Ee Mugabhoo,
Bata maji watu wengi hawajui kwa jina hilo.
Hawa hupatikana sana maeneo ya Kigoma kule Livingstone,au ule upande wa maeneo ya Machinjioni na josho,yaani maeneo ya Kibwe,chini ya Ujiji Seminary.Na hutaga sana kwenye mimeo ya viragorago inayoota kwenye maji kama matete.Au unaweza pia kuangalia wale waliopo Maeneo ya Katonga.
Pia jaribu ku deal saana na wale wanaovua Kambale na Ngege,maana ndio maeneo ndege hawa hupatikana na kuzaliana.
Kupata mayai yake au viota vyake ni shida saana,maana hawa ndege hawaishi nchi kavu kama ndege wengine.Hawa wao ni kwenye maeneo ya mkondo wa ziwa na vijito vyake.
Nwajua sana hawa niliwahi kuwafuga,na wapole sana,warefu na miguu utafikiia inakatika,wanafugika kama unavyofuga mata,ila lazima kazi iwe pevu,maana lazima uweke bwawa lenye miti ndani ili uje uasilia,laa sivyo hawazaliani.
Ila najua wewe umetumwa Mayai hayo na Mganga,maana siku hizi waganga wanawapa watu mambo magum magum saana.Maana mayai haya kama unaenda kuyatafuta mwenye basi jua Mamba au Kenge lazima wakulambe,maana hutagwa kwenye maeneo yenye maji ya lioyotulia juu ya miti iliyomo ndani ya maji.Kwa wale mnaojua maeneo ya Kibwe miaka ya 1985 basi kule mamba ndio kwao,walinikosa mara kibao
Mwambie Mganga apunguze masharti