Nataka kuacha kazi .

Nataka kuacha kazi .

Joined
May 8, 2019
Posts
38
Reaction score
68
Habari za asubuhi wana jukwaa.

Mie ni mtumishi wa umma na niliajiriwa mwaka 2013.Nina watoto wawili wa kiume,Nina viwanja vitatu ambapo kimoja nimejenga nyumba iliyoishia kwenye linta.

Toka aingie mkulu maisha yamekuwa magumu Sana,si furahii kazi yangu hata kidogo naenda tu kazini kuonekana nipo.Na siyo kuwa ni mpiga madili Wala,zamani tulikuwa tunapata hata viextra duty vinatuboost mwezi unaisha,ila saivi Nina mwaka wa tatu siijui posho.Tulikuwa tunaenda kazini hadi jmos angalau tupate chochote tulishe family.

Nimejaribu kuuza kiwanja kimoja at least nimalizie nyumba nihamie,manake Kodi inanitesa Sana huku nilikopanga ila nimekosa mteja.wanangu wanasoma mmoja baby class na mwingine class one.Bado mfanyakazi kumlipa hapo hujasaidia ndugu wanao ona nalipwa mamilioni ilihali mwisho wa mwezi napokea laki mbili na ishirini(220,000) ambayo haikidhi mahitaj yote.

Am a single parent kwahiyo mimi ndiyo baba na mama kwa wanangu.Baba yao tuliachana akaoa,na alitaka wachukua watoto ila sikuwa tayari kuacha wanangu wa under 7 years walelewe na mama wa kambo,hivyo kawasusa hatoi hata Senti tano kwaajili yao,so am their only hope.

Naona napoteza muda,nimeshafikiria hata kujirusha ghorofan ili nitoweke duniani ila nikiwafikiria wanangu roho inauma naona sitawatendea haki.So nimewaza nikaona si bora niache kazi,niuze Kila nilichonacho ingawa wateja wanakuwa tabu,nihame mji,nende sehemu nyingine nikaanze upya.Nimewaza pia kufanya nite business at least watoto wale na nipate Kodi ya nyumba,sema dhamira inakataa.

Mkuu hata Kama tulikuudhi tusamehe,tunadhalilika na familia zinateseka.Binafsi sioni faida ya kuitwa mtumishi wa umma ilhali Kuna wakati nakosa hadi nauli ya daladala kwenda kazini.Pia toka nimeajiriwa sijawahi panda cheo.

Naombeni ushauri wadau nifanyeje?je niache kazi?then niende wapi ama nifanye Nini baada ya kuacha kazi,Ningekuwa Sina watoto ningeshaondoka kitambo,tatizo mustakabali wa maisha ya wanangu utakuwaje,nikiwaza Hilo nachoka,naishia kumwaga machozi kama mtoto.
 
Habari za asubuhi wana jukwaa.

Mie ni mtumishi wa umma na niliajiriwa mwaka 2013.Nina watoto wawili wa kiume,Nina viwanja vitatu ambapo kimoja nimejenga nyumba iliyoishia kwenye linta.

Toka aingie mkulu maisha yamekuwa magumu Sana,si furahii kazi yangu hata kidogo naenda tu kazini kuonekana nipo.Na siyo kuwa ni mpiga madili Wala,zamani tulikuwa tunapata hata viextra duty vinatuboost mwezi unaisha,ila saivi Nina mwaka wa tatu siijui posho.Tulikuwa tunaenda kazini hadi jmos angalau tupate chochote tulishe family.

Nimejaribu kuuza kiwanja kimoja at least nimalizie nyumba nihamie,manake Kodi inanitesa Sana huku nilikopanga ila nimekosa mteja.wanangu wanasoma mmoja baby class na mwingine class one.Bado mfanyakazi kumlipa hapo hujasaidia ndugu wanao ona nalipwa mamilioni ilihali mwisho wa mwezi napokea laki mbili na ishirini(220,000) ambayo haikidhi mahitaj yote.

Am a single parent kwahiyo mimi ndiyo baba na mama kwa wanangu.Baba yao tuliachana akaoa,na alitaka wachukua watoto ila sikuwa tayari kuacha wanangu wa under 7 years walelewe na mama wa kambo,hivyo kawasusa hatoi hata Senti tano kwaajili yao,so am their only hope.

Naona napoteza muda,nimeshafikiria hata kujirusha ghorofan ili nitoweke duniani ila nikiwafikiria wanangu roho inauma naona sitawatendea haki.So nimewaza nikaona si bora niache kazi,niuze Kila nilichonacho ingawa wateja wanakuwa tabu,nihame mji,nende sehemu nyingine nikaanze upya.Nimewaza pia kufanya nite business at least watoto wale na nipate Kodi ya nyumba,sema dhamira inakataa.

Mkuu hata Kama tulikuudhi tusamehe,tunadhalilika na familia zinateseka.Binafsi sioni faida ya kuitwa mtumishi wa umma ilhali Kuna wakati nakosa hadi nauli ya daladala kwenda kazini.Pia toka nimeajiriwa sijawahi panda cheo.

Naombeni ushauri wadau nifanyeje?je niache kazi?then niende wapi ama nifanye Nini baada ya kuacha kazi,Ningekuwa Sina watoto ningeshaondoka kitambo,tatizo mustakabali wa maisha ya wanangu utakuwaje,nikiwaza Hilo nachoka,naishia kumwaga machozi kama mtoto.
pole sana mambo yamekua magumu kote
 
Usiache kazi kwa Sasa Cha msingi tafuta njia mbadala ambayo unaona na imeshaanza kukupa matunda au inamafanikio yeyote na baada ya kujiridhisha kua hii kitu nikikomaa nayo itanipa mafanikio Kisha ndo uache kazi, lakini ukiacha kazi huku huna njia mdala ya kukuingizia kipato unaweza ukalia zaidi ya unavyolia Sasa, pole Sana mungu atakusaidia tu, haya ni mapito tu
 
usiache kazi, utadhalilika zaidi nashauri uendelee na kaihuku ukitengeneza namna nyingine kama kujiajiri nk ni ngumu sana kupata kazi ya serikali, kazi za watu binafsi watu wanadhalilika zaidi kuliko za serikali
Kuna faida kuonekana wafanya kazi serikalini ilhali kuna wakati walala njaa na watoto?Sina sifa za kukopesheka,yani naona nilipoteza muda hata kuhangaika na shule Kama matokeo yake ndio haya.
 
Jipe moyo mkuu huko peke yako awamu hii wengi wanapitia kwenye tanuri kama lako bwana mkubwa alisema mtalimia meno na anafurahi na kukenua akiona mnalia kama hivi
 
Habari za asubuhi wana jukwaa.

Mie ni mtumishi wa umma na niliajiriwa mwaka 2013.Nina watoto wawili wa kiume,Nina viwanja vitatu ambapo kimoja nimejenga nyumba iliyoishia kwenye linta.

Toka aingie mkulu maisha yamekuwa magumu Sana,si furahii kazi yangu hata kidogo naenda tu kazini kuonekana nipo.Na siyo kuwa ni mpiga madili Wala,zamani tulikuwa tunapata hata viextra duty vinatuboost mwezi unaisha,ila saivi Nina mwaka wa tatu siijui posho.Tulikuwa tunaenda kazini hadi jmos angalau tupate chochote tulishe family.

Nimejaribu kuuza kiwanja kimoja at least nimalizie nyumba nihamie,manake Kodi inanitesa Sana huku nilikopanga ila nimekosa mteja.wanangu wanasoma mmoja baby class na mwingine class one.Bado mfanyakazi kumlipa hapo hujasaidia ndugu wanao ona nalipwa mamilioni ilihali mwisho wa mwezi napokea laki mbili na ishirini(220,000) ambayo haikidhi mahitaj yote.

Am a single parent kwahiyo mimi ndiyo baba na mama kwa wanangu.Baba yao tuliachana akaoa,na alitaka wachukua watoto ila sikuwa tayari kuacha wanangu wa under 7 years walelewe na mama wa kambo,hivyo kawasusa hatoi hata Senti tano kwaajili yao,so am their only hope.

Naona napoteza muda,nimeshafikiria hata kujirusha ghorofan ili nitoweke duniani ila nikiwafikiria wanangu roho inauma naona sitawatendea haki.So nimewaza nikaona si bora niache kazi,niuze Kila nilichonacho ingawa wateja wanakuwa tabu,nihame mji,nende sehemu nyingine nikaanze upya.Nimewaza pia kufanya nite business at least watoto wale na nipate Kodi ya nyumba,sema dhamira inakataa.

Mkuu hata Kama tulikuudhi tusamehe,tunadhalilika na familia zinateseka.Binafsi sioni faida ya kuitwa mtumishi wa umma ilhali Kuna wakati nakosa hadi nauli ya daladala kwenda kazini.Pia toka nimeajiriwa sijawahi panda cheo.

Naombeni ushauri wadau nifanyeje?je niache kazi?then niende wapi ama nifanye Nini baada ya kuacha kazi,Ningekuwa Sina watoto ningeshaondoka kitambo,tatizo mustakabali wa maisha ya wanangu utakuwaje,nikiwaza Hilo nachoka,naishia kumwaga machozi kama mtoto.
Inaonekana Una mkopo mkubwa . Tafuta wateja uuze hivyo viwanja kama utaweza ukishauza kapunguze mkopo then maisha Mengine yaendelee
 
Kuna faida kuonekana wafanya kazi serikalini ilhali kuna wakati walala njaa na watoto?Sina sifa za kukopesheka,yani naona nilipoteza muda hata kuhangaika na shule Kama matokeo yake ndio haya.
kitu pekee nachoweza kukushauri ni kwamba usikate tamaa, suala la kuacha kazi sikushauri endapo huna msingi wowote uliojiwekea kwa ajili ya kuacha kazi.

1.nyumba haijaisha
2.Watoto wanasoma
3.Kodi ya nyumba inakusumbua
4.mahitaji yanasumbua

hivyo vyote utaweza kuvimudu ukiacha kazi? ambapo hata hiyo laki mbili itakuwa si ya uhakika kuipata...usiache kazi.
 
Hayo ni mapito tu,Maisha yetu yalivyo ni kama uonavyo season za vipindi vya majira katika mandhari zetu kama kuna kipindi cha joto,Masika,vumilia maisha ndivyo yalivyo,Na pia kama unauwezo jaribu kutafuta mume uolewe huenda mawazo yakakupungikia
 
Unafanya kazi gani yaani fani ipi ,halafu mpo wangapi wa cheo hicho kuwa single parent si jinai ila USIACHE KAZI
 
Pole sana. Ukiacha kazi ndio umejimaliza. Hata hicho kidogo ulichokuwa unakipata, hutokipata. Hicho kiwanja usiuze kwa bei ya tamaa. Yani usichukue matatizo yako yote ukayajumlisha ndio ukapata bei ya kiwanja.
Watoto wasomeshe shule za nafuu. Shule za gharama zitakutesa. Panga nyumba ya kawaida sana. Hali unayopitia wewe ni ya kila mtu na kifo cha wengi ni harusi. Kama ulikopea mshahara, jitahidi kumaliza mikopo ili upate mshahara kamili. Kumlaumu Rais kuwa unapokea laki mbili na ishiri na ukute mshahara wako ni laki saba na zaidi ila umeukopa mpaka ukabaki kiduchu, itakuwa ni kumlaumu mtu kwa 'makosa au uzembe' wako mwenyewe...
Mwisho wa siku, jihusishe na shughuli ndogo ndogo za ujasiliamali iwapo mda na rasilimali zitaruhusu. Ni vyema pia ukatafuta likizo ili walau ukapumzishe akili.

Mwisho wa siku, wanawake kuweni waneyenyekevu.
Mnapata wanaume wa maana mnawatibua, na sie wanaume wapole tusiopenda mikwaruzano huwa tuna decion moja tu. You either pack and leave or I pack and leave. Sasa unajikuta uko peke ako na mizigo yote unaibeba wewe. Ukiwa mnyenyekevu mkasikizana na mwenzako mkaishi pamoja, baadhi ya changamoto mnakuwa mnazitatua kwa pamoja hivyo maisha kidogo yanakuwa na unafuu!
 
Jipe moyo mkuu huko peke yako awamu hii wengi wanapitia kwenye tanuri kama lako bwana mkubwa alisema mtalimia meno na anafurahi na kukenua akiona mnalia kama hivi
Najipa moyo vipi?nataka Sana kuacha kazi sema sijajua Cha kufanya after and hawa wanangu ntawapeleka wapi?mie yatima Sina wazazi,walezi walonilea washao doka dunian wangeweza nisaidia,ndugu waliobaki wananiona mie ndio tajiri wa ukoo ilhali naugulia ndani,inshort wote wananiangalia mie
 
Habari za asubuhi wana jukwaa.

Mie ni mtumishi wa umma na niliajiriwa mwaka 2013.Nina watoto wawili wa kiume,Nina viwanja vitatu ambapo kimoja nimejenga nyumba iliyoishia kwenye linta.

Toka aingie mkulu maisha yamekuwa magumu Sana,si furahii kazi yangu hata kidogo naenda tu kazini kuonekana nipo.Na siyo kuwa ni mpiga madili Wala,zamani tulikuwa tunapata hata viextra duty vinatuboost mwezi unaisha,ila saivi Nina mwaka wa tatu siijui posho.Tulikuwa tunaenda kazini hadi jmos angalau tupate chochote tulishe family.

Nimejaribu kuuza kiwanja kimoja at least nimalizie nyumba nihamie,manake Kodi inanitesa Sana huku nilikopanga ila nimekosa mteja.wanangu wanasoma mmoja baby class na mwingine class one.Bado mfanyakazi kumlipa hapo hujasaidia ndugu wanao ona nalipwa mamilioni ilihali mwisho wa mwezi napokea laki mbili na ishirini(220,000) ambayo haikidhi mahitaj yote.

Am a single parent kwahiyo mimi ndiyo baba na mama kwa wanangu.Baba yao tuliachana akaoa,na alitaka wachukua watoto ila sikuwa tayari kuacha wanangu wa under 7 years walelewe na mama wa kambo,hivyo kawasusa hatoi hata Senti tano kwaajili yao,so am their only hope.

Naona napoteza muda,nimeshafikiria hata kujirusha ghorofan ili nitoweke duniani ila nikiwafikiria wanangu roho inauma naona sitawatendea haki.So nimewaza nikaona si bora niache kazi,niuze Kila nilichonacho ingawa wateja wanakuwa tabu,nihame mji,nende sehemu nyingine nikaanze upya.Nimewaza pia kufanya nite business at least watoto wale na nipate Kodi ya nyumba,sema dhamira inakataa.

Mkuu hata Kama tulikuudhi tusamehe,tunadhalilika na familia zinateseka.Binafsi sioni faida ya kuitwa mtumishi wa umma ilhali Kuna wakati nakosa hadi nauli ya daladala kwenda kazini.Pia toka nimeajiriwa sijawahi panda cheo.

Naombeni ushauri wadau nifanyeje?je niache kazi?then niende wapi ama nifanye Nini baada ya kuacha kazi,Ningekuwa Sina watoto ningeshaondoka kitambo,tatizo mustakabali wa maisha ya wanangu utakuwaje,nikiwaza Hilo nachoka,naishia kumwaga machozi kama mtoto.
Kazini unatoka saa ngapi ?
Tengeneza banda la matunda hapo barabarani Jirani na ulipopanga
Ukirudi unakaa hapo mpaka saa nne unaridi zako kulala
Kwa kufanya hivyo utakuwa umeongeza kipato chako
Pambana hali sio kiukweli lakini don't give up
 
Kuna faida kuonekana wafanya kazi serikalini ilhali kuna wakati walala njaa na watoto?Sina sifa za kukopesheka,yani naona nilipoteza muda hata kuhangaika na shule Kama matokeo yake ndio haya.
Una tatizo kubwa la kisaikolojia kuliko la kikazi. Tsh 220K kwa mwezi kweli ni kipato kidogo lakini hakika nakuambia zaidi ya watanzania 85% hawana uhakika na kipato hicho mwisho wa mwezi, lakina hawajakata tamaa na hawajui watafarijika lini.

Tiba ya tatizo lako, kwanya ni:
- Kukubali kulea wanao, mtoe kabisa akilini mzazi mwenzio, pili jaribu kuangalia ni wapi unaweza kupunguza matumizi yako yanayoweza kuepukika, tatu unachokiona ni tatizo kwa sasa ni masuala ya muda tu na soon yataisha kwa kuwa ni upepo tu wa kisiasa hivyo usikutoe relini.

Kwa kuwa stage ya maisha uliyopo kama mtumishi wa umma wa kawaida siyo mbaya sana.
 
Inaonekana Una mkopo mkubwa . Tafuta wateja uuze hivyo viwanja kama utaweza ukishauza kapunguze mkopo then maisha Mengine yaendelee
Wateja hakuna kila unayemgusa hana hela,nishatumia hadi madalali,na viko sehemu nzuri tu
 
Una tatizo kubwa la kisaikolojia kuliko la kikazi. Tsh 220K kwa mwezi kweli ni kipato kidogo lakini hakika nakuambia zaidi ya watanzania 85% hawana uhakika na kipato hicho mwisho wa mwezi, lakina hawajakata tamaa na hawajui watafarijika lini.

Tiba ya tatizo lako, kwanya ni:
- Kukubali kulea wanao, mtoe kabisa akilini mzazi mwenzio, pili jaribu kuangalia ni wapi unaweza kupunguza matumizi yako yanayoweza kuepukika, tatu unachokiona ni tatizo kwa sasa ni masuala ya muda tu na soon yataisha kwa kuwa ni upepo tu wa kisiasa hivyo usikutoe relini.

Kwa kuwa stage ya maisha uliyopo kama mtumishi wa umma wa kawaida siyo mbaya sana.
Mtoa mada tatizo lake naona limeegemea katika kisaikolojia, anahitaji ushauri wa kisaikolojia zaidi
 
Pole sana mkuu,mitihani ni sehemu ya maisha,achana na wazo la kuacha kazi kwakua bado hata hio alternative huna,jitahidi kubana matumizi tu na ufanye vile ambavyo ni vya msingi tu,pia usifikirie kujiua kwakua watoto bado wanakuhitaji.

Kingine mshirikishe mzazi mwenzako kuhusu kusaidia matumizi kama hataki jaribu kwenda ustawi wa jamii ili alazimishwe kisheria kuchangia matumizi ya watoto wake.

Kuhusu 'nite business' sijaelewa vizuri lakini kama ulimaanisha kujiuza achana na hilo wazo kabisa utajiingiza kwenye matatizo zaidi

Mwisho kama unaamini katika Mungu basi ni muda wa kusali sana katika imanj yako,Kama ni mkristo jitahidi kuhudhuria ibada na hata jumuia za kusali kama zipo lakini kama ni Muislamu basi mwezi huu wa mfungo ni muda muafaka wa kufunga na kuweka mahitaji yako mbele za Mungu.

Endelea kua imara kwa ajili ya watoto wako na jipe moyo wa ujasiri naamini Mungu atakuvusha katika hili.
 
Jambo la kwanza, futa mawazo ya kujiua na nite business, utawaumiza zaidi watoto na baadae hautafaa kwa kitu chochote cha maana.

Pili, kwa kuwa una mkopo na mahitaji mengine lakini unabahatika kupata laki mbili kwa mwezi, usiache kazi isipokua kama umepata tayari kitu bora zaidi ya hii hali uliyonayo sasa hivi.

Kwa upande mwingine sikushauri kuuza vitu utauza kwa bei ya kutupa nakuishia kujuta baadae. Vinginevyo kama kuna kitu ambacho kisipofanyika kinahatarisha maisha , uhai wa mtu.

Mwisho, ndugu na jamaa inabidi waelewe tu kwamba mambo yamebadilika kwa sasa. Pia unaweza tafuta makazi ya bei nafuu kupunguza mzigo wa kodi. Ujenzi wa nyumba na mambo mengine vinaweza kusubiria.

Nyakati ngumu hazitadumu milele.
 
Back
Top Bottom