Napinga hoja zilizotolewa na Mbunge wa Kahama kuruhusu Wanafunzi kuvaa viatu vya aina yoyote na mambo mengine aliyoshauri Serikali

Mkuu nakupa kongole nyingi kwa hoja ulizojenga juu ya ubora unaopaswa kuwepo ktk masuala ya elimu. Kuna kasumba mbaya imejitokeza hivi karibuni kwa viongozi kutoa ushauri wenye fikra za kimaskini na ufukara.

Kumejitokeza kasumba ya kuwataka watu kutokuwajibika ama kukumbatia vitu duni kama sababu ya kujionyesha kuwaonea huruma. Kibaya zaidi ni kutaka kuhadaa tabaka linalotawaliwa ili kuhalalisha "mentality" za kimaskini kuwa ndiyo uzalendo wenyewe.

Kuzaa ni wajibu mpana unaohusisha chakula, malazi, mavazi, elimu, bima na vitu vingime muhimu kwa ajili ya makuzi ya watoto na kujenga familia bora. Kisingizio cha kulalamikia gharama kwa wazazi hukuondoi wajibu huu.
 
Uliyoandika umerudi kwenye hoja yake ile ile! Wewe uko mjini, unaleta maelezo ya kimjini. Kwa mazingira yako huna sababu ya kushawishiwa kununua viatu, counters, mabegi, n.k. yeye alijikita kwenye uchumi wa kijijini.
Tusipende kujibu hoja kwa kujisahaulisha mazingira tulikotoka.
Ameuliza uhusiano wa viatu vyeusi na elimu, wewe unasemaje?
Ameuliza sababu ya kuzuia kiporo cha wali na kuruhusu mkate, wewe unasemaje?
 
Hoja zako ni dhaifu sana, kwanza kiukweli ni kuwa moja ya sababu ya viatu vyeusi kuwa na bei kubwa kulinganisha na vya rangi nyingine hasa vya watoto wa rika la shule ni hiyo ya kufanywa kama sare ya shule.

Wizara ya elimu ondoa hiyo sheria sare zimepitwa na wakati hasa viatu.
Kuzuia uniform ya viatu vyeusi hakuwezi kuwa suluhisho la viatu kushuka bei kwa sababu hata kama wanafunzi wataruhusiwa kuvaa viatu vya aina yoyote bado bei itapanda tu kwakuwa navyo vitakuwa ni sehemu ya uniform ya shule. Suluhisho pekee ni serikali kuweka mkazo na mikakati madhubuti ya kuhakikisha bidhaa zote za shule ikiwemo viatu vyeusi havipandishiwi bei kiholela na wafanyabishara hasa nyakati za ufunguzi wa shule zinapokaribia.
 
Kwani askari ote.wanatakiwa kuvaa kofia.
Kwani.kofia ndio zinazolinda?

Au askari.asipovaa kofia akiwa kzini akili inavurugika?

Kuna mavaz yasipowekewa utaratibu au sheria kwa kwenye kila taasisi au kiofisi utasababisha
Vijana na tamaduni zetu kuzidi kupotoka.

Hata yeye anapoingia bungeni kuna utaratibu wa uvaaji kawekewa.
Unafikili hata angeingia na dera bungeni hayo anayoyaonge yangefutika!?

Kila kitu kina utaratibu wake,wa walioasisi hayo wana maana yao na inaweza kua bora kuliko anachokitaka yeye.
Sahihi kabisa
 
Angekuwa Magufuli ndo ameongea aliyoyaongea kishimba ,ungemuunga mkono Magufuli..ndo akili zetu zinafuata upepo.
Utoro upo na viatu vyeusi tumevaa sana.
Logic ipo kwenye uchafu tu,umasaini wanafunzi wanavaa kataa mbuga ,na bado hawaendi shule.
 
Kila siku tunapiga malele nchi ya viwanda, Ngozi tunayo ya kumwaga, hivi hao VETA ama Sekta binafsi pamoja na mimi tumeshindwa kabisa kushirikiana na Serikali kutengeneza kiwanda cha viatu BORA kwa ajili ya wanafunzi wa shule za misingi na Sekondary nchini kwa bei nafuu ?

Kupatikana wa viatu vya shule kwa kila Halmashauri ( Kila Halmashauri nchini iwe na kiwanda chake cha sare za shule) kungeondoka kabisa utitiri wa viatu vya mtumba - Kwa mfano hapa Dar wazazi tunapigana vikumbo Manzese, Ilala na Kariakoo kuvitafuta kila January na July - fursa hii nayo hadi tufundishwe na mzungu?

Halmashauri zetu zinashindwaje kuteleleza hili? sasa ni nini maana a uniform kama kila mtoto atakwenda na viatu cha rangi tofauti na mwingine peku, mwingine ndala na mwingine yebo - kuna elimu hapo? Ubora wa elimu ni pamoja na utanashati alionayo mwanafunzi
 
Angekuwa Magufuli ndo ameongea aliyoyaongea kishimba ,ungemuunga mkono Magufuli..ndo akili zetu zinafuata upepo.
Utoro upo na viatu vyeusi tumevaa sana.
Logic ipo kwenye uchafu tu,umasaini wanafunzi wanavaa kataa mbuga ,na bado hawaendi shule.
Kuna sehemu hawaendi shule kwa sababu za kwenda jandoni. Kila sehemu ina sababu zake, na yeye kaeleza sababu za anakohusika! wewe unaleta sababu za umasaini. Kwa nini hamuelewi? Elimu gani muliyonayo?
 
Huyo mbunge falsafa zake wewe huwezi kuzipambanua. Nimekuwa namfuatilia sana na ninamwelewa katika kila hoja yake. Ni mtu wa tafakari na huyu mtu angesoma ingekuwa hatari sana.

Hoja yake kwenye mada hii ni kuwa sare na vikorombwezo vyake alivyovitaja vinamchango gani katika kupokea kile mwanafunzi anachofundishwa?

Hivi mwanafunzi akienda peku shuleni na akafundishwa vizuri hawezi kuelewa? Mimi nilikuwa Chuoni na genious mmoja ambaye hakuwahi kutumia daftari bali alikuwa anaandika dondoo tu kwenye vikaratasi tu na leo ana phd na hayuko hapa nchini. Kwa hoja za huyu mbunge nadhani kuna haja ya kuzitazama kwa mapana.

Mimi huwa najuliza ni nani alileta suala la kupamba kumbi za mikutano na sherehe mbali mbali. Lengo lilikuwa nini kama sio kutengeneza vipato haramu out of hayo mapambo kwani hayana mchango wowote juu ya kunogesha dhana ya mikutano au sherehe.

Ni gharama za bure kama ilivyokuwa kustage mkutano wa idara ya taasisi iliyopo DSM kwenda Zanzibar au Mwanza. Huyu mbunge ni mchumi kama ukimfuatilia kwa mfano suala la mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
 
Mkuu nakupa kongole nyingi kwa hoja ulizojenga juu ya ubora unaopaswa kuwepo ktk masuala ya elimu. Kuna kasumba mbaya imejitokeza hivi karibuni kwa viongozi kutoa ushauri wenye fikra za kimaskini na ufukara.

Kumejitokeza kasumba ya kuwataka watu kutokuwajibika ama kukumbatia vitu duni kama sababu ya kujionyesha kuwaonea huruma. Kibaya zaidi ni kutaka kuhadaa tabaka linalotawaliwa ili kuhalalisha "mentality" za kimaskini kuwa ndiyo uzalendo wenyewe.

Kuzaa ni wajibu mpana unaohusisha chakula, malazi, mavazi, elimu, bima na vitu vingime muhimu kwa ajili ya makuzi ya watoto na kujenga familia bora. Kisingizio cha kulalamikia gharama kwa wazazi hukuondoi wajibu huu.
Upo sahihi kabisa, tumegeuka wanyama kwa kutaka kuishi Kama wao Sasa situishi misituni bila nyumba na tusiwajibike kwa chochote, Kama tunataka kuishi Kama binadamu Basi tuishi kwa kanuni, Sheria, mazingira Bora na kuwajibika alafu mtu alipoambiwa asiyefanya kazi na asile na kula kwa jasho alitegemea nini atakapo leta viumbe duniani Kama siyo kuwajibika kwao?

Napinga kwa nguvu zote huo ujinga wa kutotafutia watoto mahitaji muhimu Kama hayo eti wale kipolo kwa uzembe wa wazazi wao, hata dini zinasisitiza kuhudumiwa wajane na watoto yatima maana ilionekana wao nguvu ya kufanya kazi imewaondokea.
 
Huyu kishimba si kama msukuma tu zero brain, huyu si ndo aliongea bungeni kwamba mtoto asipomsaidia mzazi wake ,basi mzazi akamshtaki mtoto, jinga kabisa hii mibunge ya CCM
Usisahau alishauri bangi iruhusiwe kulimwa na kuuzwa nchini!
 
Uniform ni muhimu...inaondoa matabaka mkiwa shuleni. Magereza si wana kiwanda cha kutengeneza viatu wawape ruzuku watengeneze viatu rasmi vya shule kwa bei ndogo.
 
Mkuu nakupa kongole nyingi kwa hoja ulizojenga juu ya ubora unaopaswa kuwepo ktk masuala ya elimu. Kuna kasumba mbaya imejitokeza hivi karibuni kwa viongozi kutoa ushauri wenye fikra za kimaskini na ufukara.

Kumejitokeza kasumba ya kuwataka watu kutokuwajibika ama kukumbatia vitu duni kama sababu ya kujionyesha kuwaonea huruma. Kibaya zaidi ni kutaka kuhadaa tabaka linalotawaliwa ili kuhalalisha "mentality" za kimaskini kuwa ndiyo uzalendo wenyewe.

Kuzaa ni wajibu mpana unaohusisha chakula, malazi, mavazi, elimu, bima na vitu vingime muhimu kwa ajili ya makuzi ya watoto na kujenga familia bora. Kisingizio cha kulalamikia gharama kwa wazazi hukuondoi wajibu huu.
Pamoja mkuu na wewe nakupa kongole kwa hoja na mchango uliotoa
 
Angekuwa Magufuli ndo ameongea aliyoyaongea kishimba ,ungemuunga mkono Magufuli..ndo akili zetu zinafuata upepo.
Utoro upo na viatu vyeusi tumevaa sana.
Logic ipo kwenye uchafu tu,umasaini wanafunzi wanavaa kataa mbuga ,na bado hawaendi shule.
Nafikiri ndio umeanza kunifuatilia leo. Mimi ni mtu ambaye niko 'straight' si muumini wa kufuata au kupinga kila kitu kinachosemwa na Rais kwakuwa yapo baadhi ya mambo namuunga mkono na mengine simuungi mkono, haya hapa ni baadhi


 
Back
Top Bottom