PreGE2025 Nape: Wapinzani wanapinga lakini wanapanga foleni kuchukua pembejeo za bure

PreGE2025 Nape: Wapinzani wanapinga lakini wanapanga foleni kuchukua pembejeo za bure

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye, amesema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi mwenye usikivu mkubwa kwa wakulima wa korosho, akisisitiza kuwa pembejeo za bure alizotoa kupitia serikali yake ni uthibitisho wa dhamira ya kweli ya kuwawezesha wakulima nchini.

Akizungumza Aprili 12, 2025 wilayani Nachingwea mkoani Lindi, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika ziara ya Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla, Nape amesema kuwa serikali iliyoongozwa na Rais Samia imeleta mageuzi makubwa katika sekta ya korosho kwa kutoa pembejeo bure tangu mwaka 2021.

“Wakati ule tulizozana bungeni mpaka wanajeshi wakaja hapa kukusanya korosho. Baadaye tukajadili, serikali ikatuelewa, tena aliyetuelewa sana ni Rais Samia. Akaamua wakulima wasitoe hela mfukoni, akaleta bilioni 58.4 na tukagawa pembejeo za bure kwa wakulima,” amesema Nape.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mbunge huyo ameongeza kuwa hata baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliokuwa wakipinga mfumo wa korosho na kushutumu serikali, walijitokeza kuchukua pembejeo hizo, akisema: “Wakawa wanapanga foleni kuchukua pembejeo ya Samia, kweli au si kweli? Hawaulizwi kadi ya chama. Mama hana ubaguzi.”

Akitetea juhudi za Rais Samia, Nape amesema viongozi wa upinzani hawapaswi kubeza mafanikio yanayoonekana kwani wao na wafuasi wao pia wananufaika na huduma za afya, elimu na kilimo zinazotolewa na serikali ya CCM.

 
Hili nalo ni zezeta, kwani hizo pembejeo ni za ssm au za serikali, hii nchi elimu imetupitia kushoto.
Mlioko karibu nahuyo dogo angalieni hizo pembejeo kama zina nembo ya ssm
Ulevi wa madaraka ukipituka matokeo yake ndio haya mtu unakua unaonge uharo tu.
Na wanaomsikiliza wakijiangalie kwenye kioo kama kweli wamevaa au la!
 
Ndio muwapige goli la mkono?
 
Katika zero brain 🧠 taifa hili limewahi kuwa nao nape ni mmoja wapo.
 
Wanaopinga wanadaiwa na kulipa kodi pia??
 
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye, amesema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi mwenye usikivu mkubwa kwa wakulima wa korosho, akisisitiza kuwa pembejeo za bure alizotoa kupitia serikali yake ni uthibitisho wa dhamira ya kweli ya kuwawezesha wakulima nchini.

Akizungumza Aprili 12, 2025 wilayani Nachingwea mkoani Lindi, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika ziara ya Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla, Nape amesema kuwa serikali iliyoongozwa na Rais Samia imeleta mageuzi makubwa katika sekta ya korosho kwa kutoa pembejeo bure tangu mwaka 2021.

“Wakati ule tulizozana bungeni mpaka wanajeshi wakaja hapa kukusanya korosho. Baadaye tukajadili, serikali ikatuelewa, tena aliyetuelewa sana ni Rais Samia. Akaamua wakulima wasitoe hela mfukoni, akaleta bilioni 58.4 na tukagawa pembejeo za bure kwa wakulima,” amesema Nape.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mbunge huyo ameongeza kuwa hata baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliokuwa wakipinga mfumo wa korosho na kushutumu serikali, walijitokeza kuchukua pembejeo hizo, akisema: “Wakawa wanapanga foleni kuchukua pembejeo ya Samia, kweli au si kweli? Hawaulizwi kadi ya chama. Mama hana ubaguzi.”

Akitetea juhudi za Rais Samia, Nape amesema viongozi wa upinzani hawapaswi kubeza mafanikio yanayoonekana kwani wao na wafuasi wao pia wananufaika na huduma za afya, elimu na kilimo zinazotolewa na serikali ya CCM.

Nape Nnauye ni zuzu kabisa, yaani hajui kwamba pembejeo hununuliwa kwa kodi ambazo wananchi wote tumechangia bila kujalisha itikadi za vyama
 
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye, amesema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi mwenye usikivu mkubwa kwa wakulima wa korosho, akisisitiza kuwa pembejeo za bure alizotoa kupitia serikali yake ni uthibitisho wa dhamira ya kweli ya kuwawezesha wakulima nchini.

Akizungumza Aprili 12, 2025 wilayani Nachingwea mkoani Lindi, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika ziara ya Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla, Nape amesema kuwa serikali iliyoongozwa na Rais Samia imeleta mageuzi makubwa katika sekta ya korosho kwa kutoa pembejeo bure tangu mwaka 2021.

“Wakati ule tulizozana bungeni mpaka wanajeshi wakaja hapa kukusanya korosho. Baadaye tukajadili, serikali ikatuelewa, tena aliyetuelewa sana ni Rais Samia. Akaamua wakulima wasitoe hela mfukoni, akaleta bilioni 58.4 na tukagawa pembejeo za bure kwa wakulima,” amesema Nape.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mbunge huyo ameongeza kuwa hata baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliokuwa wakipinga mfumo wa korosho na kushutumu serikali, walijitokeza kuchukua pembejeo hizo, akisema: “Wakawa wanapanga foleni kuchukua pembejeo ya Samia, kweli au si kweli? Hawaulizwi kadi ya chama. Mama hana ubaguzi.”

Akitetea juhudi za Rais Samia, Nape amesema viongozi wa upinzani hawapaswi kubeza mafanikio yanayoonekana kwani wao na wafuasi wao pia wananufaika na huduma za afya, elimu na kilimo zinazotolewa na serikali ya CCM.

Kuna tofauti kubwa Kati ya uchama na utaifa
 
Hapo kwa akili yake anaona kamkosha sa100 kwelikweli, kwamba atamkumbuka kwenye teuzi!
 
Back
Top Bottom