Natafuta Dalali/Mwanamasoko kwa ajili ya app/software yangu

Natafuta Dalali/Mwanamasoko kwa ajili ya app/software yangu

Amba Samedi

Senior Member
Joined
Apr 5, 2024
Posts
193
Reaction score
326
Habari wanaJF,
Salam nyingi kutoka Morogoro Tanzania. Nimemaliza siku salama, na natumaini mambo yenu yanaenda

Nina series of softwares nlizotengeneza kwa ajili ya kurahisisha kazi kwq wateja wangu na wateja wao.

Hizi ni pamoja na

1. Mfumo wa supplies. Kuna jamaa mmoja mwenye butcher aliyeniambia kuwa amechoka na kutumia makaratasi. Hivyo akanipa details zote na sasa tuko kwenye testing phase. Mfumo unaenda vizuri.

2. Mfumo wa Shule. Nilifanya mfumo wa school Fees management. Yaani, mfumo unadaka taarifa za Ada na kuwakumbusha wazazi wanaodaiwa. Malipo yanapofanywa, mzazi hutumiwa SMS receipt kumshukuru kwa kulipa.

3. HasibuHQ Mfumo huu ndo wangu mkuu. Hasa natarget saccos ambao Wana wateja wanaoweka his, kuchukua mikopo na kuwa na deadline za mrejesho. Wahasibu hupata kero kukumbuka kila kitu (kuna mmoja ana wanachama Mia 5, shida kweli!ll). Ina app ambayo mwanachama anaweza kuangalia taarifa zake. Aidha, anakumbushwa deadline za matoleo wiki 2, Wiki 1, siku 3 na siku husika ya mrejesho... anapokea alerts zote za malipo na SMS receipts. Mhasibu pia anapata urahisi wa kuandaa ripoti maana data zote zimo


Nchi hii ni kubwa na natamani kuwafikia watu wengi sana na products hizi. Kuna kijana tunafanya nae yupo maeneo ya kahama. Ila nlitamani kufikia maeneo mengine.

Endapo unamfahamu mtu kama huyo, nishtue.
 
Unazingatia Qualifications zozote?, na ni part time au full time. In addition, be specific unataka kijana atakayefanya Nini mkuu? Maana umezungumza zaidi kuhusu bidhaa na namna zinavyofanya kazi.
 
Back
Top Bottom