Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Naye Mbunge Nassari, aliwataka wananchi wa jimbo hilo ambao kwa sasa wako katika harakati za kupigania kurejeshewa ardhi, kuwa na maono (vision) juu ya matumizi yake ili kuepuka kuja kuiuza kwa watu wengine na tatizo la ardhi likabaki palepale. Hata wananchi wa Arumeru Mashariki nimewaeleza kuwa, wanaelekeza juhudi kubwa kuhakikisha tunarejeshewa ardhi, lakini kama hatuna maono, tutajikuta ardhi hiyo imeuzwa yote, kwani tunaihitaji kwa ajili ya shule, zahanati, vyuo vya ufundi au maeneo ya watoto wetu kucheza, alisema Nassari.
Alisema kuwa aliamua kutoa sadaka ya kumshukuru Mungu kwa mambo makuu aliyomtendea kabla ya kuanza ziara kwa wapiga kura wake, ambao wamekuwa wakimuita kwenye vijiji 86 vya jimbo hilo, kwani Mungu alimlinda kipindi chote, hata wakati wa kampeni magari yao matatu yalipata ajali kwa kuanguka, lakini hakuna aliyeumia huku yeye akiibuka na ushindi kwenye uchaguzi.
Mbunge huyo kijana alisema kuwa, alikuwa na maono ya kuongoza toka akiwa mdogo, na kwamba alichofanya ni kupigana kuhakikisha anafikia ndoto hizo, licha ya hali ngumu ya kiuchumi kwenye familia yao, kiasi cha kumlazimisha akiwa na miaka 9 kuuza machungwa soko kuu la Arusha kila alipokuwa akitoka shule na mifuko ya plastiki kwenye soko la Tengeru na Mbauda.