Mkuu, mbona wako wengi tu? Wewe angalia tu hata waheshimiwa wa jukwaa hili, tafuta michango ya watu humu juu ya serikali ya kikwete na waangalie haohao wanasemaje juu ya serikali ya magufuli. Nenda kwenye kumbukumbu za bunge uone mijadala ya wabunge wa ccm zilipoibuliwa hoja juu ya uozo bandari, reli nk. halafu subiria bunge hili lianze... Nakwambia lazima ushindwe kushangaa!
njaa haina baunsa mjomba .Wakati wa dr jk alisifia lakini Dr Magufuli ameonesha kuwa ilikuwa serikali dhaifu na sasa kwa dr Magufuli dr Bana anasifia.
Je nini msimamo wake na nini mtazamo wake thabiti ktk uchambuzi wake? Je ni Itukadi inambana?
mimi simdharau bana kwakuwa najua tatizo lake ila nawadharau wale waandishi wanaoenda kumhoji!