Nape: Wapiga kelele wengi hawajui jinsi watu wanavyoishi huko vijijini

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
085f1ff72fe85c576559deb5934dcddc.jpg
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amefunguka na kusema kuna tofauti kubwa sana kati ya watu wanaoishi Dar es salaam na watu ambao wanaishi katika vijiji mbalimbali na kusema watu wanaopiga kelele hawajui jinsi watu wanavyoishi huko vijijini.

Nape Nnauye ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram na kusema kuwa ukipata nafasi ya kufanya kazi vijijini ndiyo unaweza kuona utofauti mkubwa uliopo.

"Ukikaa na kufanya kazi huku vijijini, utaona utofauti mkubwa uliopo kati ya Dar es salaam na Tanzania, wapiga kelele wengi hawajui maisha haya", alisema Nape Nnauye.

Mbunge huyo ambaye sasa yupo kwenye ziara mbalimbali ndani ya jimbo lake amekuwa akikutana na changamoto mbalimbali kutoka kwa wananchi wake ambao wengi wao ni watu wa maisha ya kawaida.

Nape alipokutana na wakulima waliweza kuishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuweza kuwapelekea mbolea ya Sulpha ya bure kwa ajili ya mikorosho yao lakini alidai kuwa wakulima hao walilalamika kwa mbolea hiyo kutokuja kwa wakati na kwa kiasi cha kutosha.
 
Ni kombora hili....kutoka Korea Kaskazini kwa dogo Kim
 
Mbunge wa Mtama, Nape Moses Nnauye amefunguka na kusema kuna tofauti kubwa sana kati ya watu wanaoishi Dar es Salaam na watu ambao wanaishi katika vijiji mbalimbali na kusema watu wanaopiga kelele hawajui jinsi watu wanavyoishi huko vijijini.




Nape.jpg

Nape Nnauye ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram na kusema kuwa ukipata nafasi ya kufanya kazi vijijini ndiyo unaweza kuona utofauti mkubwa uliopo

"Ukikaa na kufanya kazi huku vijijini, utaona utofauti mkubwa uliopo kati ya Dar es salaam na Tanzania, wapiga kelele wengi hawajui maisha haya" alisema Nape Nnauye

Mbunge huyo ambaye sasa yupo kwenye ziara mbalimbali ndani ya jimbo lake amekuwa akikutana na changamoto mbalimbali kutoka kwa wananchi wake ambao wengi wao ni watu wa maisha ya kawaida, Nape alipokutana na wakulima waliweza kuishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuweza kuwapelekea mbolea ya Sulpha ya bure kwa ajili ya mikorosho yao lakini alidai kuwa wakulima hao walilalamika kwa mbolea hiyo kutokuja kwa wakati na kwa kiasi cha kutosha.
 
Back
Top Bottom