwasasa kubadilisha mazingira ya kuishi hasa kwa ajili ya kutafuta opportunities sehemu nyingine mbali na nilipopazoea mawazo yangu yote kwasasa ni kurudi Tanzania nchi yangu nilipozaliwa kuja kuangalia opportunities na kuliendesha gurudumu la maisha.
Sasa ndugu zangu nilikuwa naomba ushauri kuhusu maisha ya huko hasa hasa opportunities za huko? usalama wa maisha huko? Urahisi na uhakika kwenye suala zima la transportation? hali ya hewa kwa ujumla ? pamoja na baadhi ya mambo na changamoto zake:
Karibuni sana ndugu zangu napokea ushaurti wa aina yeyote.
Tafuta mke wa kikenya urudi naye au hakikisha umeacha mtoto Kenya