Nashauri maandamano yafanyike tarehe 09.12.2011

Nashauri maandamano yafanyike tarehe 09.12.2011

mkweli1961

Senior Member
Joined
Nov 9, 2010
Posts
148
Reaction score
44
Kwasababu maandamano yetu yamekuwa yakizuiwa na polisi kila tunapokuwa tumewataarifu, nafikiri siku nzuri ya kufanya maandamano hayo iwe tarehe 09.12.2011 kwani siku hiyo kumbukumbu ya Jamhuri. Polisi watakuwa wanaelekea uwanja wa taifa na hawatakuwa na ubavu wa kutuzuia kufanya maandamano yetu. Vijana Mbeya waliwazidi nguvu polisi sembuse hapa Dar. Tusipoteze nafasi hii sisi wenye uchungu na nchi hii. Tuungane kuikomboa nchi yetu.

Wakati wa kusubiri kuruhusiwa maandamano kwa kibali umepitwa na wakati. Polisi wanatakiwa wavuliwe gamba. Saa ya ukombozi ndio sasa.
 
naunga mkono hoja!!! Kaulimbiu ni kupinga matumizi ya mabilioni ya wananchi kuandaa sherehe za uhuru wa tanganyika ambao hauna tija kwa watanganyika wenyewe!!!

naomba kuwasilisha ...
 
uchungu na nchi sio lazima kuandamana hiyo inaweza kuwa sera ya chama chako sio ya watanzania wote. mwisho katika kuandamana mtabomoa na maduka yetu kwa kisingizio cha maandmano. Tunawajua hamna kawaida ya kuandamana bila kubuguzi wengine kama ni hao polisi piganane nao huko huko.
 
Mimi ni mmoja wa waathirika wa maandamano kosa langu ni kupita karibu na waandamanaji wakachukua mawe na kuvunja vyoo vya gari yangu. kama hayajakupata utaona kwamba maandamano ni mazuri kwa kila mtu kumbe sio hivyo.
 
Maandamano ni haki ya kikatiba lakini yanavyotumiwa vibaya sina sababu ya kuunga mkono hoja.
 
Kipepeo inakuuma nini wakati gari lenyewe ni la kifisadi,wewe kaa kwako sisi tutaandamana tu maana tunajua tunalofanya
 
Ww unayeamasisha maandamano siku ya kuandamana wala ujitokezi umbea tu andamana uone wanaume ffu watakavyokupiga mande
 
naunga mkono hoja.........natamani iwe kweli
 
Ww unayeamasisha maandamano siku ya kuandamana wala ujitokezi umbea tu andamana uone wanaume ffu watakavyokupiga mande

ausifiaye uovu, jua yeye ni uzao wa huyo mwovu, kapime dna kama inalandana na ya babako, kuna uovu unakuandama nawe hujui! nini uanaume wa ffu, labda mama yako anajua, koma kumtukana mama yako.
 
Back
Top Bottom