Taarifa ya sasa hivi ni kuwa Abate Mkuu mstaafu wa Kambi moja ya mabruda huko mkoani Ruvuma amefariki usiku wa kuamkia leo kwa tatizo linalohisiwa kuwa ni corona. Vipimo vimechukuliwa kupelekwa Dar kwaajili ya uthibitisho.
Marehemu alitokea Italy, akaenda South Korea. Aliingia nchini siku 1 au 2 kabla ya karantini. Akaenda Mbeya, kisha kambi ya mabruda. Akaanza kuumwa, akatibiwa hospitali ya Peramiho kabla ya kurudi tena kambini. Jana usiku akazidiwa, akapoteza fahamu na kufariki.
Kwa sasa, kwa taarifa kutoka kwa Paroko mmoja wa parokia jirani, kambi yote ipo karantini kusubiria majibu ya vipimo.
Izingatiwe kuwa mpaka sasa ni hisia maana hakuna majibu ya vipimo yaliyopatikana kuthibitisha au kukanusha hisoa zilizopo.
Tuendelee kuchukua tahadhari za kujikinga.