Nassari kutoka Machinga hadi kuwa Mbunge

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
100_2802.jpg

927901577.jpg

Naye Mbunge Nassari, aliwataka wananchi wa jimbo hilo ambao kwa sasa wako katika harakati za kupigania kurejeshewa ardhi, kuwa na maono (vision) juu ya matumizi yake ili kuepuka kuja kuiuza kwa watu wengine na tatizo la ardhi likabaki palepale.
“Hata wananchi wa Arumeru Mashariki nimewaeleza kuwa, wanaelekeza juhudi kubwa kuhakikisha tunarejeshewa ardhi, lakini kama hatuna maono, tutajikuta ardhi hiyo imeuzwa yote, kwani tunaihitaji kwa ajili ya shule, zahanati, vyuo vya ufundi au maeneo ya watoto wetu kucheza,” alisema Nassari.


Alisema kuwa aliamua kutoa sadaka ya kumshukuru Mungu kwa mambo makuu aliyomtendea kabla ya kuanza ziara kwa wapiga kura wake, ambao wamekuwa wakimuita kwenye vijiji 86 vya jimbo hilo, kwani Mungu alimlinda kipindi chote, hata wakati wa kampeni magari yao matatu yalipata ajali kwa kuanguka, lakini hakuna aliyeumia huku yeye akiibuka na ushindi kwenye uchaguzi.


Mbunge huyo kijana alisema kuwa, alikuwa na maono ya kuongoza toka akiwa mdogo, na kwamba alichofanya ni kupigana kuhakikisha anafikia ndoto hizo, licha ya hali ngumu ya kiuchumi kwenye familia yao,
kiasi cha kumlazimisha akiwa na miaka 9 kuuza machungwa soko kuu la Arusha kila alipokuwa akitoka shule na mifuko ya plastiki kwenye soko la Tengeru na Mbauda.
 
Wengi wetu tumetokea huko, kuvaa lubega na kuchunga ng'ombe au mbuzi, kuuza lambo barabarani, wakati wa likizo shule inapofungwa kufanya vibarua kujipatia pesa kidogo kwa ajili ya kununulia madaftari na kalamu, au kuuza machungwa. Mama zetu kupika pombe na kuuza vilabuni ili kutusomesha.

Leo tupo tulipo, tusisahau kusema ukweli tulikotoka maana kwa njia hiyo tunawapa moyo vijana wenzetu wanaohangaika kutoka pale walipo na tuwape moyo wasikate tamaa kwani yataka tu moyo.

Watu waliotokea mazingira kama hayo wana uwezo wa kupenya kila hali ya maisha hata yawe magumu namna gani kwani wameshazoea taabu.
 
Asante! maneno mazuri sana...... lazima watanzania waelimishwe umuhimu wa kumiliki ardhi na athari za kuuza kwa wageni
 
100_2802.jpg

927901577.jpg

Naye Mbunge Nassari, aliwataka wananchi wa jimbo hilo ambao kwa sasa wako katika harakati za kupigania kurejeshewa ardhi, kuwa na maono (vision) juu ya matumizi yake ili kuepuka kuja kuiuza kwa watu wengine na tatizo la ardhi likabaki palepale.
"Hata wananchi wa Arumeru Mashariki nimewaeleza kuwa, wanaelekeza juhudi kubwa kuhakikisha tunarejeshewa ardhi, lakini kama hatuna maono, tutajikuta ardhi hiyo imeuzwa yote, kwani tunaihitaji kwa ajili ya shule, zahanati, vyuo vya ufundi au maeneo ya watoto wetu kucheza," alisema Nassari.


Alisema kuwa aliamua kutoa sadaka ya kumshukuru Mungu kwa mambo makuu aliyomtendea kabla ya kuanza ziara kwa wapiga kura wake, ambao wamekuwa wakimuita kwenye vijiji 86 vya jimbo hilo, kwani Mungu alimlinda kipindi chote, hata wakati wa kampeni magari yao matatu yalipata ajali kwa kuanguka, lakini hakuna aliyeumia huku yeye akiibuka na ushindi kwenye uchaguzi.


Mbunge huyo kijana alisema kuwa, alikuwa na maono ya kuongoza toka akiwa mdogo, na kwamba alichofanya ni kupigana kuhakikisha anafikia ndoto hizo, licha ya hali ngumu ya kiuchumi kwenye familia yao,
kiasi cha kumlazimisha akiwa na miaka 9 kuuza machungwa soko kuu la Arusha kila alipokuwa akitoka shule na mifuko ya plastiki kwenye soko la Tengeru na Mbauda.
Ukimuona maskini anashabikia Ccm nenda kampime akili!
 
Back
Top Bottom