Nataka kuhama mfuko wa PSPF

Nataka kuhama mfuko wa PSPF

PSPF wana matatizo ila bima ya afya wana matatizo makubwa eti wanahakiki wachangiaji kwa kuwaambia wapeleke picha nza wachangiaji na wategemezi na wanasema wasipofanya hivyo huduma itasitishwa tarehe 27 januari. Pesa wataendelea kupokea ila huduma watasitisha. wangekuwa waungwana kama wangeunganisha mtandfao wao na madirisha yanayotoa huduma ili kujua kama wachangiaji ni halali au la badala ya kuwasumbua hata wateja ambao ni halali

Si kweli.. PSPF inayo utaratibu kqma ilivyo mifuko mingine ya kusajili wanachama wake na kuwapa vitambulisho vya uanachama

kumsajili mteja ktk form hii husaidia kutunza kumbukumbu na kuwa rahisi ktk mchakato wa ulipaji mafao

huduma haisitishwi... Isipokuwa ni vema kwa mtu anayetarjia kustaafu au anayechangia ktk mfuko kusajiliwa
 
Mstaafu mtarajiwa anatoa taarifa miezi sita kabla ya muda.Sasa mda ukifika inakuwaje Mstaafu aendelee kusubiria malipo wakati alishatoa notice miezi sita.

Ukumbuke kuwa PSPF haiwez kutoa mafao kama mwajiri hajakuoa kibali cha kustaafu

unaweza kutoa taarifa kwa mwajiri lakin kibali kikachelewa kutikana na sababu mbalimbali

baada ya kibali kutoka ndo unatakiwa kujaza form ya maombi ya mafao na kuambatanisha nyaraka zingine.zinazohitajika

ukweli ni kuwa ukitimiza na kufata utaratibu maoema na mafao yanashughulikiwa mapema
 
Utafuatiliaje mwaka mmoja kabla wakati huwa wanadai results slp ya mwisho utakapo staff,ukiombwa salary slp ya mwez wa kustaff utatoa nn?
 
Ukumbuke kuwa PSPF haiwez kutoa mafao kama mwajiri hajakuoa kibali cha kustaafu

unaweza kutoa taarifa kwa mwajiri lakin kibali kikachelewa kutikana na sababu mbalimbali

baada ya kibali kutoka ndo unatakiwa kujaza form ya maombi ya mafao na kuambatanisha nyaraka zingine.zinazohitajika

ukweli ni kuwa ukitimiza na kufata utaratibu maoema na mafao yanashughulikiwa mapema
Kaka usitetee ujinga wa huu mfuko me navyokwambia mstaff huyu ninaemwona anahangaika mpk ss kudai mafao yake ni ndugu yangu na kila kitu kakamilisha bt wanamzungusha tu hapo mbeya mara tuyapiga cm dar mara cjui unashughulikiwa kuwa mvumilivu toka mwez wa sita till nw
 
Kama michango ilikuwa haifiki ni wazi kutakuwa na ucheleweshwaji. Nawashauri watu wanaokaribia kustaafu wafuatilie mapema sana (walau mwaka mmmoja kabla ya kustaafu) kuhakiki kama michango yao yote imekuwa ikienda!

Pia kuna utaratibu unaofuatwa kuanzia ofisi ya mwajiri, n.k.

kaka unaanza kufuatilia mwaka mmoja kabla ukiombwa salary slp ya mwez wa mwisho unaostaff utatoa nn?
 
Tatizo ni serkali ambayo imeifanya hii mifuko kuwa saccos zake

kweli kabisa kk na tunaelekea uchaguz sintashangaa mwakan watu wakistaff wasilipwe mafao yao mpk 2016 na kuendelea
 
tuna muomba CAG achunguze huu Mfuko wa PSPF kuna HARUFU ya ufujwaji wa fedha za wanachama., mizengwe iliyopo katika malipo ni ishara ya wazi

Kabisa CAG apite na hapa kuna uozo mwingi kweny huu mfuko jmn
 
kaka unaanza kufuatilia mwaka mmoja kabla ukiombwa salary slp ya mwez wa mwisho unaostaff utatoa nn?

Mkuu hujanielewa! Nilikuwa nahimiza kufuatilia walau mwaka mmoja kabla kujua kama michango yako inawafikia au la. Ni uhakiki wa kaiwada sana na wengi wamegundua michango ilikuwa haifiki na waliwasiliana na mwajiri wao na pesa zilitumwa!

Kuwa na slipu ya mwisho ni kwa ajili ya wewe kupigiwa mahesabu tu.

Hata ukiwa unayo slipu ya mshahara wako wa mwisho.....kama michango ilikuwa haiwafikii pspf basi wakati huo ndiyo utaanza mchakato wa kufuatilia pesa ilikuwa inaishia wapi. Mpaka watakapozipata ndiyo utashughurikiwa malipo yako.

Ushauri: ni vuema kuhakiki kama michango yako inawafikia pspf n.k mara moja kwa miezi mi 3 yaani mara 4 kwa mwaka!
 
Back
Top Bottom