Nashindwa nimjibu vipi dada yangu

Nashindwa nimjibu vipi dada yangu

ulimjua kabisa shemejio samaki hapishi chambo halafu unapeleka mashoga zako kwake?anyway mpe pole dadayako na wewe kuwa mkweli mana ukweli utakuweka huru. sipati picha najua shost wangu anamvurugia ndoa dadayangu!!eti nimfichie siri shosti!NEVER! ningehakikisha shosti anaachana na shen

Hivi ndugu yangu ulitegemea mi niishi bila marafiki coz shem ni mchafu? Najua kwa upande flani roho inaniume nasema ningejua but maisha yangu pia ilikua nilazima yaendelee. Halafu sijambwambia dadangu sio kwa sababu namfichia siri shosti yangu but nahofia maumivu atakayopata dadangu coz alikua ameshasikia mengi. Kukaa kwangu kimya hakukua kwa ajili ya yule msichana, bali sikuwa nimejua nisemeje ili dadangu asiumie, sasa kabla sijapata jinsi ndo na yeye akawa ambeambiwa. Afu mie siwezi kuwaachanisha dadangu na mumewe wala huyo binti na shemu wangu coz si kazi yangu, mie ntatoa ushauri tu afu maamuzi ni juu yao.
 
ila kwa jinsi shem wako alivyo kiwembe wewe umepona kweli? au hiyo ni siri yako? maana kwa mwanaume wa aina hiyo sijui!

Unamaanisha kwa kunibaka au? HAPANA.

Na hata kama ni kiwembe kama ni kwa kunitongoza maamuzi ni yangu afu mi si mtu wa aina hiyo(kataa au ukubali ukweli utabakia pale pale). Najiheshimu sana na zaidi na mweshimu dadangu siwezi mfanyia hivo.
 
huyo dada yako hana kazi, tuseme ni kwamba anamtegemea huyo mwanaume kwa kila kitu?

hata kama ni umasikini kumngangania mwanaume wa hivo ya kazi gani, si bora nife na njaa yangu kuliko kula pesa ya mwanaume wa hivo? kibaya zaidi ndoa hajafunga anasubiri nini zaidi ya kifo tu

kuna jirani yetu mmoja alikuwaga hivo hivo mwanaume malaya kupitiliza yani kila mwanamke asikatize mbele yake anaye..huyo mkewe akashauriwa na ndugu zake arudi nyumbani hakusikia akangangania hapo kama ruba na akamleta na ndugu yake wa kike ambaye naye alitongozwa na huyo baba na akatembea nae pia..kilichotokea wote waliambukizwa ukimwi na aliyeanza kufa ni yule mdogo mtu aliyetembea na shemeji yake pale alipoenda kujifungua hakukaa sana..
mume akafatia na baadae mke halali akamalizikia..
mama wa mke alilia sana kwani alipoteza watoto 2 na ndugu walisikitika sana kwani walimsihi sana ndugu yao aachane na huyo mume akakataa eti kavumilia........mfyuuuuuuuuuu ...........mwambie dadako avumilie lkn aandae hela ya sanda na jeneza kabisa mana si muda mrefu tutamuimbia parapanda
 
Mkuu ungeama hapo

Mie bado sijaweza kujitegemea coz ndo kwanza nimemaliza chuo na ndo natafuta ajira ila nina ndugu wengine amabao wapo maeneo haya sasa nashindwa kuondoka coz naona kama itakua kumtenga dadangu ukizingatia nimeanza kukaa nae mda sana na hata nikitaka kuondoka ntaoa sababu gani ili nisimkwezi dadangu.
 
Dogo... kaa chini na dada yako, mweleze hali halisi... mpe support ya kuweza kuepukana na hali hiyo sio wote mnakaa nyumbani mkijikunyata.. wake up women... wewe na dada yako wote... mnakaa kusubiri nini? Kuletewa magonjwa kesho ukatumia neno 'ningejua!!!' Mwambie anyanyuke, ajifute machozi na badala yake atabasamu... atafute maisha kwaajili ya watoto wake wadogo. Mwanaume kitu gani!!!! Wapo kona zote za dunia...
 
Dogo... kaa chini na dada yako, mweleze hali halisi... mpe support ya kuweza kuepukana na hali hiyo sio wote mnakaa nyumbani mkijikunyata.. wake up women... wewe na dada yako wote... mnakaa kusubiri nini? Kuletewa magonjwa kesho ukatumia neno 'ningejua!!!' Mwambie anyanyuke, ajifute machozi na badala yake atabasamu... atafute maisha kwaajili ya watoto wake wadogo. Mwanaume kitu gani!!!! Wapo kona zote za dunia...

Ushauri wa mtindo huo tumeshampa na karibia kila rafikiake pi anamwambia lakini ndo hivo, uamuzi anao yeye mwenywe juu ya maisha yake.
 
Mwambie dada yako acheki afya kwani kuna maradhi kasha achape lapa atateseka bure na kuwaacha watoto wake wakati mambo yanaweza kuepukika
 
sijui nianzie wapi ila kifupi pole sana.ukisikia sikio la kufa halisikii dawa ndo dada yako.kuna watu wapo kwenye ndoa yao hupenda sana kusikiliza ya watu,kuna watu wanadumu kwenye ndoa zao kutokana na sababu zao wanazozijua wao yaweza kuwa negative au positive.kuna watu wapo tayari hata roho zao zitoke kwa sababu ya mpenzi wake.lakini kuna watu hawasikilizi ya watu kabisaaaa hata wanayoyaona hawajali wanatosheka na kile anachokipata ndani.juzi mtaani kwetu bint kamwambia dada yake jinsi shem wake alivyo huko wajua alimjibu nini?ukimtaka na wewe kalale naye nilipomuuliza kwanini amesema hiyo akajibu kwanza wanaume wachache,pili mtu mzima yule anajitambua sitaweza kumfatilia,tatu nikishajua nifanyaje niachane naye au?,nne nakula,navaa sion sababu yakuhoji chochote.yule dada alinipa majibu nikachoka..mpendwa mapenzi hayaingiliwagwi na watu mimi hapa nilikuwa na kijana ambaye niliamua kumpenda kutokana na nilipoumizwa na mvulana wangu wa kwanza tuliotoka wote tangu msingi mpaka chuo mwaka wa pili.kijana huyu mimi ndo nilimpenda ila naweza sema yeye hakunipenda katika miaka2 tulokaa.waloniona walinionea huruma kwa jinsi nilivyopenda walinambia mengi tuuu mpaka kunitaka niachane naye lkn wala sikuwasikia na mengine nilishuhudia mwenyewe nilikuwa nalia tu lkn nmpenda tunaendelea sasa nilichokitaka nimepata now mwezi nov mwaka huu natakiwa niende india kimasomo mpaka sasa nimejikuta nina mimba jamaa kanitaka nitoe mimba kwakuwa wazazi wake hawataki kabila lingine zaidi ya wahaya nikishatoa tuendele na mapenzi huku akiwaomba wazazi wake wamruhusu.ndo hapo napata ufahamu hivyo hakuna cha india wala cha mume sasa.nalea mimba yangu na wazazi wangu nakujikuta kumchukia yule kijana hata kumtamkia kweli sitaki huduma yoyote kutoka kwake mwanangu ntalea mwenyewe.sasa kifupi mpendwa dada yako kapenda na hataki kupoteza ndoa yake ndo maana yupo hapo.sioni sababu ukimwambia ukweli utakuwa umemsaidia la!wakati mwingine waweza hisi unatatua tatizo kumbe watengeneza tatizo kifupi kuwa na msimamo wako kuwa hujui kama shemeji yako ni msaliti hata yeye si anajua je kafanya hatua gani?waache waparangane wakichokana wataachana
 
Asante sana wapendwa mlionipa ushauri, Mungu awajeze muundelee vema na moyo huo
 
i wish dada ako angetoka katika kifungo kilichomfunga na aachane na huyo mwanaume.
 
mshaur dada yako nae achepuke!" .......... akimwaga ugali yeye amwage mboga.kama mbwai mbwai.
 
Some things are better left unsaid...!
 
kuna watu wanayatafuta matatzo wao wenyewe...ndio maana mnalalamika wanawake mnaonewa kumbe mnajitakia wenyewe..mpe pole dada yako.
 
mwallu ulemh'ola ngw'anike.
 
Last edited by a moderator:
Kuna vitu hunasema..dada yako huwa anadundwa na huyo bwana...yuko kwenye abusive relationship
 
Ndugu yangu,
Unatafuta kukosana na dada yako tu,
Na ukimwambia ujue kuwa atasema kwa mumewe kuwa
wewe ndiwe uliyesema;

Mi naona usiseme kitu.
 
Ukimuambia utamumiza zaidi. Kwa sababu yeye anajua wewe ulikua haujui. Omba mungu akusaidie, akupe moyo wa imani. Pole wanawake jamani, kupenda gani huko jamani?
 
Back
Top Bottom