Napinga sehemu ya malipo ya Lema...

Je Lema alijisimamisha ubunge au alisimamishwa? Kwa kuwa alisimamishwa na hakujisimamisha akipatikana hana hatia analipwa stahiki zake zote!
Ni kama mshitakiwa alieshutumiwa kesi,akapambana kwa muda mrefu baadae akaja kushinda....kisha akadai fidia za malipo aliyokuwa anaingiza kwa siku...nadhani hapa utaibuka na kusema kila siku ulikuwa unashinda mahakamani ulipwe hela ya nini? Ndio unanyotaka kusema hapa...
Kwa utaratibu huo basi serikali inaweza kuwa inawafungulia kesi na kuwapotezea muda wabunge wa upinzani ili wasiwalipe!
Sidhani kama ulijipa muda wa kutosha kabla ya kupost hili.....makosa ya kisheria yanagharama na gharama ndio hizi...kuna raha ukishinda 2!
 

Ndugu Farida,
Sidhani kama Lema ameshalipwa hizo pesa tayari, wala sidhani kama hata imeshaamuliwa atalipwaje. Pia haiko wazi kama atakubali au kukataa kulipwa au kama akikubali atafanyia nini hizo pesa.

Ushauri wangu:
Tuache kumsemea. tusubiri aseme kwanza ndiyo tuhukumu. Tuangalie kama atachukua hayo malipo atayapeleka wapi. I am confident atayatumia VIZURI kuliko mtakavyotegemea.
 
Kwa hiyo Lema kapata Excuse kuchukuwa hizo pesa ambazo ajazifanyia kazi.

Mkuu unamaanisha nini kusema lema kapata excuse? Ina maana hana haki kurudishiwa stahiki zake?je aliacha mwenyewe majukumu yake au aliachishwa?je time value for money imekuwa considered?kisheria lema ana stahiki kupata hats icho kilichotajwa. Sheria mbovu za taifa letu na serikali yetu ndo zinazofuatwa wala si excuse ndugu.
 
Kwa hiyo Lema kapata Excuse kuchukuwa hizo pesa ambazo ajazifanyia kazi.

Kumhenyesha na kesi mlikomhenyesha mimi naona mlijua kuwa mtaishia kumlipa, msiwasahau mliowatumia kufungua kesi nao muwalipe baada ya kulipa gharama za kesi
 

Binafsi naguswa na huu moyo wa kuumizwa na matumizi yasiyo stahiki ya kodi za wananchi. Hata hivyo ni vema ikakumbukwa kuwa tunachoongelea hapa ni

1.Lema alikuwa mbunge halali kwa KUCHAGULIWA na KWA RIDHAA YA WANANCHI WA JIMBO LAKE. Kwa hiyo kitendo kilichofanywa cha kuitoa mahakama nje ya utaratibu na kulazimisha hukumu, kilimnyang'anya haki yake ya kisheria ya kuwawakilisha wananchi kupitia KODI hizo na mengineyo.

2.Matakwa ya sheria yanakubaliana na uhalali wa ubunge wa Lema ndiyo maana baada ya kureview hukumu wameona bado ana haki hiyo.

Kwa hiyo:
Kwa kuwa Lema alichaguliwa kwa kura halali kuwa Mbunge, na kwa kuwa uamuzi wa kumsimamisha haukuwa wa haki, na kwa kuwa hukumu ya rufaa imemrudisha tena Kuwa mbunge, Hii ni sawa na kusema: kwa mujibu wa sheria Lema alikuwa MBUNGE HALALI TANGU KUCHAGULIWA MPAKA SASA NA MPAKA WANANCHI WATAKAPOAMUA VINGINEVYO.
Kutokana na hilo Lema anastahili kila posho aliyotakiwa kupata akiwa mbunge HALALI kwa sababu hakuomba kusimamaishwa wala hakuwa na Matatizo ya kiutendaji. Kama kuna lawama za matumizi mabaya ya Kodi yanaweza kuelekezwa kunakostahili uchunguzi ufanywe, ipatikane SABABU ya kusimamishwa Lema at first place. Huyo aliyepika hilo ndo ALAUMIWE KWA UFUJAJI WA KODI ZA WANANCHI. Vinginevyo Lema, Kwa mujibu wa taratibu anatakiwa ALIPWE STAHILI YAKE KWANZA halafu, kama itaonekana sheria zinahalalisha ufujaji wa KODI kwa maana hiyo ZIFANYIWE MAREKEBISHO ili kesho lisirudie hilo.

Kwa upande wa pili ikumbukwe kuwa Lema kama Binadamu, Mtanzania, Mwanamageuzi na Mzalendo, ana maoni na utashi wake. Hivyo badala ya kuanzisha mijadala kama hii tumpe nafasi ya kuamua anataka nini. Naamini atakuja na uamuzi wa busara kama ambavyo amekuwa anafanya. Nina imani kuwa Matumizi ya pesa hizo (KAMA ATALIPWA) yatakuwa kwa manufaa ya wanachi bado na HAITAKUWA HASARA KWA VYOVYOTE KUCHUKUA FEDHA KWENYE MFUKO WAKO WA KUSHOTO KWENDA WA KULIA........Hivi Ndivyo nionavyo mimi:smiling:
 
Kumfungulia/kumbambikia kesi Lema kwako wewe ni sawa, kumlipa haki za kumbambikia kesi ni noma; hamuelewiki. Si serikali yenu choteni po pote mumlipe. Muwashauri CCM waache michezo kama hii bila kujipanga na gharama zitokanazo.
 
hoja yako ina mashiko ingawa ni tatizo la mfumo
na inawezeka baadhi ya vitu vikafanyika mfano mafuta kwa sababu alishindwa kutembelea maeneo yake kama mbunge hivyo inabidi atembee huko kwa nguvu zote yaani asubuhi mchana na jioni ni zaidi ya yale mafuta ya kawaida ambayo angetumia kwa mwezi
posho ya jimbo ile mara nyingi hutumika kwa shughuli za jimbo kwa sababu lema alisimashwa na shughuli hizo zilisimama hivyo itabidi alipwe ili shughuli ziendelee
 
Mawaziri wakuu wote vwastaafu wanalipwa 70% ya mshahara wa aziri mkuu aliyeko madarakani,hebu tuwahesabu mmoja mmoja.
1.Edward lowassa
2.Fredrick Sumaye
3.Joseph warioba
4 .Salim Ahmed
5.Cleopa Msuya
6.Sam Malechela.
Hawa wana tija gani kwa nchii hii?Kwani hawakulipwa mafao yao baada ya kuitumia nchi hii?Lyatonga nae nilimsikia bungeni akilalama nae alipwe,serikali imemtupa.Sioni shida Lema akilipwa,acha na yeye ale kidogo mbona wengine wanakula bila hata kunawa mikono?
 
Mawaziri wakuu wote wastaafu wanalipwa 70% ya mshahara wa waziri mkuu aliyeko madarakani,hebu tuwahesabu mmoja mmoja,kisha piga hesabu ni pesa ngapi inapotea kila mwezi.
1.Edward lowassa
2.Fredrick Sumaye
3.Joseph warioba
4 .Salim Ahmed
5.Cleopa Msuya
6.Sam Malechela.
Hawa wana tija gani kwa nchii hii?Kwani hawakulipwa mafao yao baada ya kuitumia nchi hii?Lyatonga nae nilimsikia bungeni akilalama nae alipwe,serikali imemtupa.Sioni shida Lema akilipwa,acha na yeye ale kidogo mbona wengine wanakula bila hata kunawa mikono?
 

Mkuu,unachosema kuhusu posho ni sahihi kabisa,but ni hao hao wabunge wa chadema ndiyo walizipigia kelele wakaonekana mataahira,na sisi wananchi badala ya kuwasaidia nasi tukawaona walewale Chadema waropokaji,sasa nini?waache wazile kutokana na umbumbumbu wetu,na siyo hizo,wengine wanalipwa malipo ya uwaziri na ubunge,hulioni hilo?yako mengi na waache wale tuu!kuleni waheshimiwa sisi waTanzania ni MAZOMBI.
 
yaani post km hii haistahili comment hata moja maana it's extremely upuuzi, nategemea tujadili ideas ambazo zitatusaidia kudhibiti incompetent judges in this country to make absurd decisions km ktk kesi ya lema
 

Akina wasira wanao lala na kukoloma bungeni mbona wanalipwa
 
Nenda mahakamani.. Ndo mahali pekee haki inapatikana! Ukianza na Dowans kulipwa!
 

Kina nani wanapenda kutunga hizo kanuni? sitegemei kupata response za kiCCM ya kwamba kila anayepinga kitu ni mpinzani, hivi hii nchi haina RAIA wenye uchungu nayo, tusipeane vyama

Kulipwa ni haki yake,tena ilipaswa na wale vizabizabina waswekwe lupango iwe fundisho.
Hii ni kanuni mpya au ni kutojua kwangu,
anyway hiyo sio sehemu ya hoja yangu, siasa pembeni ndani ya hii hoja



Naomba kwa kukazi kwa kusema POSHO za MAFUTA na JIMBO zilizilipwa, apewe mshahara tu

njaa na ujinga ni kitu kimoja
You right, Taifa limeja njaa kwa mifumo kama hii, sasa lazima tu protest kwa matumizi ya kodi zetu


View attachment 76779wao wanamchafua mitandaoni yeye ZZK yuko busy kujijenga kwa wapiga kura....BABU PADRI SLAA kaazi kweli kweli

No politics please, hii ni issue nyeti kwa ustawi wa jamii
 
Akina wasira wanao lala na kukoloma bungeni mbona wanalipwa

Kwa hiyo ume support hoja, ya kwamba Lema ni sawa na hao kina wasira walilala na kulipwa, kwa haki wote wasilipwe
HONEST IS A BEST POLICY IN MY HEAD
 
Nenda mahakamani.. Ndo mahali pekee haki inapatikana! Ukianza na Dowans kulipwa!
Hivi TANESCO hawana kesi ya zidi ya DOWANS mahakamani?
na kama haya malipo ni sawa na ya DOWANS as the referring it, let me start with this one
 
yaani post km hii haistahili comment hata moja maana it's extremely upuuzi, nategemea tujadili ideas ambazo zitatusaidia kudhibiti incompetent judges in this country to make absurd decisions km ktk kesi ya lema

Yet you did comment, ....... walk your talk mate
 

As a patriotic RED is the only line i do care, kushinda au kusimamishwa ubunge lema kuna matokeo, moja ya matokeo yake ni permanent mfano kupoteza miezi minane ya kulitumikia jimbo lake, atuwezi kusema uchaguzi wa Arusha ufanyika May 2016 kwa sababu mbunge alipoteza miezi nane, hiyo ni un-reversibly condition, pia kwenye record itajulika hivyo kwamba Lema aliwahi kusimamishwa,
Lema analipwa kulingana na sheria za kazi kama watu wengine na si kutokana na kazi yake bali kutokana na haki zake kama wananchi wengine, ya kwamba shughuli ya ubunge ni sehemu ya kipato chake na kilisimamishwa, hivyo basi mshahara wake ni haki kwa sababu ni matumizi yake.
Sasa naomba nijibu swali hili kwa makini JE POSHO za Mafuta wabunge wanapewa kwa shughuli gani? na Posho za Jimbo Je? je lema aliendesha gari kufanya hizo shughuli miezi nane iliyopita?
 
Wanasiasa bana linapokuja swala la mahela wote ni wale wale tu
Hapa Lema na washirika wake watatetea ni sheria zilizopo zina mpa haki na anakubaliana nazo sababu ni mahela.............lakini labda ikija swala la kulipwa Richmond japo lipo kisheria katu hata kuelewa sbabu tu halimuhusu yeye.
 

Mbaya zaidi watu wanaleta vyama, eti nimetumwa hivi hii post kuna ccm anayeishabikia? ninawezaje kutumwa na ccm ambao wameweka hizi sheria mbovu? yaani sawa na ccm kujishitaki wenyewe!!!!!!
Hii bora ina mazala makubwa kwa ccm kuliko chadema maana lema anawezakufanya action ya kizalendo na kuiumbua serikali na chama.

Tatizo la nchi yetu ni vyama, tumegawanyika sana kwa vyama kiasi kwamba kila mwenye hoja lazima apewe chama cha siasa, kuna watu wanataka tuamini kwamba hakuna tena maoni huru nchini kutokana na wao kubeba vyama mgongoni mwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…