Hilo ndio tatizo kubwa sana la sisi Watanzania kwamba wengi wetu tunashindwa kujiuza na kujua thamani yetu na matokeo yake watu wengi wanashindwa kupita kwenye usaili makini wa kazi kwakuwa hatujijui thamani yetu ni nini. Unaulizwa kwanini unadhani tukuchukue wewe na asiwe mwingine, unabaki unagwayagwaya tu, wapaswa ujinadi kuwa wewe ni competent na unauwezo kuliko wengine kwakuwa na sifa A,B, C......
Si kwamba najisifia ila ninajijua kuwa ni mbora kiasi gani, kwani nafanyakazi na watu waina mbalimbali kielimu, kitaifa, kwahiyo unaweza ukaona nafasi yako ipo wapi ukijima na waliokuzunguka, uwezo wako ni upi kiufanisi wa kazi, uchangiaji wa mawazo muhimu katika changamoto kubwa za kikazi na kimaisha. Vilevile unapata feedback kutoka kwa watu wanaokuzunguka kuwa wewe ni mtu wa aina gani, haiwezekani kila mtu aseme wewe ni mtu wa aina fulani halafu ikawa uongo. Sisi Watanzania tuwe na ujasiri wa kuweza kujiona ni competent people na tunaweza na kushindana na yeyote yule pahala popote pale na kwa lolote lile hasa inapokuwa suala linalohusiana na field yako. Kwa hiyo mimi najijua vizuri sana kuliko mtu mwingine yeyote yule. Tuwe nauwezo wa kufanya self-crtical analysis na evaluation ya kila kitu tunachofanya katika maisha ili tuwe na uwezo wa kujirekebisha na kuwa bora zaidi hata kama tunafanya vizuri katika nyanja fulani kwani "No matter how good you are, still there is a room for improvement.
Nadhani mmenielewa vizuri tu, si kwa nia ya kujisifu bali kueleza ukweli kuwa mimi najielewa kuwa ni nani, na amini nakwambia hii imeleta mafanikio makubwa sana katika maisha, so anza kujielewa nafasi yako wewe ni nani. Na ndo maana katika Business management and analysis kuna vitu kama SWOT Analysis, Balanced scorecards, Benchmarking etc hizo strategic tools zinazoweza kuisaidia kampuni kujua nafasi yake katika biashara ya ushindani na kujua nafasi ya makampuni yaliyomo katika the same industry ili iweze kuchagua strategy zilizosahihi zitakazowezesha kampuni hiyo ku outperform kampuni zingine. Kwahiyo hii inaweza kuwa translated kwa mtu binasfi, usipojijua wewe ni nani, strong point na weak points zako ni zipi huwezi kupiga hatua kwenye maisha. Ndo maana nasema nataka mahusiano na mtu aliye na uwezo wa kuyaelewa haya mambo ili tunapoongea tunaongea lugha tunayoelewana. Asante sana