Kawaida kwa mtu anayetaka kununua vipimo vikoje
Anayehitaji tufanye biashara ya zabibu ninamkaribisha.
Ni zabibu nyekundu, zipo na hali nzuri na mikungu mikubwa.
Bei maelewano kutokana na wingi wa mzigo na ninaweza kukujumlishia shamba zima la heka moja, nipo dodoma.
Karibuni sana.
Ingekuwa ni ile nyeupe usingetangaza mkuu, jaribu kuongeza kwa kulima zabibu nyeupe, au udongo wako unagoma?
Mkuu mbona zabibu ni dili sana how comes umekosa soko? ukiwa na zabibu nyekundu unaweza wauzia jamaa wa wine hapo dodoma ukiwa na zabibu nyeupe ndo kabisaa wakenya wanazitafuta sana kwa ajili ya kuexport ulaya hasa spain
yes ni dili sana ila wanunuzi wa hapa wanapata mzigo mwingi na kusababisha kujipangia bei, wakati mwingine wanachukua kwa mkopo, kwa mfano hadi sasa tunadai madeni ya tangu msimu uliopita hata senti hatujapata.
Kama nyeupe inamea hapo shambani kwako, basi ongeza ukubwa wa shamba mkuu ili uuze nje. Zabibu tangu kuoteshwa mpaka kuvunwa ni muda gani?