Natafuta kazi za mtandaoni

Natafuta kazi za mtandaoni

neno ni upanga

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2022
Posts
681
Reaction score
2,293
Habari wakuu! Kama kichwa ķinavyojieleza mimi ni mtaalam wa kutumia computer na simu za mkononi lakini pia nina uzoefu wa kufanya matangazo mbalimbali mtandaoni, nina uzoefu wa kufanya content creator kwenye mitandao ya kijamii kama YouTube, Facebook, twitter, Tiktok n

sambamba na hayo ni mwandishi mzuri wa makala mbalimbali na nimewahi kufanya kazi na kituo kimoja cha t.v. nchini kenya!

ni mwepesi wa kujifunza, nina laptop na simu kubwa! Nahita mtu, au taasisi, kampuni ambayo inaweza kunipa kazi ya mtandaoni, ninaamini hiyo kazi nitafanya kwa ufanisi sana maana ninao muda mrefu wa kukaa mtandaoni!
 
Tafuta Niche alaf chukuwa bidhaa au huduma piga picha post as if ni wewe fanya biashara chukuwa chako
 
Huo uwezo wote uliouandika hapo juu kwanini unataka tena kuajiriwa kijana? Nieleweshwe kidogo.
 
Naomba utakapopata hiyo kazi nikawe msaidizi wako.. Naona tunashare baadhi ya sifa.
 
nina uzoefu wa kufanya content creator kwenye mitandao ya kijamii kama YouTube, Facebook, twitter, Tiktok n

sambamba na hayo ni mwandishi mzuri wa makala mbalimbali na nimewahi kufanya kazi na kituo kimoja cha t.v. nchini kenya!

nina laptop na simu kubwa!
nitafanya kwa ufanisi sana maana ninao muda mrefu wa kukaa mtandaoni!

Huu ni mtaji tosha.
 
Tatizo ni moja umeshindwa kujipackage vizuri namaanisha kujiuza na hili ndo tatizo kubwa sana kwetu wabongo.

Jitambulishe vizuri wewe ni nani (jina lako kibiashara),Weka portifolio ya huduma zako na bei zake,weka mawasiliano yako vizuri (namba ya simu,social media profiles nk),weka sample ya kazi ulizowahi kufanya tuzicheki au tukaangalie.

Jiuze jiuze
 
Back
Top Bottom