Nas ajifananisha yeye, Biggie na Jay Z ni sawa na J Cole, Drake na Kendrick Lamar, kwenye album yake ya Magic. Awakumbuka na Wu Tang Clan

anonymousafrica

JF-Expert Member
Aug 24, 2016
611
639
Nas-magic-cover.jpg

Kwa wasiofuatilia wanaweza kudhani Msuguano baina ya Nas na Jay Z unaendelea lakini nikuambie tu ya kuwa mtafaruk wao ulishakwisha zamani sana. Awali familia zao zilihusishwa kwenye michano na mwisho wakaamua kukaa chini na kuyajenga. Wakashirikishana kwenye nyimbo baadhi na hivi majuzi tumewaona kwenye album ya D J Khalid kibao cha Sorry not Sorry.

Siku kadhaa zilizopita, Nas ameachi album (LP ALBUM-MAGIC) yenye jumla ya Nyimbo 9. Kama wewe ni shabiki na mpenzi wa nyimbo za Hip Hop tena kwa wasanii wenye mafanikio ambao bado wanaiwakilisha mitaa vizuri kabisa, sidhani kama unaweza kuruhusu album ya Nas au wimbo wowote mpya kutoka kwa Mr I can ukupite. Hii ni kwasababu ya namna anavyotunga mashairi na jumbe zenye kuvutia na kufunza katika nyimbo zake.

Wimbo nambari 6 katika album hiyo unaitwa WU FOR THE CHILDREN, Naomba kwa leo nisihusianishe sana wimbo huu na harakati za kundi la Wu Tang Clan na msaada kwa watoto kuanzia mashairi na harakati zao binafsi hadi tukio la mwaka 1998 kwenye tuzo za Grammy (RIP Ol Dirty Bastard) hili nitalizungumzia siku nyingine au huko mbele naweza kutia nakshi nakshi kidogo.


Ndani ya Wu For the Children, Nas amezungumzia wasanii wachanga ambao wanaomba msaada kwa wasanii ambao wameshatoboa,
Pia amezungumza juu ya mashabiki zake wanaotaka muziki tofauti kutoka kwake
lakini pia amegusia kuhusu utofauti wa muziki wa sasa na wa zamani.
Na hapa ndipo aliposema
i shoulda had Grammys when Ol Dirty said WU For the Children.
Akimaanisha.
Nilipaswa kuwa na Grammy wakati Ol Dirty aliposema WU ni kwa watoto (Wu Tang Clan) nilisema nitatia nakshi kidogo. Marehemu Oldirty Bastard kutoka Kundi la Wu Tang Clan aliwahi kushangaza mashabiki katika tuzo za Grammy. Naomba nimnukuu kwa uchache, Alipanda jukwaani na kusema “leo nimeingia dukani na kununua nguo za gharama mno, nilidhani tutabeba ushindi..naomba mutambue Didy ni msanii bora lakini Wu Tang ni bora zaidi.Kumbukeni Wutang tunafanya kwaajili ya watoto, rap yetu inafundisha na kuonya…” WU TANG IS FOR THE CHILDREN. Yani ni kama Chid Benz alivyoshushwa na Kalapina jukwaani baada ya kuombwa Mike na Nikki Mbish kwa muda mrefu.
ol-dirty-bastard.jpg

Lakini Oldirty aliongea maneno mazito kidogo. Tuachane na hili
Twende kwa Nas
Shoulda did that remix verse on gimme the loot for Biggie
Nas anaonyesha masikitiko kwa kusema, ni kheri angefanya remix ya Gimme the Loot (Wimbo wa Biggie) kwenye album yake ya Ready to die. Kumbuka Nas aliambiwa na Biggie afanye naye Remix lakini ilishindikana. Awali alitakiwa kufanya jambo kwenye album ya Ready to die lakini album ikatoka mapema kabla Nas hajafanya track hata moja
Anashusha mstari mwingine anasema ..
Me, Jay and Frank White is Like Cole, Drizzy and Kenny.
MIMI, JAY (JAY Z) na FRANK WHITE (BIGGIE
😆
bwana Notorious aliwahi kujipa AKA ya Frank White, character ya Christopher Walken katika movie ya King of Newyork)
Sasa anajifananisha yeye, Jay z na Biggie ni kama COLE (J COLE) DRIZZY (DRAKE) na KENNY (KENDRICK LAMAR).
Je, Nas amepatia ulinganisho wa kizazi chake na huu wa wasanii wa sasa?.
Lakini hapa tunaona ni namna gani Nas anamkubali Jay Z licha ya misuguano waliyokuwa nayo hapo awali.
Lakini pia namna anavyoheshimu uwezo wa Biggie Notorious.
Lakini Kubwa kuliko, ni kuwapa heshima kubwa Mno Jcole, Drake na Kendrick Lamar.
maxresdefault (2).jpg
jay-z-nas-biggie-documentary.jpg

Nadhani Nas amewabebesha mzigo mzito sana hawa vijana, kwasababu ya ubora wake yeye na wasanii aliowaunganisha yani JayZ na Biggie na kofia anayowavisha vijana hawa.
Nina imani kuna watu watafurahia mno kauli hii na kuna watu watakasirishwa kwa kutotajwa wasanii wanaowakubali, kwasababu ni ngumu mno kusema Jcole, Drake na Kendrick Lamar hawana uwezo mkubwa. Bali itawauma kwa wasanii wanaowakubali kutoa kutajwa.
Je tunahitaji List ya wasanii wanaopendwa na Nas kama Funga Mwaka????
😂
 
NAS Vs CORMEGA mkuu hv hawa jamaa wakishapatana maana walikuwa marafiki sana badae wakaja kuwa maadui wakubwa sana tatizo ilikuwa ni nini,?
 
nas is not only my favourite rapper of all time but also my distant brother.

uwezo wake wa kuandika ni mkubwa sana. hipohop kaibeba mabegani mwake.

kwa yeye kujifananisha na wasanii amateurs kama akina drake, ni kuonyesha how humble and down to earth he is.
 
Mwaka 2022 kijana kutoka Tanzania bado anazungumzia habari za Nas and Jay Z?

Bro I am regretting to tell u that ur mind has stuck in the 90s.

U think 2022 is 1994/96?

If u were listening to Nas,Jay,Wutang & co back then ur supposed to be a father now cause u can be 35 to 42 or something
At this age u still don't have a clue that the so called hihop is a very evil cult and it is for the ghettos of the US.

I was like you back then until when I went to the US and happen to be in the hell on earth which u people are calling hood.
Man am telling you there is nothing good in the hood and nothing good can come out of the hood.

Stop supporting those bastard. Get down with ur own African culture.

I am so much discounted.

Let me act foolishly here: Fzk Nas Fzk Jay Z fxk Wutang clan Fzk hiphop as a culture as a music genre and a mother far keen community. And if u wanna be down with hip hop then.....
 
Mwaka 2022 kijana kutoka Tanzania bado anazungumzia habari za Nas and Jay Z?

Bro I am regretting to tell u that ur mind has stuck in the 90s.

U think 2022 is 1994/96?

If u were listening to Nas,Jay,Wutang & co back then ur supposed to be a father now cause u can be 35 to 42 or something
At this age u still don't have a clue that the so called hihop is a very evil cult and it is for the ghettos of the US.

I was like you back then until when I went to the US and happen to be in the hell on earth which u people are calling hood.
Man am telling you there is nothing good in the hood and nothing good can come out of the hood.

Stop supporting those bastard. Get down with ur own African culture.

I am so much discounted.

Let me act foolishly here: Fzk Nas Fzk Jay Z fxk Wutang clan Fzk hiphop as a culture as a music genre and a mother far keen community. And if u wanna be down with hip hop then.....

bro you sound frustrated and depressed. go see a psychologist asap.

your opinion about hip-hop music is too general, would you mind telling us the negative side of it please?
 
Let me act foolishly here: Fzk Nas Fzk Jay Z fxk Wutang clan Fzk hiphop as a culture as a music genre and a mother far keen community. And if u wanna be down with hip hop then.....
Well, this is how we gonna do this:
Fack Mobb Deep, fack Biggie, fack Bad Boy as a staff, record label and as a motherfacking crew!
And if you want to be down with Bad Boy, then fack you too!

Chino XL: faaack you too!
All you motherfackers, faaack you too!
(Take money, take money)
All of y'all motherfackers, fack you; die slow, motherfacker
My .44 make sure all y'all kids don't grow!
You motherfackers can't be us or see us
We motherfackin' Thug Life-riders, Westside til we die!
Out here in California, nigga, we warned ya
We'll bomb on you motherfacker! We do our job!
You think you mob? Nigga, we the motherfackin' mob
Ain't nothing but killers and the real niggas
All you motherfackers feel us
Our shit goes triple and 4-quadruple
Take money
You niggas laugh cause our staff got guns under they motherfackin' belts
You know how it is, when we drop records they felt
You niggas can't feel it, we the realest
Fack 'em, we Bad Boy-killers
We killers, we killers, we killers
 
Back
Top Bottom