Nashindwa kuifichua siri hii

Nashindwa kuifichua siri hii

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Tuko marafiki watatu wa kiume wa karibu sana tangu shule ya sekondari, Jeshini hadi Chuo Kikuu, tumeoa na tuna watoto, lakini bahati mbaya rafiki yetu mmoja anatembea na mke wa rafiki yetu mmojawapo kwa zaidi ya miaka 5 sasa.

Mimi ninafahamu uovu huo lakini nashindwa kumtonya rafiki yetu mwenye mke kwa kuhofia kitakachotokea. Anayetembea na mke wa mwenzake hajui kama mimi ninajua.

Shemeji anajua kama mimi ninajua kwamba anatembea na rafiki yetu kwa kuniambia yeye mwenyewe, mwenye mke hajui kabisa kama hili linafanyika.
Sijui kama na mke wangu pia kasalimika kwa aina hii.

Nipeni mawazo nifanye nini kwenye hili
 
Achana na Mambo ya watu, Ukisababisha Mauaji au Watu Kuachana ndio Baadae utajua Ulivyochemka. Mbona Yeye Hajakwambia kuwa Mke Wako Pia Wanachapa. Ukweli ni Kwamba hata wewe Mke wako anachapwa na Jamaa anaechapiwa.

Achana na starehe za watu bwana Mdogo.
 
Hapo cha msingi ni kupunguza urafiki wenu na huyo ambaye anatembea na mke wa rafiki yake au ukiona inafaa mwambie ukweli kuwa anachokifanya si kitu kizuri maana atajisikiaje mkewe naye akiwa analiwa na rafiki yake?Ukiona hakuna hatua zinazochukuliwa kaa nae mbali maana siku ikijulikana ujue urafiki wenu wote nyie utavunjika kwa sababu ya mtu mmoja.
 
Jeshini wapi, jkt iliyoanza juzi tu halafu chuo kikuu na sasa mmeoa na huku jamaa akiwa anachepuka na mke wa mwenzake kwa miaka mitano sasa! ina maana mlioa kabla hamjafika o level? au uliposema jeshini ulimaanisha nini?
Mmm nawaachia wengine wakujibu kuhusu hili, hii inaonyesha kuwa wewe umetoka familia ambayo haijasoma kabisa, maana hata babu yangu mimi alipitia jkt kwa mujibu wa sheria tangu enzi ya Nyerere, hata Mzee Kawawa rip pia alipitia jkt sembuse mimi?
 
ni na mashaka na ukweli wa huu uzi, sekondari kisha jeshini,chuo kikuu kisha tumeona afu watoto duh,jkt ya juzi tu haya yote mmeyatimiza vp?
 
urafiki wa kweli gharama......mweleze huyo rafiki/kiatu kishkaji kwamba analofanya sio kabisa asipokusikiliza mnapokutana watatu jiondoe .....lakini kumweleza mtendwa tukio hilo napata ukakasi
 
Mmm nawaachia wengine wakujibu kuhusu hili, hii inaonyesha kuwa wewe umetoka familia ambayo haijasoma kabisa, maana hata babu yangu mimi alipitia jkt kwa mujibu wa sheria tangu enzi ya Nyerere, hata Mzee Kawawa rip pia alipitia jkt sembuse mimi?

Sasa mbona umeishanijibu, halafu ukisoma user nane yangu huitaji kufikiri sana ili ujue kuwa shule sina.
 
huyo shemeji yako alianzaje kukwambia kuwa anagongwa na rafiki yenu??..Na alipokwambia ulimwambiaje??..siku zote umeficha huu uovu kwa rafiki yako kinachokufanya leo utake kusema ni nn?
 
Dunia inaangamia sio kwa sababu ya watu waovu la hasha!!Ila ni kwa sababu ya watu wema ila wamekuwa kimya huku wakifahamu uovu unaoendelea!!..JITAFAKARI!!
 
Situation kama hiyo nlishawahi kukumbana nayo wakat flani ila nilichokifanya,nikumuonya vikali sana yule mwanamke na huyu jamaa....

lakini nikaenda mbali zaidi kumshauri huyu jamaa aanzishe mahusiano na mdogo wake na yule mwanamke ili yule mwanamke amchukie jamaa(maana ndo hulka ya mwanamke,ukitaka akuchukie milele,tembea na ndugu au rafiki yake),na lengo likatimia..baada ya jamaa kuanza kutembea nae na yule mwanamke kujua,alimchukia sana jamaa hadi kesho,kwa hiyo kwa namna yoyote ile hawawez kurudiana...

hivyo ndo jinsi nlivyoweza solve hilo tatizo na bado ndoa yao inaendelea fresh
 
Ndio maana sipendi urafiki mbele ya mke wangu. Urafiki wetu ni huko, mambo ya kumzoea mke ni kumkaribisha shetain tu.
Kaa kimya, huyo kwenye mke atajua tu, unless awe zoba. Japo naona mwisho m'baya wa urafiki wenu.
 
Back
Top Bottom