Nataka kuhama mfuko wa PSPF

Nataka kuhama mfuko wa PSPF

sigitoro

Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
68
Reaction score
6
Jamani naomba ushauri kuhusu huu mfuko kwasababu wastaafu wengi wanalalamika wanachelewa lipwa mafao yao kwa wakati mtu kastaafu mwezi wa sita mpk ss hajapewa mafao yake na data zote kapeleka sehemu husika haki kweli hii au pesa zetu zinaliwa huko jamani
 
Jamani naomba ushauri kuhusu huu mfuko kwasababu wastaafu wengi wanalalamika wanachelewa lipwa mafao yao kwa wakati mtu kastaafu mwezi wa sita mpk ss hajapewa mafao yake na data zote kapeleka sehemu husika haki kweli hii au pesa zetu zinaliwa huko jamani

Kama michango ilikuwa haifiki ni wazi kutakuwa na ucheleweshwaji. Nawashauri watu wanaokaribia kustaafu wafuatilie mapema sana (walau mwaka mmmoja kabla ya kustaafu) kuhakiki kama michango yao yote imekuwa ikienda!

Pia kuna utaratibu unaofuatwa kuanzia ofisi ya mwajiri, n.k.
 
Tatizo ni serkali ambayo imeifanya hii mifuko kuwa saccos zake
 
Huo mfuko hauna maana kabisa walitangaza wanatoa mkopo wa elimu mzee mzima kufika pale naambiwa mkopo ni kwa wachangiaji wa hiari siyo anayekatwa kwenye mshahara direct,nikachoka!!!!
 
Jamani naomba ushauri kuhusu huu mfuko kwasababu wastaafu wengi wanalalamika wanachelewa lipwa mafao yao kwa wakati mtu kastaafu mwezi wa sita mpk ss hajapewa mafao yake na data zote kapeleka sehemu husika haki kweli hii au pesa zetu zinaliwa huko jamani

Hii mada imelenga kuchafua mfuko ila ukweli ni kuwa PSPF ndyo mfuko unaolipa mafao bora zaidi nchini kwa sababu upo maalum kwa ajili ya ulipaji mafao... Hvyo faida yake kubwa inayopatikana ni kwa ajili ya wanachama.....

Kucheleweshwa kwa mafao husababishwa na mambo mengi ikiwemo mwajiri kutopeleka michango ya mtumishi wake.. Hivyo mstaafu mtarajiwa huna budi kufatiliwa upelekaj michango mara kwa mara kuepusha usumbufu


NB. ukihama utaumia utakapomwona rafiki yako uliyeanza naye kaz.analipwa milion 120 halafu ww unaambulia milion 70 ktk kada moja mfuko tofauti

fikiri kabla ya kutenda
 
Huo mfuko hauna maana kabisa walitangaza wanatoa mkopo wa elimu mzee mzima kufika pale naambiwa mkopo ni kwa wachangiaji wa hiari siyo anayekatwa kwenye mshahara direct,nikachoka!!!!

Huenda hukusikiliza kwa makini semina......
Fao la elimu hutolewa kwa wanachama wa mpango wa hiyari

hata hivyo.. PSPF imelishughulikia jambo hili ktk mpango wa lazima (main scheme) ambapo kuanzia mwakani JULY... watumish watakuwa na haki ya kuchukua mkopo wa elimu hadi kufikia mshahara wa miezi mitatu kwa riba nafuu
 
Huu Mfuko hauna lengo la kuwasaidia Watumishi, unamlipa mtumishi mafao yake miaka mitano kabla hajastaafu ni sawa na kumkejeli, kama kweli unalengo la kumkomboa mtumishi basi kuwepo na fursa za kukopeshwa fedha taslimu ili mchangiaji afanye jambo analo Ona linafaida kwake. Kuna haja ya kufanya mabadiliko ya sheria zinazo ongoza Mfuko huu haswa PSPF
 
Instagramboy..... Tunashukuru lakini mmechelewa sisi wazee ndiyo basi tena anyway tunashukuru pia
 
Huenda hukusikiliza kwa makini semina......
Fao la elimu hutolewa kwa wanachama wa mpango wa hiyari

hata hivyo.. PSPF imelishughulikia jambo hili ktk mpango wa lazima (main scheme) ambapo kuanzia mwakani JULY... watumish watakuwa na haki ya kuchukua mkopo wa elimu hadi kufikia mshahara wa miezi mitatu kwa riba nafuu

PSPF hawana lengo la kumkomboa mtumishi katika umaskini, waanzishe utaratibu wa Kumkopesha mwanachama wa lazima Fedha taslimu kabla hajafikia muda wa kustaafu, hakuna sababu ya kumkopesha nyumba ambayo si chaguo lake, mpeni hela akajenge nyumba anayotaka mwenyewe. Acheni kuwafisidi Watumishi
 
Jamani naomba ushauri kuhusu huu mfuko kwasababu wastaafu wengi wanalalamika wanachelewa lipwa mafao yao kwa wakati mtu kastaafu mwezi wa sita mpk ss hajapewa mafao yake na data zote kapeleka sehemu husika haki kweli hii au pesa zetu zinaliwa huko jamani

karibu nssf kwa dr.Dau huku tuna enjoy sana mkuuc
 
PSPF hawana lengo la kumkomboa mtumishi katika umaskini, waanzishe utaratibu wa Kumkopesha mwanachama wa lazima Fedha taslimu kabla hajafikia muda wa kustaafu, hakuna sababu ya kumkopesha nyumba ambayo si chaguo lake, mpeni hela akajenge nyumba anayotaka mwenyewe. Acheni kuwafisidi Watumishi

Kaka uko sahihi sana me waliniambia kama nataka nichukue mkopo wa nyumba!!me wa nini me nataka mkopo wa elimu,sasa sijaelewa mimi ninayechangishwa kwa lazima hela yangu inathamani totauti na anayechangia kwa hiyari,cha msingi ni pspf wafanya marekebisho kidogo kwenye hili jambo
 
tuna muomba CAG achunguze huu Mfuko wa PSPF kuna HARUFU ya ufujwaji wa fedha za wanachama., mizengwe iliyopo katika malipo ni ishara ya wazi
 
PSPF hawana lengo la kumkomboa mtumishi katika umaskini, waanzishe utaratibu wa Kumkopesha mwanachama wa lazima Fedha taslimu kabla hajafikia muda wa kustaafu, hakuna sababu ya kumkopesha nyumba ambayo si chaguo lake, mpeni hela akajenge nyumba anayotaka mwenyewe. Acheni kuwafisidi Watumishi

Si kweli... PSPF inatoa mkopo mkopo kwa wanachama wake kabla hata ya kufikia umri wa kustaafu

unaruhusiwa kukopa nyumba au fedha taslimu

pia jambo lingine la pekee.. Mwanachama anayo hiyariya kuchukua nusu ya mafao yake ya uzeeni miaka mitano kabla ya umri wa kustaafu kwa lazima na nusu nyingine akawa na hiyari ya kuichukua atakapostaafu kwa lazima

mfn kama ww ni askari polisi umri wa kustaafu kwa lazima labda ni miaka 50.ukifikisha miaka 45 unaruhusiwa kuchuku nusi ya mafao yako ya uzeen na kumalizia nusi iliyobak ukistaafu

au unaweza kusubiri kuchukua yote kwa mkupuo ukistaafu


pia, PSPF ni mfuko pekee unaomkopesha mtumishi ALIYESTAAFU...... Tena bila riba.... Na pesa hii hukatwa ktk pensheni ya kila mwezi anayolipwa mstaafu

hivyo PSPF imedhamiriwa kumsaidia mtumishi kukabiliana na changamoto za maisha
 
Mstaafu mtarajiwa anatoa taarifa miezi sita kabla ya muda.Sasa mda ukifika inakuwaje Mstaafu aendelee kusubiria malipo wakati alishatoa notice miezi sita.
 
Si kweli... PSPF inatoa mkopo mkopo kwa wanachama wake kabla hata ya kufikia umri wa kustaafu

unaruhusiwa kukopa nyumba au fedha taslimu

pia jambo lingine la pekee.. Mwanachama anayo hiyariya kuchukua nusu ya mafao yake ya uzeeni miaka mitano kabla ya umri wa kustaafu kwa lazima na nusu nyingine akawa na hiyari ya kuichukua atakapostaafu kwa lazima

mfn kama ww ni askari polisi umri wa kustaafu kwa lazima labda ni miaka 50.ukifikisha miaka 45 unaruhusiwa kuchuku nusi ya mafao yako ya uzeen na kumalizia nusi iliyobak ukistaafu

au unaweza kusubiri kuchukua yote kwa mkupuo ukistaafu


pia, PSPF ni mfuko pekee unaomkopesha mtumishi ALIYESTAAFU...... Tena bila riba.... Na pesa hii hukatwa ktk pensheni ya kila mwezi anayolipwa mstaafu

hivyo PSPF imedhamiriwa kumsaidia mtumishi kukabiliana na changamoto za maisha

Kaka unaudanganya umma hakuna mkopo wa pesa taslimu kwa wachangiaji wa lazima i mean mtu uliyeajiriwa then unakatwa pesa zako kwenda pspf mkopo uliopo kwa wachangiji wa lazima ni mkopo wa nyumba tena hukopeshwi hela una pesa nyumba ambayo hata haifanani na pesa utakayokatwa yaana hakuna VALUE FOR MONEY kabisa hapo.Ninachokiongea nina uhakika nacho since nilienda mm mwenyewe kwa miguu yangu pspf Golden jubilee tower nikajibiwa hayo niliyojibiwa tena kwa lugha ambayo hata sikuridhika nayo.
 
Jamani naomba ushauri kuhusu huu mfuko kwasababu wastaafu wengi wanalalamika wanachelewa lipwa mafao yao kwa wakati mtu kastaafu mwezi wa sita mpk ss hajapewa mafao yake na data zote kapeleka sehemu husika haki kweli hii au pesa zetu zinaliwa huko jamani


Mkuu usiache mbachao kwa msala upitao...

Kwa sasa PESA nyingi zimekopwa na govt baada ya budget kubuma but mambo yatatengemaa soon msiogope....

PSPF NI TULIZO LA WASTAAFU.
 
Huo mfuko hauna maana kabisa walitangaza wanatoa mkopo wa elimu mzee mzima kufika pale naambiwa mkopo ni kwa wachangiaji wa hiari siyo anayekatwa kwenye mshahara direct,nikachoka!!!!

Hata mimi mkuu walinizingua hivyo hivyo, yani sina hamu nao kabisa na ninampango wa kuachana nao kimoja kwa sababu ya weledi wao mdogo katika kuwahudumia wateja.Watu sasa wako ki-digitali wao bado wapo ki-analojia! Pu......mbavu
 
PSPF wana matatizo ila bima ya afya wana matatizo makubwa eti wanahakiki wachangiaji kwa kuwaambia wapeleke picha nza wachangiaji na wategemezi na wanasema wasipofanya hivyo huduma itasitishwa tarehe 27 januari. Pesa wataendelea kupokea ila huduma watasitisha. wangekuwa waungwana kama wangeunganisha mtandfao wao na madirisha yanayotoa huduma ili kujua kama wachangiaji ni halali au la badala ya kuwasumbua hata wateja ambao ni halali
 
Jamani naomba ushauri kuhusu huu mfuko kwasababu wastaafu wengi wanalalamika wanachelewa lipwa mafao yao kwa wakati mtu kastaafu mwezi wa sita mpk ss hajapewa mafao yake na data zote kapeleka sehemu husika haki kweli hii au pesa zetu zinaliwa huko jamani

Hama Tu Na Uhamie Mfuko Wa TEGETA ESCROW ACCOUNT na Huko Utafaidika Na Mafao Ya Bwerere!
 
Back
Top Bottom