kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Kwanza, Alloyce Nyanda kwa nafasi yake katika jamii apaswi kuwa mtu wakuhubir au hata kujaribu kuutukuza ukabila. Yeye Sasa ameshakuwa zao la jamii.
Pili, kauli ya Mdude nyangali kwamba Atatumia Wembe uleule aliotumia kumnyoa mtanguliz wa Rais aliyepo kumnyoa aliyepo ni kauli thabiti na ambayo Mdude anaiishi kwa matendo. Alimkosoa mtangulizi wa Rais aliyepo na bado anaendelea kumkosoa Rais aliyepo kitu ambacho ni Cha kikatiba na kisheria. Wembe ni ule ule Ni kauli ya wote, inapotumika na viongozi dhidi yetu isionekeane Kama ni sahihi lakini wananchi wakiitumia wakahukumiwa. Tukubali kwamba sheria haijakataza kiongozi kunyolewa kwa wembe ule ule hasa katika medani za kisiasa.
Tatu, Nyanda anauvaa uzazi kwenye jukwaa la siasa kitu ambacho hakipo. Kwenye jukwaa la siasa kwenye taaluma hakuna mkubwa na mdogo wote mnashawishi kwa lugha na hoja. Kuendelea kutoa maneno kwa kujifanya wewe ni mkubwa au mdogo ukaacha kusimamia hoja nikukosa hoja. Lazima tukubali kuadhibiwa kwa kadri tunavyocheza na jukwaa. Rejeeni kauli za mama kwenye kampeni alizungumziaje hoja ya risasi, wapi tumewahi kumkosoa? Usawa uzaliwa kwa nidhamu kutoka juu kwenda chini na kutoka chini kwenda juu.
Nne, Nyanda kabla yakuandika maoni yake alipaswa kumhoji mtoa hoja. Yeye anapaswa kuwa neutral person, muda wa kusimama Instagram kwa maoni binafsi nakutoa hukumu umeisha pale alipojipambanua kama mwana habari. Alitaka kuwa na upande aondoke kwenye uandishi na akitaka atoe maoni yake basi akubali kuhojiwa ili atakapokuwa anajibu hoja kwenye mahojiano aweze kujibu anayopenda na asiyopenda kusikia.
Mdude Nyangali chapa kazi ila usilewe sifa.
Pili, kauli ya Mdude nyangali kwamba Atatumia Wembe uleule aliotumia kumnyoa mtanguliz wa Rais aliyepo kumnyoa aliyepo ni kauli thabiti na ambayo Mdude anaiishi kwa matendo. Alimkosoa mtangulizi wa Rais aliyepo na bado anaendelea kumkosoa Rais aliyepo kitu ambacho ni Cha kikatiba na kisheria. Wembe ni ule ule Ni kauli ya wote, inapotumika na viongozi dhidi yetu isionekeane Kama ni sahihi lakini wananchi wakiitumia wakahukumiwa. Tukubali kwamba sheria haijakataza kiongozi kunyolewa kwa wembe ule ule hasa katika medani za kisiasa.
Tatu, Nyanda anauvaa uzazi kwenye jukwaa la siasa kitu ambacho hakipo. Kwenye jukwaa la siasa kwenye taaluma hakuna mkubwa na mdogo wote mnashawishi kwa lugha na hoja. Kuendelea kutoa maneno kwa kujifanya wewe ni mkubwa au mdogo ukaacha kusimamia hoja nikukosa hoja. Lazima tukubali kuadhibiwa kwa kadri tunavyocheza na jukwaa. Rejeeni kauli za mama kwenye kampeni alizungumziaje hoja ya risasi, wapi tumewahi kumkosoa? Usawa uzaliwa kwa nidhamu kutoka juu kwenda chini na kutoka chini kwenda juu.
Nne, Nyanda kabla yakuandika maoni yake alipaswa kumhoji mtoa hoja. Yeye anapaswa kuwa neutral person, muda wa kusimama Instagram kwa maoni binafsi nakutoa hukumu umeisha pale alipojipambanua kama mwana habari. Alitaka kuwa na upande aondoke kwenye uandishi na akitaka atoe maoni yake basi akubali kuhojiwa ili atakapokuwa anajibu hoja kwenye mahojiano aweze kujibu anayopenda na asiyopenda kusikia.
Mdude Nyangali chapa kazi ila usilewe sifa.