Natafuta paka nipo Dar

Natafuta paka nipo Dar

CHE GUEVARA-II

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2010
Posts
571
Reaction score
157
Habari zenu wadau?

Naomba msaada.

Natafuta paka (domestic cats) wawili - dume na jike.
Wasio na mabaka kama ya chui.
Wenye mabaka kama ya chui wana asili ya kuwa deviant (paka mwitu)- huwa na tabia ya kukamata vifaranga na hata kuku.
Nawahitaji sana, panya wananisumbua.
Sipendi kutumia sumu au mitego - ni kinyume na taratibu za mazingira, pia hazimalizi tatizo - hupunguza tatizo tu.
Njia sahihi ni kufanya mazingira yasiwe rafiki kwa panya (i.e kutoacha mabaki ya vyakula hovyo au kutohifadhi vibaya vyakula) na biological control (kwa kutumia paka).

Natanguliza shukrani
 
Nenda muhimbili mkuu wapo nyomi ni chaguo lako tu
 
Nenda kwa marehemu bibi nyau pale. Still nyau nyau nyauuu bado wapo
 
Wewe kaa baa yoyote yenye nyama choma mfano hapo dagaa dagaa shekilango utawapata nyau hadi ushindwe kuchukua..!
 
imewasifia kweli kwa usafi
wakati mm najua Paka wana aibu na hupenda starehe sana
akishiba hakati Panya
akikuta maziwa anakomba
haja kubwa ni kwenye unga wa ugali
Achana na Paka tafuta kitabu cha gundi ni chini ya 2,000/-
utawamaliza wote kwa kunaswa

naweza kuwa-Parcel kwenye Champion Bus akawalipie pale Ubungo huku wapo wengi
 
Mtafute Mmakonde yoyote humu ufanye supply ya Kitoweo cha Panya.
Mbona utajiri unao halafu umeukalia?
 
tumegawa wengine amebaki mmoja tu mweupe dume
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom