Natafuta Kazi nisaidieni

beautifulonyinye

JF-Expert Member
Mar 16, 2015
726
478
Habari za asubuhi ndugu zangu, Mimi ni binti wa miaka 25 elimu yangu ni kidato cha 4, natafuta Kazi kwa Mara nyingine Kazi ambazo naweza kufanya na ambazo Nina uzoefu nazo, ni:
Hotel
Duka la simu/spea n.k
Slot mashines
Sports betting.
Hizo ni baadhi ya Kazi ambazo naweza kufanya. Naomba Msaada wenu na Mungu awabariki, Asubuhi njema
 
Ukiangalia kwa undani kazi zote ulizotaja hapo juu ndizo zenye ushindani mkubwa kwa sasa hasa maeneo ya mijini, kwa kuwa kazi hizo zina wigo mpana na zinaweza kufanywa na mtu yeyote kulingana na elimu zetu za kibongo! Kama upo mjini ni vizuri ukaangalia kazi au shughuli yenye mahitaji makubwa ya binadamu, unaweza fanya biashara ya chakula ambayo ni mahitaji ya kila siku ya sisi binadamu..tatizo kila mtu anataka akae ofisini tu duh..hili ni tatizo..karibu kwenye kilimo cha mbogamboga!
 
Ukiangalia kwa undani kazi zote ulizotaja hapo juu ndizo zenye ushindani mkubwa kwa sasa hasa maeneo ya mijini, kwa kuwa kazi hizo zina wigo mpana na zinaweza kufanywa na mtu yeyote kulingana na elimu zetu za kibongo! Kama upo mjini ni vizuri ukaangalia kazi au shughuli yenye mahitaji makubwa ya binadamu, unaweza fanya biashara ya chakula ambayo ni mahitaji ya kila siku ya sisi binadamu..tatizo kila mtu anataka akae ofisini tu duh..hili ni tatizo..karibu kwenye kilimo cha mbogamboga!
Mkuu hakuna MTU anayechukia kujiajiri lkn mtaji ndo changamoto
 
Kazi huwa wanakosa wanaume tu mara nyingi.. kuna sehem nilishawahi kwenda kuomba kazi fulani hv nikaambiwa kazi hamna kesho yake akaenda mdada akaambiwa njoo uanze kazi kesho
Mmmh basi ni bahati ya mtu lkn sio kusema wadada hawakosi Kazi wako kibao tu mtaani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom