Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye, jana akihutubia Mkutano wa Kampeni za Ubunge katika Kijiji cha Mbizi, Jimbo la Buyungu, wilayani Kakonko, alidai kuwa, CCM ilimpitisha Dk. John Pombe Magufuli mwaka 2015 kuwania urais kwa kuwa, walimtaka mtu ambaye angeweza kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za Serikali.Vilevile, mtu asiyewachekea wezi na pia kubana mianya yote ya rushwa.
Aliwaonya Wapinzani kuwa, kutokana na kazi nzuri inayoendelea kufanywa na Rais Magufuli, Wapinzani wanatakiwa kuacha Siasa zao za kipindi kilichopita kwani wakiendelea watakimbiwa na wanachama wote.
Alidai wanaoilalamikia Serikali ya Awamu ya Tano, ni wale waliozoea kuiba fedha za wananchi ambao kwa sasa wamebanwa. Huyu ndiye Kiongozi anayehitajika.... hakuna jambo ambalo Watanzania wanaweza kumsema vibaya Rais Magufuli.
Aliwaonya Wapinzani kuwa, lengo la kuwepo kwa Mfumo wa Vyama vingi ni kuikosoa Serikali, siyo kuipinga inapofanya maendeleo.
View attachment 828430
kwa kweli kwa hili nape kajidhalilisha sana.....................Unafiki !View attachment 828939
Huyo naye anaongea tu kwa sababu ni siasa lakini moyoni kuna kitu kinamuumiza sana kuhusu huyo huyo mtu anayemfagilia
Hao ni opportunists politicians ....!!Puwer politics. Political sciience inasema ukuwa na lengo B huku watu wako wana lengo A basi unaingia na lengo A ili u win support wakishakupa nafasi unarudia lengo lako B. Lakini maneno havunji mfupa japo yaweza kuchekesha au kumliza mtu!
Kwa kweli!Haijalishi chama alichopo ila Nape anaijua siasa
Wana siasa wote wako hivyo!Hao ni opportunists politicians ....!!
Kitu gani kinamwumiza, mmeishiwa sera hadi mnaanza kusemea watu mioyoHuyo naye anaongea tu kwa sababu ni siasa lakini moyoni kuna kitu kinamuumiza sana kuhusu huyo huyo mtu anayemfagilia
Mbowe sio DJ wewe,umekuja lini Dar toka kijijini kwenu. Unawajua akina Chris Phabby,Kalikali, et al,ulikuwa bush gani wakati huo.BONGOLALA, kweli bana afadhali Mbowe ni DJ, Msigwa ni mchungaji; Zitto ni mwanasiasa nk
Siyo kutegemea bali ni wajibu wake wa kumsifia Rais Magufuli na Serikali yake. Asipoisifia Serikali inakuwa unusual.Kwahiyo ulitegemea nape aiponde ccm?
Wanatamani wabadili maji yawe gesi, rangi nyeusi ing'ae kama sufi.... aaahhh!! Watapata tabu sana.Kitu gani kinamwumiza, mmeishiwa sera hadi mnaanza kusemea watu mioyo