Nashauri Serikali itengeneze madawati ya Zege

Nashauri Serikali itengeneze madawati ya Zege

Chrizant Kibogoyo

Senior Member
Joined
Aug 12, 2016
Posts
159
Reaction score
81
Nianze kwa kumpongeza JPM kwa kuvalia njuga tatizo la ukosefu wa madawati. Leo nimetembelea moja ya shule wilaya Kibaha na kukuta madawati ya zege yaliyojengwa mwaka 1981,miaka 35 iliyopita.

Hadi Leo ni mazima na kwa kweli yanaonekana imara kuliko hata chumba cha darasa husika. Ktk picha utaona baadhi ya madawati ya mbao yakiwa yameandikwa ukarabati,kwa maana ya kuhitaji kufanyiwa ukarabati licha ya kutengenezwa miaka michache iliyopita.

Ni vyema wateule wa JPM wakaiga huu ubunifu ili kumaliza kabisa tatizo la madawati hapa nchini
IMG_20160917_105115.jpg
IMG_20160917_105158.jpg
 
Nianze kwa kumpongeza JPM kwa kuvalia njuga tatizo la ukosefu wa madawati. Leo nimetembelea moja ya shule wilaya Kibaha na kukuta madawati ya zege yaliyojengwa mwaka 1981,miaka 35 iliyopita. Hadi Leo ni maxima na kwa kweli yanaonekana imara kuliko hata chumba cha darasa husika. Ktk picha utaona baadhi ya madawati ya mbao yakiwa yameandikwa ukarabati,kwa maana ya kuhitaji kufanyiwa ukarabati licha ya kutengenezwa miaka michache iliyopita. Ni vyema wateule wa JPM wakaiga huu ubunifu ili kumaliza kabisa tatizo la madawati hapa nchini
Hayo siyo madawati ni vimbweta...
 
dah, nilisomeaga haya madawati 1998! mpaka leo bado yako fresh?! Tungefanya mpango madawati yoote TZ yawe ya cement, ikiwezekana yawe yanahamishika na darasa liwe na sehemu ya kutengwa (vikalio )vya madawati! Tukifanya hivo hii shida haitarudia teena TZ at the same tutkuwa tumeepuka kuharibu misitu
 
Ushaur mzur tatizo serkal yetu hainaga hata vision wala malengo ya muda mrefu. Yani malengu huwa ni miaka 5 bac ndyo maana ukiangalia kila vipaumbele kwenye awamu hii ni vya hadi 2020. Cjasikia kipaumbele cha zaidi ya miaka 20 ijayo.

Serkal yenyeuwezo wa kujenga dawati za zege ni serkal yenyewe malengo ya muda mrefu. Kwa hii ya Tz tutasubir sana.

Mfano mzur angalia kwenye barabara. Kila siku mara wanazirepair mara wanazipanua. Hii yote ni kwa sababu barabara zilijengwa kwa malengo ya muda mfupi 2 kwa sababu za kisiasa.
 
mimi napendekeza tutengeneze ya chuma.
 
Zege linamadhara yake ukikalia muda mrefu.
 
Nianze kwa kumpongeza JPM kwa kuvalia njuga tatizo la ukosefu wa madawati. Leo nimetembelea moja ya shule wilaya Kibaha na kukuta madawati ya zege yaliyojengwa mwaka 1981,miaka 35 iliyopita.

Hadi Leo ni mazima na kwa kweli yanaonekana imara kuliko hata chumba cha darasa husika. Ktk picha utaona baadhi ya madawati ya mbao yakiwa yameandikwa ukarabati,kwa maana ya kuhitaji kufanyiwa ukarabati licha ya kutengenezwa miaka michache iliyopita.

Ni vyema wateule wa JPM wakaiga huu ubunifu ili kumaliza kabisa tatizo la madawati hapa nchini
View attachment 402228 View attachment 402229
hongera sana kwa idea yako nzuri
 
.....
.....sugu na viraka kuongezeka ....walioserereka majabalini juwa hii mambo
 
Back
Top Bottom