Napinga hoja zilizotolewa na Mbunge wa Kahama kuruhusu Wanafunzi kuvaa viatu vya aina yoyote na mambo mengine aliyoshauri Serikali

Alwatan kamba

Member
Nov 16, 2020
70
236
Leo kwenye uzinduzi wa ofisi ya makao makuu ya wilaya ya kahama, mbunge wa jimbo hilo mh. Kishimba ameiomba serikali kupiga marufuku wanafunzi kulazimishwa kununua madaftari aina ya 'counter book'. Pia ameiomba serikali kuruhusu wanafunzi kuvaa viatu vya rangi yoyote kwakuwa viatu havisaidii chochote kwenye elimu isipokuwa maarifa wanayopata shuleni.

Kwanza nianze kumpongeza mheshimiwa kishimba kwa kuwa kinara wa kuibua mambo mbali mbali ya kielimu na kuishauri serikali hatua za kuchukua.

Pili nakubaliana na mheshimiwa kishimba ya kwamba ni kweli viatu havisaidii chochote kwenye elimu ya mwanafunzi isipokuwa maarifa anayofundishwa na walimu wake.

Pamoja na kukubaliana na hoja hiyo, nampinga mheshimiwa mbunge kwa mambo yafuatayo;

HOJA YA VIATU VYEUSI
(i) viatu vyeusi ni sehemu ya sare za shule. Sare hizi husaidia kumtambulisha mwanafunzi pamoja na shule.

(ii) viatu vyeusi vinasaidia kupunguza utoro shuleni. Kwakuwa viatu vya rangi nyeusi havishiki uchafu kwa wepesi tofauti na rangi zingine mf. rangi nyeupe ni rahisi kwa wanafunzi kuhudhuria vipindi shuleni bila kusingizia kwamba viatu ni vichafu.

(iii) Rangi nyeusi ndio rangi inayopatika kwa wingi kuliko rangi nyingine kwenye viatu. Hivyo hata upatikanaji wake ni rahisi.

(iv) viatu rangi nyeusi husaidia kupunguza matabaka kwa wanafunzi. Kama nilivyotangulia kusema viatu ni sehemu ya sare 'uniform' hivyo vikiwa vya rangi ya kufanana kwa wanafunzi wote husaidia kupunguza tabaka kati ya mwanafunzi anayetoka kwenye familia ya wenye nacho na wasio nacho.

(v) viatu vyeusi ni sehemu ya mafundisho kwa wanafunzi kuhusu namna ya uvaaji wa kihaiba 'smart' na hivyo kuwafanya wawe na mwonekano nadhifu pindi wawapo shuleni na wamalizapo masomo.

(vi) kwakuwa hoja ya mheshimiwa mbunge imejikita kwenye kuwapunguzia wazazi gharama na endapo hoja hiyo ikafanyiwa kazi tusitegemee itaishia hapo.

Endapo hoja hiyo itatatuliwa tutarajie wazazi kwenda mbali zaidi kudai na uniform zingine ziondolewe kwa sababu nazo ni gharama hivyo mwisho wa siku kila kitu kitafanyike nje ya utaratibu na matabaka kwa wanafunzi yataongezeka.


HOJA YA MADAFTARI AINA YA COUNTER BOOK
Mheshimiwa mbunge amelalamika kuwa daftari aina ya counter book zinauzwa bei kubwa hivyo zinawaongezea wazazi gharama. Kwa mtazamo wangu naona ni sahihi wanafunzi kutumia counter books kwa sababu;

(i) daftari zinazouzwa kati ya 250 - 300 ni ndogo sana kiasi kwamba mwanafunzi akiandikia kipande kidogo cha mada 'sub topic' linaisha hivyo ni sahihi kabisa wanafunzi kutumia counter books kwakuwa zina nafasi 'space' kubwa na kurasa 'pages' nyingi na haziishi mapema.

(ii) counter books zinasaidia kupunguza usumbufu kwa wazazi kununua madaftari kila wakati kwakuwa zinachukua muda mrefu aghalabu mwaka mmoja na ushee bila kuisha lakini daftari ndogo ndani ya week 2-3 au hata week moja haizimalizi hivyo kufanya wazazi kununua daftari kila wakati.

(iii) counter books zinasaidia kupunguza migogoro ya kifamilia kati ya mwanafunzi na wazazi. Kwakuwa daftari ndogo hujaa mapema kuna wakati wazazi wanakuwa 'reluctant' na kuwashutumu watoto wao kwa matumizi mabaya ya madaftari jambo ambalo hupelekea baadhi ya wazazi kuacha kabisa kuwanunulia. Ikumbukwe migogoro kama hii ikitokea hata 'performance' ya mwanafunzi shuleni hushuka kwa sababu ya ukosefu wa nyenzo muhimu 'madaftari' ya kujifunzia.

(iv) kwakuwa counter books hununuliwa kwa gharama kubwa hata utunzaji wake wanafunzi huuzingatia sana tofauti na daftari ndogo ndogo.

(v) kutokana na daftari ndogo ndogo kujaa haraka, hulazimu wazazi kununua nyingi kwa mwaka ambapo kimahesabu gharama inayotumika kuzinunulia inakuwa sawa au hata kuzidi kabisa gharama iliyotumika kununulia counter book moja.

HOJA YA MABEGI
Mheshimiwa mbunge pia amedai ni gharama wazazi kuwanunulia wanafunzi mabegi ya shule.

Yamkini inaweza kuwa hoja nzuri lakini mheshimiwa mbunge akumbuke kuwa mabegi ni kwaajili ya usalama wa vifaa vya mwanafunzi mwenyewe na vifaa au mali anazo azima mwanafunzi shuleni kama vile vitabu. Ili kuhakikisha vifaa hivyo vinakuwa salama muda wote hasa kwa vipindi korofi kama vipindi vya mvua au hatari yoyote ya upotevu na uharibifu ni vyema vikahifadhiwa kwenye begi.

Ushauri wangu: kufuatia hoja zilizotolewa na mheshimiwa mbunge na kwakuwa hoja zake zote zimelenga eneo moja la gharama nikiwa kama mdau wa elimu nashauri serikali iweke mikakati madhubuti ya kudhibiti upandaji holela wa bei za vifaa vya shule hasa nyakati vipindi vya shule vinapokaribia kwakuwa ndio chanzo cha gharama kuwa juu. Namaanisha tabia ya baadhi ya wafanya biashara wachache ambao sio waaminifu kuuza vifaa vya shule kwa bei kubwa pindi shule zinapokaribia kufunguliwa ikomeshwe.
 
Hoja zako ni dhaifu sana, kwanza kiukweli ni kuwa moja ya sababu ya viatu vyeusi kuwa na bei kubwa kulinganisha na vya rangi nyingine hasa vya watoto wa rika la shule ni hiyo ya kufanywa kama sare ya shule.

Wizara ya elimu ondoa hiyo sheria sare zimepitwa na wakati hasa viatu.
 
Hoja zako hazijashiba vilivyo.

1) lengo la elimu ni kumtunza mtu kuyatawala mazingira yake...utofauti wa kipato ni sehemu ya mazingira ya wanafunzi... Mfumo tulionao ni wa kijima. Watoto hawahitaji sare kujifunza wanahitaji mazingira rafiki.

Viatu vyeusi kutokana na kuwa mandatory kwa ajili ya sare za shule vimekuwa ghali sana.. lakini wangeruhusu watoto wavae kwa usafi na unadhifu viatu au nguo zozote shuleni nadhani ingekuwa sahihi na kuwaondolea uzito wa gharama wazazi.

2) Madaftari serikali ingetoa guidelines kwa wazalishaji wa madaftari maalumu kwa ajili ya wanafunzi wa shule (Exercise books) zenye karatasi za kutosha na ukubwa... Kisha ziwapunguzie/kuwaondolea kodi wazalishaji kwenye madaftari haya pekee.

3) Shule zisiruhusiwe kubwa kubwa sana.. angalau kwa shule kubwa isizidi wanafunzi 105 kwa darasa.. ili walimu waweze kumudu pressure za kuwahudumia wanafunzi kwa umakini.
 
suala la uniform nibkatika kumfundisha mtoto nidhamu.ndio mana majeshin hakuna kuchekeana ni uniform kwa kwenda mbele.
huwa najiuliza maulaya na marekan kuan shule za public kule matoto yanajivalia kila mtu anavojiskia ila kwann zile shule za private unakuta matoto ya kizungu yana uniform na ni very strict na ni watoto wa matajir sana.?? why
 
suala la uniform nibkatika kumfundisha mtoto nidhamu.ndio mana majeshin hakuna kuchekeana ni uniform kwa kwenda mbele.
huwa najiuliza maulaya na marekan kuan shule za public kule matoto yanajivalia kila mtu anavojiskia ila kwann zile shule za private unakuta matoto ya kizungu yana uniform na ni very strict na ni watoto wa matajir sana.?? why
Hatuna namna nyingine ya kufunzana nidhamu!?

Mfano kukaa na wananchi wa eneo husika kupata maoni yao ili sare iwe kile wanachoweza kukipata kwa urahisi(if there is such a thing)

Maana shida inakuwa hatutaki kufanya upatikanaji wa elimu kuwa a fun experience kwa mtoto na mzazi.. imekuwa ya kimtego mtego tu.. fedha ziwatokeeeee wazazi mpaka wanachukia kupeleka Watt shule..

Kwann badala ya Kaptula ya buluu, ya tetron wasivae kaptula ya Khaki ya kadet, au bluu ya jeans.. akitoka shule hata mtaani anavaa tu... Au Kwann wavae mashati meupe kila siku, kwamba kutunza mashati meupe wavae siku za Jumatatu tuu na siku nyingine za matukio muhimu kama mitihani na mahafali.

Siku nyingine zote wavae mashati mengine ya kawaida au tisheti zenye Nembo ya shule wanayoweza kuwekewa kwa sh. Elfu moja shuleni.!?

Nawaza tu Bibi yangu... Supu na chapati zina mambo
 
Nimekuwa nikimuunga mkono, hoja zake nyingi huwa ni hoja fikirishi ila hili la ushauri wa viporo na viatu kwa wanafunzi nasema hapna tunaweza leta maafa mashuleni hasa issue ya chakula. Embu fikiria mwanafunzi kaenda na baga na mwingine kabeba makukuru, au mwanafunzi mwingine kavaa yebo na mwingine kavaa buti la Jeje hilo darasa litakuwaje?
 
Nimekuwa nikimuunga mkono, hoja zake nyingi huwa ni hoja fikirishi ila hili la ushauri wa viporo na viatu kwa wanafunzi nasema hapna tunaweza leta maafa mashuleni hasa issue ya chakula. Embu fikiria mwanafunzi kaenda na baga na mwingine kabeba makukuru, au mwanafunzi mwingine kavaa yebo na mwingine kavaa buti la Jeje hilo darasa litakuwaje?
Lakini huo si ndio uhalisia!? Hatulingani...
Watoto wajifunze mapema.. ndio maana wakifika makazini ni ushirikina na kuchomeana kwa kwenda mbele.. hatuwafunzi juu yakuappreciate uhalisia.. mapema
 
Uko sahihi mkuu japo nimekumbuka January hii nikiwa sido nasagula/natafuta viatu vya mtumba pembeni yangu alikuwa mama mmoja anahangaika kutafuta kiatu cha shule kwa ajili ya mwanawe akafanikiwa kupata kiatu cha ngozi cheupe tatizo likaja siyo rangi inayohitajika shuleni ikabidi nimshauri akakipige rangi nyeusi tu.
 
Mtoa maada, mtoa maada. Yamkini mm ni zuzu. Swali ushawahi kuwa familiar na mtot wa mzazi masikini?
Hoja zako zimejikita zaidi kutetea upande mmoja na kunufaisha pande zingne!,
Anyway ngoja niache tu mana hii haisaidiii
Mbuge aliongea facts 97%
Wewe umekubali na kuzipga facts za mbuge? Hii inawezekanaje mkuu?
Na binafs hoja zako nazipa 48% kuziunga.
The strong reason is ELIMU. mengine mazengwe tu yanayaweza kumzuia huyu wa kipato kidg akashindwa kuipata hii formal ed💥
 
Kwani askari ote.wanatakiwa kuvaa kofia.
Kwani.kofia ndio zinazolinda?

Au askari.asipovaa kofia akiwa kzini akili inavurugika?

Kuna mavaz yasipowekewa utaratibu au sheria kwa kwenye kila taasisi au kiofisi utasababisha
Vijana na tamaduni zetu kuzidi kupotoka.

Hata yeye anapoingia bungeni kuna utaratibu wa uvaaji kawekewa.
Unafikili hata angeingia na dera bungeni hayo anayoyaonge yangefutika!?

Kila kitu kina utaratibu wake,wa walioasisi hayo wana maana yao na inaweza kua bora kuliko anachokitaka yeye.
 
Kama ni kwa wanafunzi wa primary counter book might not be very suitable for them. Tunajua mazingira ya shule zetu za msingi; madaftari ya saizi ya kati ni appropriate kwao. Kwa sekondari counter books sawa.
 
ACHA watoto wagonge raba.
Mimi nilikuwa naingia shule na raba.
Japo Kila siku ugomvi na walimu ulikuwa hauishi.
Kuna siku walitupokonya viatu nilitembea kwa miguu mpaka home
 
Back
Top Bottom