natafuta mchumba-serious pls no jokes!!

Nilikuwa UK kwa miezi mitatu, sikuwa na muda kabisa wa kukaa na laptop ilikuwa ni mchakamchaka, na hata Blackberry ninayotumia nina access tu ya kuingia lakini kucoment siwezi hata nikilog in lakini JF inakataa comment zangu, bado sijajuwa tatizo la hii simu ni nini.
Anyway am in Dar for almost two weeks now, sweet home. Pamo1 sana.

We Mhaya??
 
Ee kweli nakuombea upate mchumba lakini masharti uliyoweka ni magumu yangekuwa mepesi kidogo ningejitokeza. Ninaupendo wa kweli kwako.
 
Mume mwema hatafutwi kwenye keyboard.

Mtaani kwenu umekosa! Shuleni umekosa! Kazini pia umekosa basi kuna uwezekano mkubwa we ni mbaya sana.

Wengine si wanaweka mada humu kwakuchallenge watu tu
 
Pole kwa upweke.

Nitamfikishia habari Kaka yangu ana sifa zote unazozitaka.

ANGALIZO. Tatizo lake ni moja, Kikojozi
 
Daah sisi wafupi jee maana sijaona hata siku moja mwanamke akataja sifa ya mwanaume anayemtaka akasema awe mfupi!!daah tuna bahati mbaya sijui!!!
 
Nina sifa zaidi ya hizo,
Tatizo age tunalingana so unaweza kuonekana kama shugamami wangu,
Wacha nikatafute wa age ya 23-28
 
Tatizo wana jf mnazodoa baada ya kushauri,nadhani kama angetaka masharobaro angeenda fb au twiter,sasa kaja kwenu wana great thinker mnajibu kama watoto wa fb,tupunguze utani dadayetu yupo serious anatafuta mme.

Dada mimi sina vigezo ulivyotaka ila nakuombea kwa Mungu umpate aliye wako na akufaaye.
 
Dada mpendwa vigezo vyako cjavifikia kwa kiasi fulani hasa umri,kwa hyo nikutakie kila la kheri na wadau acheni utani kwa bibie Noela yupo seriazi kutafuta mwenza wake
 
Pole mwaya dada angu, nakuombea mwaya utapata tu m2 wa kukuoa na kuishi happy life.
 
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 31,nina mtoto mmoja mwenye umri wa miaka miwili.elimu yangu ni shahada ya pili ninaishi dar. Ninatafuta mchumba hatimaye awe wangu wa milele,nimpende anipende awe tayari kumkubali mwanangu kama wa kwake.

Awe na sifa zifuatazo;

Mrefu mwenye mvuto,
Awe mkristo anayependa kusali na mwenye kumuogopa Mungu,
Awe mwenye mapenzi ya dhati na sio macho juu juu,
Awe mwenye kukosoa panapohitaji kukosoa na sio kukaa na gubu na kutafuta suluhu nje,
Awe mwenye elimu angalau degree moja kama si mbili,
Awe mpenda maendeleo na mwenye kuona mbali hata kama hana kitu,
Awe muwazi na si muongo,
Awe muelewa na mwenye kujali.

Kama uko serious ni-pm tuone kama tuta-cope na Mungu aweke mkono wake.

Nawashukuru na kuwatakia weekend njema.

utajuaje kama degree yake ni genuine au feki?
 
Mume mwema hatafutwi kwenye keyboard.

Mtaani kwenu umekosa! Shuleni umekosa! Kazini pia umekosa basi kuna uwezekano mkubwa we ni mbaya sana.

Kwani hawa waliopo hapa JF si ndio hao hao waliopo shuleni, na kazini? Iam the witness of a very happy marriage ya watu walioanza relationship kupitia tangazo la 'natafuta mchumba' gazetini.
Anajua anachohitaji ndio maana amejitangaza.
 
Asanteni wote mlioonyesha kuwa positive na post yangu. Be blessed.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom