Ni kweli Mwenyezi Mungu kaibariki nchi hii kwa kila kitu ambacho hata ukienda dunia ipi sidhani kama utakikuta (naongea kwa uzoefu wa kusafiri na kukaa nje)
Imagine nchi ina Mbuga za wanyama kubwa (Serengeti, Ngorongoro n.k) Maziwa makubwa (Victoria, Tanganyika, Nyasa n.k) Madini ya kila aina (almasi, dhahabu, Tanzanite n.k)
Wasanii wakubwa kama Diamond Platnumz, Ali kiba, Harmonize n.k
Sasa kinachoniumiza mimi, ni hawa wasanii wetu, na wengi wa watu maarufu wa mitandaoni, yaani wengi wao waliingia kwenye mziki baada ya kuitupa elimu mapema kabisa kwenye maisha yao, sasa inawagharimu, hilo siyo kosa lao
Tatizo linakuja kwamba hata akiandika kitu au kupost kitu bado haweza hata kutofautisha kati ya baadhi ya herufi za kutumia kwenye sentensi, siyo kiswahili wala kiingeleza. Mfano, Sehemu ya kuweka 'r' anaweka 'l' na kinyume chake, na maneno mengine mengi tu, yaani ukisoma wanachoandika unabaki kuumia moyoni maana unawapenda sana na unawaombea mema lakini sasa kwa style hii kama nchi tutafika wapi kimziki na umaarufu wa watu wetu.
Kama tunataka kufika mbali zaidi, Serikali irudishe elimu ya kusoma na kuandika kwa wasanii wetu, hao ni kioo cha jamii yetu pia.
Hatuwezi kuwakilishwa na watu ambao hawawezi hata kuunga sentensi ikakamilika bila makosa.
Imagine nchi ina Mbuga za wanyama kubwa (Serengeti, Ngorongoro n.k) Maziwa makubwa (Victoria, Tanganyika, Nyasa n.k) Madini ya kila aina (almasi, dhahabu, Tanzanite n.k)
Wasanii wakubwa kama Diamond Platnumz, Ali kiba, Harmonize n.k
Sasa kinachoniumiza mimi, ni hawa wasanii wetu, na wengi wa watu maarufu wa mitandaoni, yaani wengi wao waliingia kwenye mziki baada ya kuitupa elimu mapema kabisa kwenye maisha yao, sasa inawagharimu, hilo siyo kosa lao
Tatizo linakuja kwamba hata akiandika kitu au kupost kitu bado haweza hata kutofautisha kati ya baadhi ya herufi za kutumia kwenye sentensi, siyo kiswahili wala kiingeleza. Mfano, Sehemu ya kuweka 'r' anaweka 'l' na kinyume chake, na maneno mengine mengi tu, yaani ukisoma wanachoandika unabaki kuumia moyoni maana unawapenda sana na unawaombea mema lakini sasa kwa style hii kama nchi tutafika wapi kimziki na umaarufu wa watu wetu.
Kama tunataka kufika mbali zaidi, Serikali irudishe elimu ya kusoma na kuandika kwa wasanii wetu, hao ni kioo cha jamii yetu pia.
Hatuwezi kuwakilishwa na watu ambao hawawezi hata kuunga sentensi ikakamilika bila makosa.